Na
John Gagarini, Kibaha
HALMASHAURI
za wilaya mkoani Pwani zimetakiwa kuwa na ubunifu kwa kushirikiana na wadau wa
maendeleo ili kujenga barabara badala ya kuisubiri Wakala wa Barabara Tanzania
(TANROADS).
Kutokana
na kutokuwa na ubunifu baadhi ya wilaya hazina hata kilomita moja ya barabara
ya iliyojengwa kwa kiwango cha lami.
Ushauri
huo ulitolewa mjini Kibaha na mkuu wa mkoa wa Pwani Mwantumu Mahiza, wakati wa
kikao cha bodi ya barabara ya mkoa huo.
Mahiza
alisema kuwa inashangaza kuona kuwa hakuna jitihada zozote zikifanyika za
kuhakikisha kunakuwa na ujenzi wa barabara za lami.
“Kaeni
na wadau wenu jengeni barabara za lami hata kilomita moja moja mfano mzuri ni
Halmashauri ya Mji wa Kibaha imejenga lami kidogo kidogo kwenye baadhi ya maeno
lakini zingine hazifanyi jitihada kama hizo,” alisema Mahiza.
Aidha
alisema kama halamashauri hazina uwezo zinaweza kuingia mikataba na wajenzi wa
barabara ili baadaye wawalipe.
“Mji
wa Kibaha ulikopa fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara zake kwa kiwango cha
lami kwa hiyo na Halmashauri nyingine ziige mfano huu kwani kikubwa ni ubunifu
msikubali kukaa tu,” alisema Mahiza.
Alibainisha
kuwa kuna Halmashauri zina vyanzo vingi vya mapato ambavyo vinaweza kuwasaidia
katika kufanikisha ujenzi huo kwani haipendezi kutokuwa na lami ambayo
inapendeza na inapunguza ukarabati wa mara kwa mara unaotumia fedha nyingi.
Kwa
upande wake Meneja wa TANROADS Injinia Tumaini Sarakikya alisema uwezo wao siyo
mkubwa kutokana na kutokuwa na fedha nyingi kwani wanategemea kutoka
serikalini.
Injinia
Sarakikya alisema kuwa wao wataendelea kuboresha barabara pamoja na miundombinu
yake ikiwemo madaraja, makalavati na shughuli nyingine zinazohusiana na masuala
mazima ya barabara.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment