Monday, December 15, 2014

CCM YAONGOZA MATOKEO YA UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA, VITONGOJI NA VIJIJI

Na John Gagarini, Kibaha
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Pwani kimeonyesha kufanya vizuri kwenye uchaguzi wa serikali za Mitaa, Vitongoji na Vijiji ambapo kwenye matokeo ya awali kimeonekana kushinda maeneo mengi.
Katika Jimbo la Mafia CCM ilishinda vitongoji  96 kati ya 136 sawa na asilimia 70 Chama Cha Wananchi CUF asilimia 40 sawa na asilimia 29,katika vijiji  CCM ilishinda vijiji 19 kati ya 23 sawa na asilimia 82.6 CUF vijiji 4 sawa na asilimia 17.3.
Katika Jimbo la Kibaha Mjini kati ya mitaa iliyopo 73 ,CCM imeshinda mitaa 62 sawa na asilimia 84.9, huku wapinzani wao Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wakishinda kwenye mitaa 10 sawa na asimilia 13.7.
Katika Jimbo Kibaha  Vijijini kwenye Vijini 32 CCM ilishinda mitaa 31 , ambapo kwenye mitaa 10 ilishinda bila kupingwa sawa na asimilia 96.9 ,upinzani ilishinda kijiji kimoja sawa na asimilia 13.1, kati ya vitongoji 106 CCM ilishinda vitongoji 98 sawa na asilimia 92.5,upinzani vitongoji 4 sawa na asilimia 3.8.
Katika Wilaya ya Bagamoyo vijiji vilivyopo ni 75 CCM ilishinda vijiji 67 sawa na asilimia 90.5 na vijiji 8 havijafanya uchaguzi, kati ya vitongoji  610 CCM ilishinda 540 sawa na asilimia 88.5 na vitongoji 45 havijafanya uchaguzi ambapo wapinzani walishinda vitongoji sawa na  asilimia 4.1.
Wilaya ya Bagamoyo haijafanya uchaguzi katika vijiji 8 na vitongoji 45 kutokana na uhaba wa vifaa ikiwemo katasi husika za viti maalum na kuchanga majina ya wananchi na nembo za vyama vya siasa.
Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo Ibrahim Matovu alithibitisha kutokea kwa mabadiliko ya uchaguzi katika maeneo hayo ambapo alisema uchaguzi huo baadhi ya maeneo ulifanyika jana na kwingine utafanyika leo desemba 16.

Mwisho

No comments:

Post a Comment