Na John
Gagarini, Bagamoyo
SAKATA la
viongozi wa Vijiji kuondolewa madarakani limezidi kushika kasi kwenye kata ya
Vigwaza wilayani Bagamoyo ambapo juzi wananchi wa Kijiji cha Ruvu Darajani
wameuondoa madarakani uongozi wa Kijiji hicho.
Vijiji vingine
ambavyo uongozi wake umeondolewa na wananchi kwenye mikutano ya Kijiji ni
Kitonga na Milo ambo wamewaondoa viongozi wao kutokana na tuhuma mbalimbali.
Wananchi wa
Kijiji cha Ruvu Darajani waliukataa uongozi huo kwa tuhuma za kutoa eneo la
soko kwa mwekezaji bila ya kupitishwa na wananchi ambao ndiyo wenye ridhaa ya
kukubali maeno kupewa watu kwa ajili ya kuwekeza.
Uongozi huo chini
ya Mwenyekiti Bw Kambona Athuman Kwaro na ofisa mtendaji wake Bi Mwajuma Bigo na
wajumbe wa halmashauri ya Kijiji uliondolewa kwenye mkutano wa dharura ambao uliitishwa kwa lengo la kuwapitisha
wawekezaji walioomba maeneo kwa ajili ya
kuwekeza.
Mwenyekiti huyo
bila ya kujua kilichokuwa kikiendelea alifungua mkutano na kusema kuwtaakuwa na
ajenda mbalimbali lakini kubwa ilikuwa ni kuwapitisha wawekezaji hao ili
wapatiwe hati za kumiliki maeneo hayo kwa kipindi watakachokuwa wamekubaliana.
Wananchi hao
waliwapinga wawekezaji hao huku wakiwa na mabango wakiwataka viongozi wao
kuachia ngazi na kusema kuwa mazingira ya kuwapitisha hayakuwahusisha wao hivyo
hawako tayari kuwakubali kuwekeza kwenye kijiji hicho kwani kwa kipindi
walioomba hawajaweza kutoa mchango ndani ya Kijiji.
“Mbali ya
wawekezaji hawa wengine kilichotuudhi zaidi ni uongozi kumpa mwekezaji eti
ajenge ofisi kwenye eneo ambalo lilipangwa kwa ajili ya soko na tayari
kulishawekwa mabanda ambayo yameondolewa na kibaya hawajatushirikisha
tunashangaa mtu kaanza kujenga,” alisema Bw Athuman Mnyamani.
Bw Mnyamani
alisema kuwa maeneo mengi yametolewa kinyemela huku maeneo mengine
wamewaongezea ukubwa tofauti na makubaliano ambapo hili eneo la soko
walikubaliana ajenge lakini leo wanaitisha mkutano kutaka tumkubali au kumkataa
wakati ameanza ujenzi kwa kuchimba msingi.
“Hapa hatuna
hata maeneo ya wazi kwani yote yametolewa kwa wawekezaji ambao hatuoni manufaa
yao kwani wanaahidi wakishapewa maeneo hayo hawatoi msaada wowote hivyo
hawastahili kuwa viongozi ndiyo sababu ya sisi kuwakataa,” alisema Bw Mnyamani.
Akijibu tuhuma
hizo mwenyekiti Bw Kwaro alisema kuwa ni kweli walikubalina na mwekezaji huyo
kujenga ofisi kwa ajili ya mambo ya biashara lakini tulimwambia aanze ujenzi
mwezi huu na si mwezi uliopita jambo ambalo alikwenda kinyume na kuanza
kuchimba msingi.
“Tulikubaliana
aanze ujenzi januari lakini yeye aliwahi na wakati anafanya hivyo mimi sikuwepo
na tulimkubalia kwa nia njema hakukuwa na jambo lolote la kificho ambapo kama
kijiji hakina uwezo wa kujenga hivyo tulikubaliana atakuwa akikilipa kijiji
kiasi cha shilingi 100,000 kwa mwezi,” alisema Bw Kwaro.
Kutokana na
majibu hayo watu walianza kupiga kelele za kusema kuwa hawana imani na uongozi
huokila mtu aliyetakiwa kuuliza swali au akutoa mchango wake alikuwa akisema
uongozi uondoke madarakani huku wananchi wengine wakizomea.
Kwa upande
wake ofisa mtendaji wa kata ya Vigwaza Bw Masukuzi Masukuzi alijaribu kuwazuia
wananchi hao kuacha makelelena vurugu na
kutoa hoja zao za msingi ili maamuzi yaweze kuwa sahihi.
“Kama mlivyoona
wananchi wametoa kauli moja kuwa hawautaki uongozi na kikubwa ni tuhuma kuwa
wametoa maeneo bila ya ridhaa yao likiwa hili la hapa ambapo ni makosa kwani
wananchi ndiyo wenye maamuzi ya kumkubali au kumkataa mwekezaji,” alisema Bw
Masukuzi.
Kutokana na
wananchi kuukata uongozi inabidi nafasi hiyo kuongoza ichukuliwe aidha na
mwalimu mkuu wa shule au ofisa ugani hadi pale halmashauri itakapotoa utaratibu
mwingine namna ya kupata uongozi mwingine.
Wananchi hao
kwa pamoja walimpitisha mwalimu mkuu wa shule ya msingi Ruvu Darajani Bi Meri
Nzowa kuongoza Kijiji hicho hadi utakapochaguliwa uongozi mwingine. Mkutano huo
ulihudhuriwa na diwani wa kata hiyo Bw Mbegu Dilunga na mkuu wa kituo cha
polisi Vigwaza Bw Salim Msangi
Mwisho.
No comments:
Post a Comment