Na John
Gagarini, Kibaha
CHAMA cha Netiboli
mkoa wa Pwani kimefanya uchaguzi wa kuwachagua viongozi wake ambao wataongoza
kwa kipindi cha miaka minne ambapo Fatuma Mgeni amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa
chama hicho.
Uchaguzi huo
ambao ulifanyika mjini Kibaha na kusimamiwa na kamati ya michezo ya mkoa
ikiongozwa na ofisa michezo wa mkoa huo Grace Bureta ulimrudisha madarakani
mwenyekiti huyo.
Wengine
waliochaguliwa ni makamu mwenyekiti Faraji Makale, katibu ni Steven Mzee,
katibu msaidizi ni Rehema Kiharaza, mweka hazina Octavian Chuma.
Kwa upande wa
wawakilishi mkutano mkuu taifa ni Ndimbumi Ifuge, Lonjin Mzava, Omega Shuma,
Witnes Kitereja na Grace Paschal.
Akiwaasa
viongozi waliochaguliwa ofisa michezo huyo aliwataka viongozi hao kuwa kitu
kimoja na kushirikiana ili kuinua mchezo huo kwenye mkoa kwa manufaa ya
wachezaji wa mchezo huo.
Bureta
alisema kuwa uongozi imara ndiyo utakaofanikisha kukabili changamoto mbalimbali
zilizopo za kuuboresha mchezo huo ambao ulikuwa maarufu kwenye mkoa wa Pwani
kwa miaka ya nyuma.
“Muwe na
maamuzi ya pamoja na si ya mtu mmoja na kusitokee akafanya kama ni mali yake
hali ambayo itasababisha mchezo huo ushindwe kupiga hatua,” alisema Bureta.
Kwa upande
wake mwenyekiti wa chama hicho Fatuma Mgeni alisema kuwa moja ya vitu
atakavyovifanyia kazi ni kufanya mafunzo kwa walimu wa mchezo huo ili wajue
sheria mpya za mchezo huo ambazo zilifanyiwa marekebisho mwaka 2016 nchini
Afrika Kusini.
Mgeni alisema
kuwa mafunzo hayo yatakuwa kwa walimu wa mashule, vyuo na kwa wadau mbalimbali
wanaoupenda mchezo huo na wanaotaka kuwa walimu wa kufundisha netiboli.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment