Wednesday, December 24, 2014

POLISI KUWEKA ULINZI MKALI SIKUKUU ZA X-MASS NA MWAKA MPAYA

Na John Gagarini, Kibaha
JESHI la Polisi mkoani Pwani limewataka wananchi kutumia vikundi vya ulinzi shirikishi ili kukabiliana na uhalifu katika kipindi hichi cha sikukuu za X-Mass na mwaka mpya.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha, kamanda wa Polisi mkoani hapa Ulrich Matei alisema kuwa wamejipanga vyema kudhibiti vitendo viovu kwa kushirikiana na wananchi.
Matei alisema kuwa katika kukabiliana na matukio ya uhalifu kipindi cha sikukuu kwa kutumia ulinzi shirikishi, ulinzi jirani na mgambo.
“Tutashirikiana na wananchi katika ulinzi ili washerehekee kwa amani na utulivu na tutakaowabaini wanaofanya matukio ya uhalifu,” alisema Matei.
Alisema kuwa katika ulinzi jirani wananchi wanatakiwa kuacha tabia ya kuondoka nyumbani bila ya kuacha mtu au hata kama wanatoka wawajulishe majirani zao.
“Baadhi ya vitendo viovu vinavyofanyika ni pamoja na uchomaji matairi ni kinyume cha sheria na hairuhusiwi kufanya hivyo,” alisema Matei.
Aidha alisema kuwa wazazi wanapaswa kutowaacha watoto wao kwenda kwenye maeneo ya starehe peke yao kwani ni hatari.
Aliwataka madereva kuhakikisha wanaendesha magari wakiwa hawajalewa ili kuepukana na ajali pia watawapima ulevi madereva hao kwani vifaa vya kupimia sasa wanavyo vya kutosha.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment