Na John
Gagarini, Bagamoyo
MKUU wa
wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani Bw Ahmed Kipozi ametaka apewe majina ya ofisa
aliyetoa viwanja kwenye hifadhi ya Misitu ya Mikoko wilayani humo.
Akizungumza
na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya mara baada ya zira
kutembelea misitu ya hifadhi ya Uzigua na Mikoko iliyoandaliwa na Wakala wa
Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Bagamoyo na kusema uharibifu uliofanyika
alisema kuwa misitu hiyo imeharibiwa kwa kiasi kikubwa.
Bw Kipozi
alisema kuwa inashangaza kuona maofisa hao kugawa viwanja kwenye hifadhi ya
misitu badala ya kutoa viwanja kwenye maeneo yaliyotengwa maalumu kwa ajili ya
viwanja.
“Siwezi
kukubaliana na watu ambao hawawajibiki ipasavyo kwani inashangaza kuona kuwa
watu wanatoa maeneo ambayo ni hifadhi kwani misitu ni muhimu kwa viumbe hai
hivyo nataka niwajue waliofanya hivi ili hatua ziweze kuchukuliwa,” alisema Bw
Kipozi.
Aidha alisema
kuwa watu waliopewa viwanja kwenye maeneo hayo ya hifadhi ya mikoko wamekata
miti hiyo ambapo baadhi walikata ili kuona madhari ya bahari na wengine
walianzisha miradi ya samaki.
“Wameharibu
hifadhi hii kwa kiasi kikubwa kwani kila mtu anaelewa umuhimu wa misitu kwani
kukata miti kuna athari nyingi ikiwa ni pamoja na ukosefu wa mvua kuharibu
mazalio ya samaki na kubadili uoto wa asili hivyo lazima wahusika wawajibike,”
alisema Bw Kipozi.
Kwa upande
wake meneja wa wilaya ya Bagamoyo Bw Charles Mwamfute alisema kuwa hifadhi za
misitu hiyo zimeharibiwa na watu kwa ajili ya kukata miti, kuchoma mkaa na
wafugaji kuingia kwenye misitu hiyo.
“Sisi wakala
mpya ambao umeanzishw akwa ajili ya kulinda misitu ya asili kila wailaya hivyo
hatua ya kjwanza ni kuangalia eneo ambalo limeathirika na uharibifu ambapo tutawachukulia
hatua za kisheria wale waliongia kwenye hifadhi za misitu,” alisema Bw
Mwamfute.
Bw Mwamfute
alisema kuwa Misitu ya Uzigua zaidi ya nusu ya misitu hiyo imeharibiwa ambayo
ni hekta 24,436 kwenye msitu wa Uzigua huku ile ya mikoko hekta 70 zimeharibiwa
kati ya hekta zaidi ya 5,000.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
MKUU wa mkoa wa Pwani Bi Mwantumu Mahiza ni moja kati ya
wagombea watakaowania nafasi ya skauti mkuu wa Tanzania ambapo mchakato wa
kumpata unaendelea.
Akizungumza na waandishi wa habari Kamishna mkuu wa mkoa huo
Bw. Hamis Masasa alimpongeza mkuu wa mkoa wa mkoa wa Pwani kwa kuweza kujitokeza
kwenye mchakato huo na kushinda nafasi ya kwanza katika mchakato wa kumpata
Skauti mkuu wa Tanzania.
Alisema kuwa kutokana na kuongoza katika kinyang'anyiro
hicho kwa kuwashinda kwa kura 47 huku wagombea wengine wawili ambao wamepata kura 22
kila mmoja ambao ni Bw.Abdulkarim Shah Mbunge wa Mafia na Bw. Kajungumjuli
kutoka mkoa wa Mwanza.
“Baada ya hatua hiyo majina matatu
yatawasilishwa kwa Rais wa Chama cha skauti Tanzania, ambaye ni Waziri wa elimu
na mafunzo ya ufundi Bw Shukuru Kawambwa kama utaratibu unavyoelekeza ambaye
naye atayawakilisha kwa mlezi wa Chama cha Skauti Tanzania, Rais wa Jamhuri ya
muungano wa Tanzania, Dkt Jakaya Kikwete ambaye yeye atakuwa na jukumu la kuchagua jina
moja kati ya matatu yaliyochaguliwa ili kumpata skauti mkuu na badaye kuapishwa
kwa mujibu wa taratibu,” alisema Bw Masasa.
Aidha alisema kuwa Bi Mahiza
anauwezo wa kupanga mipango mbalimbali ya kumuendeleza kijana na mfano ni
uanzishaji wa kambi ya maarifa iliyokufanyika katika kijiji cha Msoga wilayani
Bagamoyo ambapo vijana walikusanywa kutoka wilaya za Mkoa wa Pwani na kupatiwa
mafunzo ya ujenzi wa nyumba kwa gharama nafuu na kuwezesha vijana hao kupatiwa
mashine za kufyatua tofali na mifuko 100 ya udongo ulaya.
