Na John
Gagarini, Kibaha
TAWI la Simba
wilayani Kibaha limepongezwa na zahanati ya Mwendapole wilayani Kibaha kwa
kujitolea zawadi kwa wagonjwa pamoja na kufanya usafi.
Hayo
yalisemwa na muuguzi mganga mfawidhi wa zahanati hyo Gloria Leonidas wakati wa
kuushukuru uongozi wa tawi hilo baada ya kumaliza kufanya usafi na kutoa zawadi
za sabuni kwa wagonjwa.
Dk leonidas
alisema kuwa vilabu vyote vinapaswa kuunga mkono kitu kilichofanywa na tawi
hilo la Simba kwa kufanya shughuli za usafi na kujitolea kile walichonacho.
“Timu
zinapaswa kuangalia mbali zaidi kwa kujishughulisha na kuisaidia jamii kama
walivyofanya Wanasimba hawa kwani wameonyesha uzalendo wa hali ya juu,” alisema
Dk Leonidas.
Alisema kuwa
kusaidia sehemu kama hizo za jamii kunaleta motisha kwa watumishi wanaofanya
kazi sehemu hizo za kutolea huduma inawafanya kuona kuwa wanawajali.
“Mkitusaidia
kama hivi tunapata faraja hata wagonjwa nao wanajisikia vizuri kufarijiwa kama
walivyofanya Wanasimba Kibaha tunaomba na klabu za hapa nazo ziige mfano huu,”
alisema Dk Leonidas.
Kwa upande
wake makamu mwenyekiti wa tawi la Simba Kibaha Said Tisa alisema kuwa wamekuwa
na utaratibu wa kujitolea kwa jamii na sehemu za kutolea huduma.
Tisa alisema
kuwa wanaungana na Simba makao makuu wakati wa kuelekea tamasha la Simba Day
ambalo huazimishwa kila mwaka ambapo mwaka huu linafanyika leo uwanja wa taifa.
Alisema kuwa
wataendelea na utamaduni huo ili kuisaidia jamii iweze kuona faida ya timu na
siyo kushiriki uwanjani pekee bali hata kuwajibika kwa jamii.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment