Friday, August 4, 2017

AUWAWA NA WANANCHI WENYE HASIRA KALI KWA TUHUMA ZA WIZI


Na John Gagarini, Kibaha

JESHI la Polisi limesema kuwa bado linaendelea kumshikilia kijana wa kiume mkazi wa Mbagala Jijini Dar es Salaam ambaye alivalia mavazi ya kike ikiwemo dera hijabu na kuficha sura yake kwa kuva nikabu.

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Pwani Jonathan Shana alisema kuwa kijana huyo alikamatwa Agosti 2 maeneo ya Picha ya Ndege barabara ya kuelekea Magereza huku akiwa amevaa mavazi hayo.

Shana alisema kuwa kwa sasa jeshi hilo bado linamshikilia kijana huyo kwa ajili ya mahojiano ili kubaini mtandao anaoshirikiana nao kwenye matukio ya uhalifu.

“Kijana huyu tulimkamata baada ya kumwekea mtego uliowekwa na makachero wetu waliokuwa wamepata taarifa kutoka kwa wasiri waliokuwa wanamtilia mashaka na walifanikiwa kumkamata akiwa kwenye bodaboda akielekea maeneo ya Magereza,” alisema Shana.

Alisema kuwa hadi sasa bado hawajajua kijana huyo alikuwa na lengo gani la kuvaa nguo hizo za kike hali ambayo hadi sasa bado haijafahamika hasa alidhamiria nini.

“Hadi sasa tunaendelea kumhoji kujua ni kwanini avae mavazi ya kike na tunawashukuru wananchi na wasiri wetu kwa kuendelea kutupa ushirikiano wa kufanikisha kukamatwa kwa wahalifu,” alisema Shana.


Mwisho.

No comments:

Post a Comment