Thursday, August 3, 2017

PICHA YA NDEGE WAPATA ENEO UJENZI SHULE YA SEKONDARI

Na John Gagarini,Kibaha

KATA ya Picha ya Ndege imepata eneo lenye ukubwa wa hekari 11 kwa ajili ya ujenzi wa shule ya sekondari ya Kata ambapo kwa sasa wanafunzi wanaotoka kata hiyo wanasoma shule ya sekondari ya kata kwenye mtaa wa Mkuza.

Hayo yalisemwa na Diwani wa Kata hiyo Robert Machumbe wakati wa mkutano wa kata uliofanyika kwenye shule ya Msingi ya Lulanzi na kusema kuwa eneo hilo limepatikana kutokana na jitihada zake na wananchi.

Machumbe alisema kuwa licha wanafunzi wanaotoka kwenye kata yake wanasoma kwenye mazingira magumu kwani darasa moja linawanafunzi 450 hali ambayo inafanya usomaji kuwa mgumu.

“Watoto wetu wanapata shida kwanza kule ni mbali na pia madarasa yao yamejaa wanafunzi hivyo hupunguza ari ya usomaji na ufaulu kuwa mdogo,” alisema Machumbe.

Naye Thomas Raymond alisema kuwa ujenzi wa shule hiyo itakuwa mkombozi kwa wanafunzi wanaotoka kwenye kata hiyo ambayo ni mpya ikiwa haina shule yake ya sekondari.
Raymond alisema kuwa wao wako tayari kuchangia ujenzi wa shule hiyo mara wakati utakapofika ili kuhakikisha shule hiyo inajengwa haraka kwenye kata yao.

Mwisho.


No comments:

Post a Comment