Kwa hatua hiyo yeye kama kamishna wa
Skauti mkoa wa Pwani kwa niaba ya skauti wa mkoa huo amechukua fursa hiyo
kumpongeza mkuu huyo wa mkoa wa Pwani kwa kuweza kuongoza katika mchakato huo
na hasa ikizingatiwa toka amefika mkoa wa Pwani, Agenda yake kubwa imekuwa ni
maendeleo ya vijana na kuna uhakika mkubwa akibahatika kupata nafasi hiyo
ataweza kusaidia vijana wa nchi nzima badala ya wale mkoa wa Pwani pekee yake.
Mwisho.
Na
John Gagarini, Bagamoyo
KATIKA
kuwajengea uwezo Vijana Halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo imetenga kiasi cha
shilingi milioni 75 kwa ajili ya kuwakopesha vijana wanaojishughulisha na
biashara mbalimbali.
Akizungumza
na waandishi wa habari mwenyekiti wa kamati ya elimu,afya, na maji katika
halamshauri hiyo Bw Said Zikatimu alisema kuwa fedha hizo ni kutoka
kwenye mapato yake ya ndani kwa ajili ya kuwakopesha vijana
ambao wameunda vikundi vya ujasiriamali.
Bw Zikatimu alisema kuwa halmashauri
imetenga fedha hizo kwa lengo la kukabiliana na tatizo la ukosefu wa ajira
kwa vijana ili kupunguza kero hiyo kwa vijana wanaojitambua kwa kuanza
kijituma.
“Hadi sasa baadhi ya kata tayari zimenufaika kwa vijana
hao kuanzisha vikundi ambazo ni ikiwa ni pamoja na Zinga,Chalinze Saccos,Kerege
na Kiwangwa na kuzitaka kata nyingine kuanzisha saccos ili ziweze kupata fedha
hizo ambazo zimetengwa na Halmashauri,” alisema Bw Zikatimu.
Bw Zikatimu ambaye ni diwani wa kata
ya Talawanda alisema kundi la vijana halina mwamko katika masuala ya
kuunda vikundi vya ujasiliamali ambavyo kwasasa ndio mkombozi kwa wajasiliamali
walio wengi katika maeneo mbalimbali nchini.
“Vikundi mbalimbali vikiwemo vya
vijana vinasaidiwa kupata mikopo na misaada kwa urahisi mara panapotokea fursa
ya ufadhili kuliko kutoa msaada kwa mtu mmoja mmoja,” alisema Bw Zikatimu.
Aidha aliwaasa vijana hao kuachana
na tabia ya kukaa vijiweni kujadili masuala yasiyo na tija kwao badala ya
kushauriana kuanzisha vikundi vya ujasiliamali ili kupunguza wimbi la
vijana wasio na ajira wilayani humo.
Aliongeza kuwa mbali ya kundi la
vijana kutengewa fungu hilo pia wanawake wametengewa kiasi cha shilingi Milioni
65 kutoka mfuko wa Women Development Fund (WDF) ambao awali ulikuwa ukitoa
Milioni Kumi huku wanawake wakipewa mikopo kutokana na kuwa na sifa za yakuwa
na mwamko wa kuunda vikundi hivyo na
wengi wameshanufaika navyo.
Mwisho
Na John Gagarini, Bagamoyo
MEYA wa Mji wa Bagamoyo mkoa wa
Pwani Bw Abdul Sharif amewataka wananchi wa mji huo kutotupa takataka hovyo
ili kuepukana na mlipuko wa magonjwa ya mlipuko ukiwemo ule wa kipindupindu.
Akizungumzia hofu hiyo kwa
waandishi wa habari,mjini Bagamoyo ,Meya huyo alisema kutupwa ovyo kwa taka
hizo kunasababisha mvua zinazoendelea kunyesha kuzisomba taka na kuweka
mkusanyo wa mafungu ya uchafu.
Alisema kuwa kutokana na tabia ya
watu kutupa taka hovyo kuna hatari ya kutokea kwa magonjwa hayo ya mlipuko
hivyo hatua za dharura za kusafisha mji huo zinahitajika ili kuweka mji safi.
“Mamlaka ya mji mdogo imekuwa ikichukua
jitihada za makusudi mara kwa mara kusafisha na kuzolewa taka zinazolundikwa
lakini jitihada hizo zinakwama kutokana na kukosa fedha za kufanyia usafi,”
alisema Bw Sharif .
Aalisema kuwa Halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo imewapa jukumu la kusimamia usafi wa mji huo lakini bila kupewa nyenzo yoyote ,magari ya kubeba uchafu wala kiwango cha fedha na kupewa agizo la kushirikiana na idara ya afya ambayo nayo imesema imebaki na kiasi cha shilingi Milioni mbili ambazo hazikidhi mahitaji .
