Na John
Gagarini, Kibaha
WADAU wa watu
wenye ulemavu kwenye Halmashauri ya Mji Kibaha wameiomba Halmashauri hiyo
kutenga asilimia moja ya mapato ya ndani kwa ajili ya kukabili changamoto za
ulemavu.
Hayo yalisemwa
na Methew Chungu mwezeshaji wa mafunzo
yaliyoandliwa na Shirikisho la Watu wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA) Kibaha
Mjini kwa wadau wa huduma za afya kwa watu wenye ulemavu.
Chungu alisema
kuwa mapato hayo yangesaidia kuwapatia huduma mbalimbali watu wenye ulemavu zikiwemo
za kiafya, elimu, kiuchumi na huduma nyingine za kiutu.
Naye katibu
wa SIVYAWATA Kibaha Mjini Happiness Matagi alisema kuwa kwa sasa changamoto za
upataji huduma kwa watu wenye uelemavu zimepungua ambapo kumwona daktari kwa ni
bure.
Matagi
alisema kuwa kupitia kituo chao cha watu wenye ulemavu kilichopo Kwa Mfipa
wanatoa huduma mbalimbali za kiafya hasa kwa wale walemavu wa viungo pamoja na
shughuli za ujasiriamali.
“Pale watu
wenye ulemavu wanafanya shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na kufuma, kushona
nguo na mradi wa matofali ambao uko mbioni kuanza lengo kuwakwamua watu wenye
ulemavu ili wasijione wanyonge na kuachana na tabia ya kuomba ambayo itawafanya
washindwe kujitegemea,” alisema Matagi.
Kwa upande
wake mwakilishi wa mganga mkuu wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha Dk Mariamu Mgaya
alisema kuwa watu wenye ulemavu wamekuwa wakisaidia ili kuhakikisha wanapata
huduma za afya bila ya usumbufu kwa kuwapa kipaumbele.
Akijibu
baadhi ya hoja ofisa mipango wa Halmashauri ya Mji Kibaha Amkauane Ngilangwa alisema
kuwa katika bajeti iliyopitishwa watu wenye ulemavu wametengewa kiasi cha
shilingi milioni 10.
Ngilangwa
alisema kuwa pia wanapatiwa vitu mbalimbali ikiwa ni pamoja na mafuta ya
kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ngozi albino ili ngozi zao zisiharibike na
fimbo kwa ajili ya wasioona.
No comments:
Post a Comment