Sunday, August 13, 2017

MBUNGE APONGEZA KAMATI MALIASILI UTALII







Na John Gagarini, Chalinze

MBUNGE wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete ameipongeza serikali kwa kuipeleka kamati ya Maliasili na Utalii kufuatilia changamoto zinazokabili Vijiji vinavyopakana na Hifadhi.

Aliyasema hayo kwenye kikao cha mwaka cha Madiwani wa Halmashauri ya Chalinze na kusema kuwa kumekuwa na changamoto nyingi kwenye vijiji hivyo.

Ridhiwani alisema kuwa baadhi ya changamoto ni mipaka baina ya vijiji hivyo na mbuga hiyo hali ambayo imejenga mahusiano mabaya baina ya vijiji na mbuga hiyo.

“Kamati hyo kuja itakuwa ni moja ya njia za kupata ufumbuzi wa changamoto nyingi zilizopo kwa pande zote na itasidia kupunguza tatizo lililopo, ” alisema Ridhiwani.

Alisema kuwa sehemu ya Hifadhi ya Wami Mbiki ambayo ni njia ya kupita wanyama nayo imeingiliwa hivyo kuna haja ya hatua kuchukuliwa ili kunusuru maeneo hayo.

Naye mwenyekiti wa Halmashauri Said Zikatimu alisema kuwa kamati hiyo itasaidia sana kuleta suluhu kwani migogoro kwenye vijiji vilivyojirani na hifadhi ni kero kubwa.

Zikatimu alisema kuwa wanaafiki kamati hiyo kuja na kusikiliza ili kutatua changamoto kwenye vijiji husika ili navyo vipate haki zao.


Mwisho.

No comments:

Post a Comment