“Ukosefu wa fedha unasababisha
kushindwa hata kuzibua vyoo vya stendi kuu ambavyo vimekuwa vinatitirisha
vinyesi katika baadhi ya makazi ya watu pale mvua zinaponyesha na soko
linalotegemewa mjini humo limekuwa kama kisiwa kwa kuzungukwa na mabwawa ya
maji huku hali ya ndadi ya soko ni mbaya,” alisema Bw Sharif.
Aidha alisema Halmashauri inatakiwa kutafakari namna ya kusaidia mamlaka hiyo ili kuweka mji safi kwa manufaa hasa ikizingatiwa kuwa kuna wageni wengi wanaotembelea mji huo.
Hivi karibuni Mwenyekiti wa baraza
la madiwani wa halmashauri ya wilaya hiyo,Bw Shukuru Mbatto alisema yeye
binafsi anachukua dhima ya kwenda kutembelea katika eneo hilo na kuhakikisha
anakaa na Mkurugenzi mtendaji wa wilaya ya Bagamoyo ili kutatua tatizo hilo
lakini hadi sasa mambo yanakwenda ndivyo sivyo.
Mwisho
|
Na John Gagarini, Kibaha
IMEELEZWA kuwa kitengo cha Dawati la jinsia na watoto kinakabiliwa na
changamoto ya watu kuwa na mwamko mdogo kutoa taarifa juu ya unyanyasaji wa kijinsia
hali inayosababisha vitendo hivyo kukithiri.
Kwa mujibu wa katibu wa Dawati hilo lililopo kwenye ofisi ya Jeshi la
polisi Mkoa wa Pwani, Bi Mwamshamba Rashid alisema wakati wa mafunzo juu ya
ukatili yaliyoandaliwa kikundi cha Inuka.
“Vitendo hivyo vinakithiri kwa kiasi kikubwa pembezoni mwa miji kutokana
na ushirikiano hafifu hivyo kuna kila sababu ya kujenga ukaribu ili
kutokomeza vitendo hivyo,” alisema Bw Rashid.
Aidha Bi Rashid alibainisha kuwa suala hilo si la wanaofanyiwa pekee bali linaigusa jamii inayowazunguka wahusika hivyo wananchi watambue ushirikiano utasaidia urahisi wa utendaji kazi dawati hilo.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa
Kikundi cha wajasiliamali cha Inuka Bw David Msuya aliipongeza serikali
kwa uongozi kwa kuzingatia utawala bora na uwajibikaji uliopelekea matukio
ya uhalifu mbalimbali nchini ikiwemo ujambazi kupungua.
Bw Msuya ambae pia ni mwanasheria wa kujitegemea alisema jitihada za dhati
zilizowezesha kutokomeza matukio hayo zinalipa imani taifa kwa kuwa na imani na
serikali yao.
Mafunzo hayo ya kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia na watoto, yalifanyika
Mwendapole, Kibaha na kuandaliwa na kikundi cha Inuka na kuendeshwa na dawati
hilo kutoka Jeshi la Polisi Mkoani Pwani.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
KUFUATIA kuanzishwa kwa benki ya Familia ya Jumuiya ya Wazazi wilaya ya
Kibaha mkoani Pwani wajasiriamali wengi wamejitokeza kukopa kwa ajili ya
kuendeleza shghuli zao za ujasiriamali.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake katibu wa Jumuiya hiyo
Kibaha Mjini Bw David Mramba alisema kuwa hadi sasa watu zaidi ya 400
wamejitokeza kukopa fedha hizo ambazo zinatolewa kwa vikundi vya watu watano
watano.
Bw Mramba alisema kuwa kwa sasa wanaendelea kupokea maombi ikiwa ni
pamoja na kuwasajili ili waeze kuwa na akaunti kwa ajili ya kuwekea akiba zao.
“Malengo ni kupata watu 800 lakini kwa kasi hii watu wanaweza kufikia 1,000
ambao wanataka kukopa fedha kwa ajili ya shughuli zao za ujasiriamali,” alisema
Bw Mramba.
Alisema kuwa benki hiyo ya familia ilitenga kiasi cha shilingi millioni
800 kwa ajili ya wakopaji kwenye wilaya kwa lengo la kuwainua wajasiriamali
wadogo.
“Mara taratibu zitakapokamilika tutawakopesha na zopezi linaendelea
vizuri kwani watu wengi wanajitokeza kutaka kukopa hasa ikizingatiwa masharti
yaliyowekwa ni mepesi tofauti na sehemu zingine,” alisema Bw Mramba.
Aidha alisema kuwa changamoto kubwa wanayoipata ni baadhi ya wananchi
kuwa na hofu kwani baadhi ya taasisi za kifedha ziliondoka na fedha zao.
“Lengo ni kuwainua wajasiriamali wadogo wadogo ili nao waweze kuinua biashara zao ndiyo
sababu tumeweka taratibu rahisi ili kila mtu aweze kukopa bila ya kujali chama,”
alisema Bw Mramba.
Aliwataka wananchi kujitokeza kukopa kwani masharti yaliyopo ni nafuu kwa
mtu yoyote kuweza kukopa ambapo riba yake ni ndogo sawa na asilimia moja tu.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment