![]() |
Moja ya watu wanaotuhumiwa kuwa ni mhamiaji haramu toka nchi ya Ethiopia akiwekewa uji pembeni ni askari akisubiri kupewa uji kwa ajili ya kuwapa watuhumiwa hao. |
![]() |
Baadhi ya waethiopia wanaotuhumiwa kuingia nchini bila ya kibali wakipata kifungua kinywa cha uji. |
![]() |
Askari akiwapatia mikate watu wanaotuhumiwa kuingia nchini bila ya kibali raia wa Ethiopia wakipata uji. |
![]() |
Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani Jonathan Shana akiwa mbele ya watu ambao wanatuhumiwa kuwa ni wahamiaji haramu kutoka nchi ya Ethiopia ambao walikamatwa mkoani humo. |
Na John
Gagarini, Chalinze
HUKU Serikali
ikiwa inaweka mikakati ya kukabiliana na wimbi la wahamiaji haramu hapa nchini
Jeshi la polisi mkoa wa Pwani limewakamata wahamiaji haramu 72 kutoka nchi ya
Ethiopia kwa tuhuma za kuingia nchini bila ya kibali.
Akizungumza
na waandishi wa habari kwenye kituo cha wilaya ya Kipolisi ya Chalinze kamanda
wa polisi mkoani Pwani Jonathan Shana alisema kuwa wahamiaji hao walikuwa
safarini kwenda Afrika ya Kusini.
Shana alisema
kuwa tukio hilo lilitokea Agosti 5 majira ya saa 3:30 asubuhi kwenye Pori la
Ranchi ya Taifa (NARCO) kata ya Vigwaza wilaya ya Kipolisi ya Chalinze wilaya
ya Bagamoyo.
“Mbali ya
wahamiaji hao haramu pia tunamshikilia Rajabu Hitaji (30) mkazi na
mfanyabiashara wa Vigwaza baada ya msako mkali uliofanywa na makchero wa jeshi
la polisi baada ya kupata taarifa kuwa kuna wahamiaji haramu wameingia bila ya
kibali,” alisema Shana.
Alisema kuwa
wahamiaji hao haramu baada ya kugundua kuwa kuna gari la polisi linawafuatilia
waliingia kwenye hifadhi hiyo kwa lengo la kujificha lakini msako mkali
uliofanywa uliweza kuwabaini na kukamata kundi la kwanza la watu 63 ambao
walikaa sehemu ambayo gari haliwezi kufika.
“Baada ya
kuwakamata wahamiaji hao haramu kundi la kwanza askari waliendelea na msako
ambapo waliwakamata wahamiaji wengine tisa waliokuwa wakijaribu kutaka kutoka
kwenye pori hilo,” alisema Shana.
Alisema kuwa
wahamiaji hao haramu wanatarajiwa kukabidhiwa idara ya Uhamiaji kwa ajili ya
hatua za kisheria pamoja na mfanyabiashara aliyekamatwa ambaye anatuhumiwa
kuwasafirisha.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment