Na John Gagarini, Kibaha
HUKU leo ikiwa ni sikukukuu ya
kumbukumbu ya kuzaliwa Yesu Kristo X-MASS ikiwa inaadhimishwa duniani kote wakazi
wa wilaya ya Kibaha mkoani Pwani wanasherehekea kwa furaha kutokana na bei za
bidhaa za vyakula zikiwa hazijapanda kama inavyokuwa miaka ya nyuma.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili
umebaini kuwa bei za bidhaa za vyakula hazijapanda kama miaka ya nyuma kwani
nyingi ziko vilevile hali amabyo imefurahiwa na wananchi wengi.
Akizungumza na gazeti hili mjini Kibaha
mkazi wa Maili Moja Kibena Mtoro alisema kuwa wanasherehekea sikukuu hii huku
bei za bidhaa za vyakula zikiwa ni za kawaida.
“Miaka ya nyuma beiza bidhaa za vyakula
zilikuwa zinapanda mara dufu lakini mwaka huu tunamshukuru Mungu kwani bei ni
zilezile,” alisema Mtoro.
Mtoro alisema kipindi cha nyuma baadhi
ya watu wenye kipato cha chini walikuwa hawaifurahii sikukuu kutokana na bei
kuwa juu.
“Kutokana na hali ya kiuchumi kuwa
mabaya na bei kuwa za kawaida ni dhahiri tunasherehekea sikuku hii kwa furaha
kwani kila mtu anamudu kununua chakula,” alisema Mtoro.
Kwa upande wake katibu wa soko kuu la
wilaya ya Kibaha Maili Moja, Muhsin Abdu alisema kuwa kwa mwaka huu bei
hazijapanda kabisa.
Abdu alisema kuwa bei ya ndizi pekee
ndiyo iliyopanda ambapo mkungu umepanda bei kutoka shilingi 20, 000 hadi 35,000
kwa mkungu pamoja na tanagawizi toka shilingi 3,000 kwa kilo hadi 4,500.
“Bei haijapanda kwa sababu mojawapo ni
wakulima wengi kuleta bidhaa toka mashambani na kuja kuziuza mjini tofauti na
kipindi cha nyuma ambapo wafanyabiashara walikuwa wakileta bidhaa na kuuza kwa
bei kubwa,” alisema Muhsin.
Alisema kuwa wafanyabiashara ndiyo
walikuwa wakipandisha bei kwa kuficha bidhaa ili wauze kwa bei kubwa wakitoa
visingizio mbalimbali.
“Kipindi kile bei zilikuwa juu na
zinakuwa adimu lakini safari hii vyakula vingi na bado vinakuja kwa wingi hata
sisi tunafurahia hali kwani bei zikiwa juu hata uuzaji unakuwa mgumu,” alisema
Abdu.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment