Monday, August 7, 2017

SIMBA WATOA MISAADA WAFANYA USAFI ZAHANATI YA MWENDAPOLE KIBAHA













Na John Gagarini, Kibaha

TAWI la Simba wilayani Kibaha limepongezwa na zahanati ya Mwendapole wilayani Kibaha kwa kujitolea zawadi kwa wagonjwa pamoja na kufanya usafi.

Hayo yalisemwa na muuguzi mganga mfawidhi wa zahanati hyo Gloria Leonidas wakati wa kuushukuru uongozi wa tawi hilo baada ya kumaliza kufanya usafi na kutoa zawadi za sabuni kwa wagonjwa.

Dk leonidas alisema kuwa vilabu vyote vinapaswa kuunga mkono kitu kilichofanywa na tawi hilo la Simba kwa kufanya shughuli za usafi na kujitolea kile walichonacho.

“Timu zinapaswa kuangalia mbali zaidi kwa kujishughulisha na kuisaidia jamii kama walivyofanya Wanasimba hawa kwani wameonyesha uzalendo wa hali ya juu,” alisema Dk Leonidas.

Alisema kuwa kusaidia sehemu kama hizo za jamii kunaleta motisha kwa watumishi wanaofanya kazi sehemu hizo za kutolea huduma inawafanya kuona kuwa wanawajali.

“Mkitusaidia kama hivi tunapata faraja hata wagonjwa nao wanajisikia vizuri kufarijiwa kama walivyofanya Wanasimba Kibaha tunaomba na klabu za hapa nazo ziige mfano huu,” alisema Dk Leonidas.

Kwa upande wake makamu mwenyekiti wa tawi la Simba Kibaha Said Tisa alisema kuwa wamekuwa na utaratibu wa kujitolea kwa jamii na sehemu za kutolea huduma.

Tisa alisema kuwa wanaungana na Simba makao makuu wakati wa kuelekea tamasha la Simba Day ambalo huazimishwa kila mwaka ambapo mwaka huu linafanyika leo uwanja wa taifa.

Alisema kuwa wataendelea na utamaduni huo ili kuisaidia jamii iweze kuona faida ya timu na siyo kushiriki uwanjani pekee bali hata kuwajibika kwa jamii.


Mwisho.  
                                         



No comments:

Post a Comment