Na John Gagarini,
Bagamoyo
WATANZANIA wametakiwa
kuzingatia ulaji wa vyakula na ufanyaji wa mazoezi ili kukabiliana na magonjwa
yasiyoambukiza ambayo kwa sasa yanasababisha vifo vya watu wengi hapa nchini.
Hayo yamesemwa hivi
karibu kwenye Kijiji cha Msoga wilayani Bagamoyo mkoani Pwani na katibu mkuu wa
Wizara ya Afya Dk Donan Mmbando alipotembelea kukagua ujenzi wa kituo cha afya
cha kisasa cha Kijiji hicho.
Dk Mmbando amesema
kuwa kwa sasa kumekuwa na ushindani mkubwa wa magonjwa yasiyoambukiza na yale
yanayoambukiza katika kusababisha vifo hivyo jamii inapaswa kuangalia njia za
kujikinga na magonjwa hayo.
Amesema kuwa magonjwa
yasiyoambukiza kama vile kisukari, magonjwa ya moyo na presha na mengineyo ya
namna hiyo yanasababisha vifo vingi hapa nchini kwa sasa ambapo serikali imekuwa
ikitumia gharama kubwa kuyadhibiti
Ametoa mfano wa baadhi
ya nchi zilizoendelea zimekuwa zikitenga hadi kufikia asilimia 15 ya bajeti
katika kukabiliana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza ili kupunguza vifo.
Amebainisha baadhi ya
vitu vinavyochangia magonjwa hayo kuongezeka ni pamoja na uvutaji wa sigara,
unywaji wa pombe na kutofanya mazoezi ni baadhi ya mambo yanayochangia
kuongezeka kwa magonjwa hayo.
Aidha amesema kuwa wao
kama wizara wanasisistiza kinga zaidi ili kukabilina na magonjwa hayo na ndiyo
maana wamekuwa wakitoa chanjo za kinga za magonjwa mbalimbali hasa kwa watoto
ili kukabiliana na magonjwa mbalimbali.
Katibu mkkuu huyo wa
wizara ya Afya amesema wamekuwa wakihamasisha ulaji wa chakula kwa mpangilio
kwani chakula nacho kimekuwa ni changamoto ya ongezeko la magonjwa hayo kutokana
na ulaji usiofaa, na wamekuwa wakikabili magonjwa hayo kwa kuzingatia taratibu
za afya kupunguza vifo.
Amewataka wananchi
kupata tiba sahihi ya magonjwa ili kupunguza madhara yatokanayo na magonjwa
kuwa sugu pia wajiunge na mifuko ya afya ili kupunguza mzigo wa malipo kwa
ajili ya matibabu.
Na John Gagarini,
Kibaha
WAZEE wa Halmashauri
ya wilaya ya Kibaha mkoani Pwani wameipongeza serikali kwa kuwatengea kitengo
maalumu kwa ajili ya kuwahudumia.
Akizungumza na waandishi
wa habari mjini Kibaha mwenyikiti wa wazee Mlandizi Mohamed Pongwe wakati wa
mafunzo ya kuwahudumia wazee majumbani alisema kuwa kwa sasa huduma zao
zimeboreshwa tofauti na ilivyokuwa mwanzo.
Pongwe alisema kuwa
huduma kwa wazee kwenye kituo cha Afya cha Mlandizi na sehemu nyingine za
huduma za afya zilikuwa ni mbaya kutokana na wazee kutopewa kipaumbele wakati
wa kupata matibabu.
“Kwa sasa tunaishukuru
serikali ya wilaya kwa kutuwekea kitengo chetu dirisha malumu kwa ajili ya
kuwapatiwa huduma za matibabu kwenye kituo hicho cha afya cha Mlandizi kwani
tunahudumiwa vizuri,” alisema Pongwe.
Alisema kuwa kama
unavyojua wazee wana matatizo mengi hasa ya kiafya lakini walikuwa wakipuuzwa
kwenye suala la afya hali iliyokuwa ikisababisha waishi katika hali mbaya za
kiafya.
“Tunakwenda hospitali
tukiwa hautna wasiwasi wa matibabu kwani tuna dirisha letu maaalumu tunapata
huduma kwa upendo kutoka kwa wahudumu wa afya kwa kweli hata afya zetu
zinaridhisha,” alisema Pongwe.
Kwa upande wake
mwezeshaji wa mafunzo hayo Elizabeth Sekaya ambaye ni muuguzi wagonjwa
majumbani na huduma kwa wazee kutoka halmashauri ya wilaya alisema kuwa lengo
la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo wazee waweze kuwasaidia wenzao kwenye
huduma za afya wakiwa majumbani.
“Tumekuwa tukiwapatia
mafunzo haya mara kwa mara na tumeona mafanikio kwani sasa wameweza kuyakabili
baadhi ya magonjwa wakiwa nyumbani ikiwa ni pamoja na ufanyaji wa mazoezi na
lishe bora,” alisema Sekaya.
Sekaya alsiema kuwa
wazee wanachangamoto kadhaa ikiwa ni pamoja na maumivu ya mwili na kingine ni
ususaji wa chakula endapo wanaudhiwa hivyo tunawajengea uwezo wa kujiamini na
kukabilina na changamoto mbalimbali.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment