Wednesday, December 31, 2014

AFA KWA KUJINYONGA KISA KUUGUA MUDA MREFU

Na John Gagarini, Kibaha
HUKU leo ikiwa ndiyo siku ya kwanza ya mwaka mpya wa 2015 ikiwa imeanza fundi wa kuchomelea Michael Mpondo (36) mkazi wa Machinjioni wilayani Kibaha mkoani Pwani ameamua kukatisha uhai kwa kujinyonga.
Imeelezwa kuwa chanzo cha fundi huyo kuamua kuchukua maamuzi hayo magumu ya kuamua kujiua kunatokana na kuugua kwa muda mrefu.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mjini Kibaha mwenyekiti wa mtaa wa Machinjioni Evarist Kamugisha alisema kuwa marehemu alijinyonga jirani na nyumba laiyokuwa akiishi.
Akielezea kwa kina tukio hilo Kamugisha alisema kuwa tukio hilo lilitokea Desemba 30 mwaka huu majaira ya saa 4:30 asubuhi baada ya mwili wake kukutwa ukininginia kwenye mti umbali wa mita 60 na alipokuwa akiishi.
“Marehemu usiku wa majira ya saa 2:30 kabla ya kifo chake alikula chakula na ndugu zake lakini aliondoka na jitihada za kumtafuta zilifanyika bila ya mafanikio lakini asubuhi yake ndipo watu walipouona mwili wake ukinginginia,” alisema Kamugisha.
Kamugisha alisema kuwa marahemu alikuwa akiumwa ambapo baada ya chumba chake kupelkuliwa kulikutwa dawa aina ya Panadoli pamoja na Amoxilini ambazo inasemekana alikuwa akizitumia.
“Marehemu alijinyonga kwa kutumia kamba ya nguo ya jeshi ambayo aliikata na kuwa kama kamba na kujinyonga nayo na hakuacha ujumbe wowote juu ya kifo chake,” alisema Kamugisha.
Kwa upande wake kamanda wa Polisi mkoani Pwani Ulrich Matei alithibitisha kutokea tukio hilo na kusema kuwa chanzo cha kifo hicho ni marehemu kuugua muda mrefu na kukata tamaa ya maisha.

Mwisho.   

No comments:

Post a Comment