Saturday, September 9, 2023

NYERERE SUPER CUP TIMU ZAKABIDHIWA VIFAA



Katika kuelekea kumbukizi ya Miaka 24 ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani ikiwakirishwa na Ndugu Omary Abdull Katibu wa Taasisi hiyo Mkoa wa Pwani Leo Tarehe 9.9.2023 imekabidhi Vifaa vya michezo ya mashindano ya NYERERE SUPER CUP Jezi seti Moja na Mpira Mmoja Kwa Kila Timu, Tshirt za maandalizi ya Ufunguzi, Zawadi za Mashindano na Mpira Kwa Chama Cha Mpira Rufiji Kwa Mkuu wa wilaya ya Rufiji Mhe Meja Edward Gowele ili akabidhi Kwa Timu sita hizo zitakazoshiriki kwa upande wa Rufiji 1. NGORONGO 2.UTETE,3.MGOMBA, 4.MUHORO 5.UMWE na 6.MKONGO yatakayoshirikisha Wilaya Mbili KIBITI na RUFIJI yatanza kutimua vumbi kuanzia tarehe 23.9.2023 na kutamatika 12.10.2023 Wadhamini wa mashindano hayo NBC bank, NSSF, TANGANYIKA ORGANIC na UNGA AFYA LISHE kauli mbiu ya Mashindano UMOJA NA AMANI VITAWALE MITANO TENA

No comments:

Post a Comment