Thursday, August 3, 2017

UCHAGUZI CHAMA CHA NETIBOLI PWANI

Na John Gagarini, Kibaha

CHAMA Cha Netiboli mkoa wa Pwani (CHANEPWA) kinatarajia kufanya uchaguzi wake Agosti 5 mwaka huu.

Hayo yalisemwa mjini Kibaha na ofisa michezo mkoa wa Pwani Grace Bureta na kusema kuwa uchaguzi huo utafanyika Tanita mjini Kibaha.

Bureta alisema kuwa mchakato wa uchaguzi huo unaendelea ambapo usaili unatarajiwa kufanyika wiki hii ili kuwapitisha wadau watakaogombea nafasi mbalimbali.

“Mchakato unaendelea na tunasubiri taarifa kutoka kwenye wilaya za mkoa wetu ili watuletee majina ya wagombea na baadaye tufanye usaili wiki hii ili kuwapata wale wenye sifa,” alisema Bureta.
Alisema kuwa fomu zilianza kutolewa tangu Aprili lakini baadye uchaguzi huo uliahirishwa kutokana na sababu mbalimbali ambapo sasa unafanyika kesho endapo taratibu zitakuwa ziko sawa.

“Fomu zote zinatakiwa zirejeshwe kwa maofisa michezo wa wilaya ambao nao wataziwasilisha mkoani kwa ajili ya taratibu za uchaguzi huo ambao utawaweka madarakani viongozi wapya kwa kipindi cha miaka minne,” alisema Bureta.

Aidha alisema kuwa uchaguzi huo unatarajiwa kusimamiwa na kamati ya michezo ya mkoa na kuwataka wagombea hao kutimiza taratibu ili wawanie nafasi hizo.


Mwisho. 

No comments:

Post a Comment