Wednesday, January 30, 2013



Na John Gagarini, Kibaha
MWANAFUNZI ambaye ni miongoni mwa wanafunzi waliofeli kidato cha pili mwaka jana kwenye shule ya sekondari ya Tumbi wilayani Kibaha mkoani Pwani Shaban Kihemele (16) ametoroka nyumbani kwa madai kuwa wanafunzi wenzake kumzomea kuwa amerudia darasa.
Akizungumza na waandishi wa habari hizi mjini Kibaha mzazi wa mtoto huyo Bw Shaban Kihemele alisema kuwa mwanae huyo huyo alitoroka Januari 24 mwaka huu na hadi leo hajaonekana licha ya jitihada za kumtafuta kushindwa kufua dafu.
Bw Kihemele alisema kuwa mwanae aliondoka nyumbani majira ya saa 4 asubuhi huku akiwa amevalia kaptura nyeusi ya Jeans iliyokatwa tisheti ya rangi ya zambarau yenye ufito mweupe kifuani na ndala nyekundu.
“Chanzo cha yeye kutoroka siku ya Januari 23 alimwambia mama yake kuwa kutokana na kufeli mtihani wa kidato cha pili ni vema wamwamishe shule kuliko kuendelea kusoma hapo kwani wanafunzi wanaomfahamu wanamzomea lakini mama yake alimwambia asubiri mimi nirudi kwani sikuwepo nilikuwa Bagamoyo kikazi,” alisema bw Kihemele.
Alisema mama yake alimjibu kuwa asubiri hadi nirudi lakini kesho yake alirudi kutoka shuleni na kubadilisha nguo huku majirani wakimwuliza kuwa ni kwanini amewahi kurudi na anakwenda wapi akawaambia yuko hapa hapa pia baba yake hajalipa ada hivyo amerudishwa.
“Alichukua fedha kiasi cha shilingi 20,000 kati ya shilingi 50,000 zilizokuwepo kasha akachukua na shuka kisha kuondoka kusikojulikana na inawezekana aliotoroka kutokana na kuona kuwa ni fedheha kurudia darasa na madai kuwa wenzake wanamzomea jambo ambalo linatushangaza,” alisema Bw Kihemele.
Aidha alisema siku ya kwanza walimsubiri hakutokea na ilipofika usiku walikwenda kutoa taarifa kituo cha polisi cha Maili Moja KMM/RB/108/2013 juu ya kutoonekana mtoto wao, walikwenda nyumbani kwao Bagamoyo lakini hawajaweza kufanikiwa kumwona pia waliwasiliana na ndugu zao wote lakini imeshindikana.
Mwisho.

HABARI ZA PWANI




Na John Gagarini, Mkuranga
IMEELEZWA kuwa kuishi mbali na vituo vyao vya kazi kwa baadhi ya maofisa
ugani kwenye vijiji wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani kumechangia kudumaza
shughuli za kilimo wilayani humo.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa mafunzo kwenye kijiji cha
Msufini kata ya Mbezi, mratibu wa mradi wa Wajibu wa Jamii Katika Usimamizi
wa Rasilimali za Umma za Sekta ya Kilimo wilaya hiyo (POCUSO), Bw Said
Gwaja alisema kuwa maofisa hao wamekuwa hawafiki kwenye vijiji
walivyopangiwa.

Bw Gwaja alisema kuwa kutokana na kuishi mbali na vituo vyao vya kazi
wamekuwa wakiishia ofisini na kushindwa kwenda kwenye maoeneo waliyopangiwa
hasa yale ya vijijini.

“Ni vema wangekaa kwenye maeneo yao ya kazi ili iwe rahisi kwao kutoa
huduma kwa wakulima ambao wanakosa fursa nyingi kutokana na kutofahamishwa
namna ya kuweza kuzipata,” alisema Bw Gwaja.

Alisema kuwa fursa ambazo wakulima walipaswa kuzijua zinashindwa kuwafikia
kwani wanazipata wakati muda wa kilimo unakuwa umepita hivyo kushindwa kupata pembejeo za ruzuku kwa wakati muafaka.
Aidha alisema kuwa endapo wangekuwa wanafanya kazi kwenye maeneo waliyopangiwa hususani vijijini ingekuwa raisi kwao kujua chanagamoto zinazo wakabili wakulima hivyo ingekuwa rahisi kuwasaidia kuliko ilivyosasa.
Aliwataka wakulima kujitokeza kwenye mafunzo yanayoandaliwa na shirika lake ili waweze kujua namna ya kufuatilia matumizi ya rasilimali za wananchi zikiwemo zile za kilimo ambazo nyingine zinawalenga wao moja kwa moja.
Mwisho.
Na Mwandishi Wetu, Mkuranga
WANANCHI wametaka katiba mpya iwe na kipengele cha wafanyakazi wa serikali kufanya kazi kwa mkataba wa miaka 10 ili aweze kuwajibishwa endapo utendaji kazi wake hautaridhisha.
Hayo yalisemwa jana Mkuranga na Bw Mohamed Abdul wakati wa Mdahalo wa Katiba kwa wakazi wa Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani uliandaliwa na Mtandao wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali wilayani Mkuranga (MKUNGONET).
Alisema kuwa baadhi ya wafanyakazi wa serikali wamekuwa hawatekelezi vema majukumu yao hali inayofanya washindwe kuwaletea maenedeleo wananchi ambao wanaamini kuwa elimu walizonazo hawazitumii kikamilifu.
“Tungetaka katiba iwe na kipengele cha wafanyakazi wa serikali kuwa na mkataba wa miaka 10 ili akifanya vema aongezewe mkataba na kama akifanya vibaya asiongezewe mkataba wa kazi,” alisema Bw Abdul.
Alisema kuwa endapo kutakuwa na mikataba ya muda wa kufanya kazi kutaleta uwajibikaji sehemu za kazi tofauti na ilivyo sasa baadhi ya wafanyakazi kutowajibika kwa kuamini kuwa hawawezi kuondolewa kazini hata kama wameboronga.
Aidha alisema kuwa pia sifa za wataalamu  mbalimbali ziwekwe kwenye mbao za matangazo ili wananchi waweze kujua uwezo wa wataalamu hao.
“Hii itasaidia kuwawajibisha wataalamu hao ambao wataonekana uwezo wao ni mdogo kwani baadhi hawana uwezo,” alisema Bw Abdul.
Kwa upande wake mratibu wa MKUNGONET Bw Mohamed Katundu alisema kuwa lengo la mdahalo huo ni kuwaelekeza namna ya kutoa maoni yao juu ya marekebisho ya katiba mpya.
Bw Katundu alisema kuwa mdahalo huo uliofadhiliwa na The Foundation for Civil Society ulihudhuriwa na madiwani, wataalamu toka wilayani, mashirika mbalimbali yasiyo ya kiserikali na wananchi.
Mwisho.   
Na John Gagarini, Kibaha
MWANAFUNZI ambaye ni miongoni mwa wanafunzi waliofeli kidato cha pili mwaka jana kwenye shule ya sekondari ya Tumbi wilayani Kibaha mkoani Pwani Shaban Kihemele (16) ametoroka nyumbani kwa madai kuwa wanafunzi wenzake kumzomea kuwa amerudia darasa.
Akizungumza na waandishi wa habari hizi mjini Kibaha mzazi wa mtoto huyo Bw Shaban Kihemele alisema kuwa mwanae huyo huyo alitoroka Januari 24 mwaka huu na hadi leo hajaonekana licha ya jitihada za kumtafuta kushindwa kufua dafu.
Bw Kihemele alisema kuwa mwanae aliondoka nyumbani majira ya saa 4 asubuhi huku akiwa amevalia kaptura nyeusi ya Jeans iliyokatwa tisheti ya rangi ya zambarau yenye ufito mweupe kifuani na ndala nyekundu.
“Chanzo cha yeye kutoroka siku ya Januari 23 alimwambia mama yake kuwa kutokana na kufeli mtihani wa kidato cha pili ni vema wamwamishe shule kuliko kuendelea kusoma hapo kwani wanafunzi wanaomfahamu wanamzomea lakini mama yake alimwambia asubiri mimi nirudi kwani sikuwepo nilikuwa Bagamoyo kikazi,” alisema bw Kihemele.
Alisema mama yake alimjibu kuwa asubiri hadi nirudi lakini kesho yake alirudi kutoka shuleni na kubadilisha nguo huku majirani wakimwuliza kuwa ni kwanini amewahi kurudi na anakwenda wapi akawaambia yuko hapa hapa pia baba yake hajalipa ada hivyo amerudishwa.
“Alichukua fedha kiasi cha shilingi 20,000 kati ya shilingi 50,000 zilizokuwepo kasha akachukua na shuka kisha kuondoka kusikojulikana na inawezekana aliotoroka kutokana na kuona kuwa ni fedheha kurudia darasa na madai kuwa wenzake wanamzomea jambo ambalo linatushangaza,” alisema Bw Kihemele.
Aidha alisema siku ya kwanza walimsubiri hakutokea na ilipofika usiku walikwenda kutoa taarifa kituo cha polisi cha Maili Moja KMM/RB/108/2013 juu ya kutoonekana mtoto wao, walikwenda nyumbani kwao Bagamoyo lakini hawajaweza kufanikiwa kumwona pia waliwasiliana na ndugu zao wote lakini imeshindikana.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
