Na John Gagarini, Chalinze
MBUNGE wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete ameipongeza serikali kwa
kuipeleka kamati ya Maliasili na Utalii kufuatilia changamoto zinazokabili
Vijiji vinavyopakana na Hifadhi.
Aliyasema hayo kwenye kikao cha mwaka cha Madiwani wa Halmashauri ya
Chalinze na kusema kuwa kumekuwa na changamoto nyingi kwenye vijiji hivyo.
Ridhiwani alisema kuwa baadhi ya changamoto ni mipaka baina ya vijiji
hivyo na mbuga hiyo hali ambayo imejenga mahusiano mabaya baina ya vijiji na
mbuga hiyo.
“Kamati hyo kuja itakuwa ni moja ya njia za kupata ufumbuzi wa
changamoto nyingi zilizopo kwa pande zote na itasidia kupunguza tatizo
lililopo, ” alisema Ridhiwani.
Alisema kuwa sehemu ya Hifadhi ya Wami Mbiki ambayo ni njia ya kupita
wanyama nayo imeingiliwa hivyo kuna haja ya hatua kuchukuliwa ili kunusuru
maeneo hayo.
Naye mwenyekiti wa Halmashauri Said Zikatimu alisema kuwa kamati hiyo
itasaidia sana kuleta suluhu kwani migogoro kwenye vijiji vilivyojirani na
hifadhi ni kero kubwa.
Zikatimu alisema kuwa wanaafiki kamati hiyo kuja na kusikiliza ili
kutatua changamoto kwenye vijiji husika ili navyo vipate haki zao.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment