Saturday, December 20, 2014

RIDHIWANI AKARIBISHWA KIJIJINI MSOGA KWA SHEREHE ZA JADI

Na John Gagarini, Chalinze

MBUNGE wa Jimbo la Chalinze Wilayani Bagamoyo mkoani Pwani  Ridhiwani Kikwete juzi alifanyiwa sherehe za jadi za kabila la Kikwere kama kiongozi baada ya kuchaguliwa kuwa mbunge.

Sherehe hizo za jadi ambazo zilifanyika kijijini kwao Msoga ziliambatana na kukabidhiwa vitu mbalimbali vya kijadi kwa ajili ya matumizi ya nyumbani.

Baadhi ya vitu alivyoakabidhiwa na mzee wa kabila hilo Zaidi Rufunga ni pamoja na fimbo kama kiongozi, kitanda cha kamba, msuli, kigoda na kinu pamoja na vitu mbalimbali.


Sherehe hizo za kijadi ziliamabatana na ngoma ya Kikwere na ulaji wa chakula kiitwacho Bambiko ambacho hutumiwa na kabila hilo. 

 Mzee Zaidi Rufunga kulia akimkabidhi vyungu mbunge wa Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani Ridhiwani Kikwete wakati wa sherehe za jadi za kumkaribisha nyumbani zilizofanyika juzi kijiji cha Msoga. 




 Mbunge wa Jimbo la Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani  akielekezwa jambo na mzee Zaidi Rufunga  kabla ya kula chakula cha jadi cha kabila la Wakwere kiitwacho Bambiko baada ya kukaribishwa nyumbani na kufanyiwa sherehe za jadi za kikabila zilizofanyika kwenye Kijiji cha Msoga.




Baadhi ya akina mama wakila chakula mcha jadi cha kabila la Kikwere kiitwacho Bambiko mara baada ya kumkaribisha nyumbani Mbunge wa Jimbo la Chalinze wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani

 Baadhi ya akina mama wakila chakula mcha jadi cha kabila la Kikwere kiitwacho Bambiko mara baada ya kumkaribisha nyumbani Mbunge wa Jimbo la Chalinze wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani

Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete kushoto na katikati diwani wa kata ya Msoga Mohamed Mzimba na baadhi ya wageni wakila chakula cha jadi kiitwacho Bambiko mara baada ya sherehe za jadi za kumkaribisha nyumbani kwenye Kijiji cha Msoga .


No comments:

Post a Comment