DIWANI wa kata ya Picha ya Ndege wilayani Kibaha mkoani Pwani Bw Bosco Mfundo kupitia chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) juzi alitolewa nje kwenye kikao cha baraza la Madiwani wa halmashauri ya Mji wa Kibaha baada ya kusema kuwa meya wa mji huo Bw Adhudadi Mkomambo ni mwizi.
Sakata la diwani huyo maarufu kama Obama kutolewa nje lilikuja wakati wa kikao cha madiwani kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo uliopo Kibaha.
Chanzo cha diwani huyo kutolewa nje ni kukataa kupokea taarifa ya halmashauri na kusema kuna wizi umefanyika kwenye taarifa ya fedha na mwenyekiti ni mwizi jambo ambalo lilimfanya meya huyo kumtaka diwani huyo atoke nje kwa muda kabla ya kurejea na kuendelea na kikao.
“Nilikataa taarifa ya mwenyekiti wa halmashauri kwa sababu kuna wizi umefanywa na halmashauri ya mji wa Kibahakiasi cha shilingi milioni 533 zinaoneka zimeibwa ni wazi taarifa hii ni kuanzia mwezi Oktoba hadi Desemba lakini inaleta matumizi ambayo yalishaletwa kwenye taarifa ya robo ya mwaka uliopita,” alisema Bw Mfundo.
Alisema kuwa kitendo cha wao kutohoji taarifa na kuikubali na kuridhia wizi uliofanyika hadi mwenyekiti anamtoa nje ni wazi naye ni shemu ya wizi huo.
“Mimi ni mwakilishi wa wananchi hivyo siwezi kuridhia kuona fedha za walipa kodi zinachotwa na kutumika kinyume cha taratibu sikotayari,” alisema bw Mfundo.
Kwa upande wake mwenyekiti wa halmashauri hiyo Bw Mkomambo alisema kuwa alimtoa kwenye kikao kwa kufuata kanuni za baraza kwa kutoa lugha mbaya.
“Lugha aliyotumia ilikuwa inahatarisha kikao kishindwe kuendelea na ni jambo ambalo ni kinyume kwani ni utovu wa nidhamu kutumia lugha mabya kwenye kikao kama hicho ambacho ni cha kisheria,” alisema Bw Mkomambo.
Bw Mkomambo alisema kuwa anashangaa diwani huyo kumwita kuwa yeye ni mwizi kwani kama kaiba kaiba nini hasa ikizingatiwa kuwa taarifa hiyo ya fedha ilipitiwa chama chetu na chama chake kabla ya kuletwa kwenye baraza na kama kulikuwa na hoja si wangeileta kwa maandishi juu ya hilo.
“Nawasii madiwani kufuata kanuni na taratibu na kuacha jazba hata kama kuna jambo lazima lifuate taratibu na si kuwa na jazba kwani wanapaswa kutetea maslahi ya wananchi ili kuwaletea maendeleo,” alisema Bw Mkomambo.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
MKUU wa Mkoa wa Pwani amesema kuwa kupatikana kwa greda la kuchongea barabara kwa Halmashauri ya Mji wa Kibaha kuwe changamoto ya kukabiliana na miundombinu mibovu ya barabara za mji huo.
Aliyasema hayo kwenye uzinduzi wa greda hiloa na gari la kuzolea uchafu ambapo taarifa yake ilisomwa na mkuu wa wilaya ya Kibaha Bi Halima Kihemba na kusema kuwa kwa sasa hakuna haja ya kusema kuwa kuna kiporo cha mradi wa barabara.
Alisema kuwa miradi mingi ya barabara ilikuwa inakwama kwa sababu ya kuwa na bajeti ndogo ya kuwalipa wakandarasi kwa ajili ya kufanya kazi hiyo lakini kwa sasa watakuwa wameondokana na kujenga barabara kwa gaharama kubwa.
“Tunawapongeza kwa kununua greda hili ambalo lina thamani ya shilingi milioni 528 zikiwa ni fedha za mapato yenu ya ndani, sasa mtaondokana na kuweka viporo vya miradi ya barabara kwani sasa hivi mtakuwa mkiweka mafuta tu na kutengeneza barabara zenu wenyewe,” alisema Bi Mahiza.
Bi Mahiza alisema kuwa mbali ya kutengeneza barabara hizo wao wenyewe kwa gharama nafuu pia wataweza kulikodisha kwa wakandarasi mbalimbali ndani na nje ya mkoa hali itakayosababisha kujiongezea mapato ya halmashauri.
Aidha alisema kuwa mbali ya kununua greda hilo changaamoto nyingine inayowakabili ni namna ya kulitunza hivyo wanapaswa kuwa makini ili liweze kuleta manufaa kwa halmashauri na wananchi ambao sasa wataondokana na kero ya barabara.
Akizungumzia gari la kuzolea uchafu ambalo limetolewa kama msaada na kutoka Gotland Sweden alisema litasaidia kuboresha mazingira ya mji huo kwani gari walilokuwa nalo mwanzo lilikuwa dogo hivyo kushindwa kumudu uchafu uliopo.
Aliwataka wananchi kulitumia gari hilo kwa kuweka mazingira yao katika hali ya usafi kuondokana na kero hiyo ambayo ilikuwa ni kubwa kwa muda mrefu 
Kwa upande wake kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kibaha Bi Lweah Lwanji alisema kuwa wamejipanga kuvitumia vyombo hivyo katika kuboresha barabara za mji na kuuweka katika usafi ili ufanane na ile ya Moshi na Arusha.
Mwisho.   


Monday, January 28, 2013

WAHAMIAJI HARAMU WADAKWA



Na John Gagarini, Kibaha
JESHI la Polisi mkoani Pwani linawashikilia wahamiaji haramu watano wa nchi ya Ethiopia na Somalia kwa kuingia nchini bila ya kibali.
Kwa mujibu wa kamanda wa Polisi mkoani humo Ulrich Matei alisema kuwa raia hao walikamatwa wakati wa msako wa kukamata wahamiaji haramu.
Kamanda Matei alisema kuwa wahamiaji haramu hao walikamatwa Januari 23 mwaka huu huko Kitongoji cha Kibosha Kijiji cha Mapinga wilayani Bagamoyo.
“Wahamiaji haramu hao walikamatwa wakiwa wanasafirishwa kwenye gari namba T 371 BTL aina ya Noah,” alisema Kamanda Matei.
Alisema kuwa gari hilo lilikuwa likiendeshw ana Bw Evarist Mbilinyi (25) dereva wa Mwananyamala Jijini Dar es Salaam akisaidiwa na Omary Karim (28) fundi magari mkazi wa Magomeni Makuti wakielekea Ethiopia kupitia Bagamoyo.
Aliwataja wahamiaji hao kuwa ni Itemegen Wolde (20) mwanafunzi, Beyene Dutano (25), Aduel Ashebo (24) na Detene Bore (25) kutoka nchini Ethiopia na Abdirsa Abdilim (20) ambaye ni raia wa nchi ya Somali.
Mwisho.   

Sunday, January 27, 2013

WANANCHI NA KATIBA MPYA


John Gagarini, Mkuranga
WANANCHI wametaka katiba mpya iwe na kipengele cha wafanyakazi wa serikali kufanya kazi kwa mkataba wa miaka 10 ili aweze kuwajibishwa endapo utendaji kazi wake hautaridhisha.
Hayo yalisemwa jana Mkuranga na Bw Mohamed Abdul wakati wa Mdahalo wa Katiba kwa wakazi wa Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani uliandaliwa na Mtandao wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali wilayani Mkuranga (MKUNGONET).
Alisema kuwa baadhi ya wafanyakazi wa serikali wamekuwa hawatekelezi vema majukumu yao hali inayofanya washindwe kuwaletea maenedeleo wananchi ambao wanaamini kuwa elimu walizonazo hawazitumii kikamilifu.
“Tungetaka katiba iwe na kipengele cha wafanyakazi wa serikali kuwa na mkataba wa miaka 10 ili akifanya vema aongezewe mkataba na kama akifanya vibaya asiongezewe mkataba wa kazi,” alisema Bw Abdul.
Alisema kuwa endapo kutakuwa na mikataba ya muda wa kufanya kazi kutaleta uwajibikaji sehemu za kazi tofauti na ilivyo sasa baadhi ya wafanyakazi kutowajibika kwa kuamini kuwa hawawezi kuondolewa kazini hata kama wameboronga.
Aidha alisema kuwa pia sifa za wataalamu  mbalimbali ziwekwe kwenye mbao za matangazo ili wananchi waweze kujua uwezo wa wataalamu hao.
“Hii itasaidia kuwawajibisha wataalamu hao ambao wataonekana uwezo wao ni mdogo kwani baadhi hawana uwezo,” alisema Bw Abdul.
Kwa upande wake mratibu wa MKUNGONET Bw Mohamed Katundu alisema kuwa lengo la mdahalo huo ni kuwaelekeza namna ya kutoa maoni yao juu ya marekebisho ya katiba mpya.
Bw Katundu alisema kuwa mdahalo huo uliofadhiliwa na The Foundation for Civil Society ulihudhuriwa na madiwani, wataalamu toka wilayani, mashirika mbalimbali yasiyo ya kiserikali na wananchi.
Mwisho.     
Na Mwandishi Wetu, Mkuranga
WATU wenye ulemavu wametaka kuwe na mchakato wa kuwapata wabunge wanaowakilisha kundi hilo ili kila moja liwe na mwakilishi wake tofauti na sasa kuwa na mwakilishi mmoja ambaye hawezi kutoa mawazo ya makundi mengine.
Akizungumza wilayani Mkuranga kwenye mdahalo wa katiba ulioandaliwa na mtandao wa mashirika yasiyo ya kiserikali wilayani Mkuranga (MKUNGONET) Ester Waziri alisema kuwa wabunge wanaochaguliwa kwa ajili ya uwakilishi watu wenye ulemavu uwakilishi wake bado unalegalega.
Waziri alisema kuwa kuna karibu iana tano za watu wenye ulemavu lakini uwkailishi unakuwa wa kundi moja huku mengine yakiwa yamesahauliwa.
“Tungependa katiba ionyeshe kila kundui kuwa na uwakilishi bungeni kwani kila moja lina mahitaji yake na vipaumbele vyake,” alisema Waziri.
Alitaja baadhi ya makundi hayo ni kama vile walemavu wa viungo, ngozi, wasioona, viziwi, bubu na wengineo ambao kila mmoja ana mahitaji yake.
“Kila kundi ni vema lingekuwa na mwakilsihi wake bungeni kuliko mmoja kuwakilisha makundi yote hivyo mengine kushindwa kuwekewa mazingira mazuri ya kupata fursa mbalimbali za kimaendeleo,” alisema Waziri.
Mratibu wa shirika hilo Mohamed Katundu alisema kuwa waliamua kuandaa mdahalo huo ili wananchi wajue namna ya kutoa maoni yao juu marekebisho ya katiba mpya kwenye mchakato unaoendelea.
Mwisho.  
Na John Gagarini, Kibaha
KATIKA kuihamsisha jamii wilayani Kibaha mkoani Pwani kushiriki kwenye michezo wadau wa michezo wameanzisha klabu ya mazoezi ijulikanayo kama Kongowe Jogging Club.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mjini hapa moja ya waanzilishia wa klabu hiyo Simon Mbelwa alisema kuwa lengo la kuanzisha klabu hiyo ni kuwahamasisha watu kushiriki michezo kwani mbali ya kutoa burudani pia ni ajira.
Mbelwa ambaye pia ni mwamuzi wa ligi Kuu ya Voda Com alisema kuwa tayari wana wanachama 18 na tayari wameshaanza mazoezi ambayo hufanyika kila siku ya Jumamosi na Jumapili.
“Michezo hapa bado haijahamasishwa vya kutosha hivyo wao kama wadau wameona njia mojawapo ni kuanzisha klabu hiyo ambayo itayahusisha michezo mingi kama vile soka, mpira wa pete, riadha na michezo mingine,” alisema Mbelwa.
Alisema kuwa jamii imekuwa haina mwamko wa michezo hivyo wao watashirikiana na wadau wengine kuhakikisha michezo inakuwa kwenye wilaya ya Kibaha
“Wataalamu wa michezo hiyo wapo nikiwemo mimi mwenyewe ambapo nitafundisha michezo mingi kama soka na mingne pia walimu wa michezo mbalimbali tayari tumeshwapata hivyo wapenda michezo wajitokeze kutuunga mkono,” alisema Mbelwa.
Alisema changamoto kubwa ni ukosefu wa vifaa kwa wanamichezo wa klabu yao na kuwataka wafadhili mbalimbali kujitokeza kuwasaidia ili waweze kufanikisha michezo.
Aliwataka wazazi kuwaruhusu watoto wao kujitokeza kushiriki michezo kwani ni moja ya njia za kupata ajira na kuboresha afya zao na kuondokana na magonjwa madogomadogo.
Mwisho.