Na John
Gagarini, Chalinze
WATU watatu wakiwemo
mtoto wa miezi minne na wa mwaka mmoja wamekufa huku watu wawili wakinusurika
kifo baada ya mtumbwi waliokuwa wakisafiria kuzama kwenye mto Ruvu.
Akizungumza
na waandishi wa habari kamanda wa polisi mkoani Pwani Jonathan Shana alisema
kuwa licha ya watu hao kubainika kufa dereva wa mtumbwi huo hajulikani alipo.
Shana alisema
kuwa tukio hilo lilitokea Agosti 5 majira ya saa 4:00 asubuhi wakati watu hao walipokuwa wakijaribu kuvuka mto kutoka Vigwaza kwenda Mlandizi kwenye mto Ruvu
wilaya ya kipolisi Chalinze.
“Ajali hiyo
imepoteza maisha ya watoto wawili ambao ni Nusrat Haji miezi minne na Feisal
Hamza mwenye umri wa mwaka mmoja na nusu pamoja na Sikuzani Musa (41) ambaye
mwili wake bado haujapatikana,” alisema Shana.
Alisema kuwa
walionusurika ni Zuwena Ramadhan (29) na Tero Mziray (20) ambapo dereva wa
mtumbwi huo hajulikani alipo na inaaminika hakufa maji.
“Chanzo cha
mtumbwi huo kuzama bado kinachunguzwa na miili ya marehemu imefanyiwa uchunguzi
na kukabidhiwa ndugu zao kwa ajili ya mazishi,” alisema Shana.
Aliwataka
wamiliki wa vyombo hivyo kuhakikisha vinakuwa kwenye hali nzuri ili kuepukana
na ajali kama hizo ambazo zinapoteza uhai wa watu kutokana na ubovu.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment