Na John
Gagarini, Kibaha
HATIMAYE
wakazi wa mtaa wa Tangini wilayani Kibaha mkoani Pwani wameridhia kuwekwa
kalavati kwenye eneo ambalo walidai halmashauri imehamisha mkondo wa maji ya
mvua na kuuelekeza kwenye makazi ya watu.
Pande hizo
mbili zilifikia makubaliano baada ya mkurugenzi wa halmashauri Bi Jenifa Omolo
na Injinia Bw Ezekiel Kunyaranyara kufika kwenye eneo hilo na kufikia
makubaliano.
Wananchi hao
walifikia hatu ya kumzuia mkandarasi wa barabara kuweka klavati hilo kutokana
na kupata vitisho kutoka kwa wakazi hao.
Moja ya
wakazi wa mtaa huo Bw Michael Mwambashi alisema walizuia kuwekwa kalavati kwani
halmashauri ilihamisha mkondo wa maji na kuelekezea kwenye nyumba za watu
badala ya kutumia mkondo wa zamani.
“Baada ya
kupata ufafanuzi tumekubaliana waweke kisima kwa ajili ya kutuliza kasi ya maji
kisha yaendee mbele lakini awali hawakutuambia kuwa watachimba kisima,” alisema
Bw Mwambashi.
Kwa upande
wake Injinia Bw Kunyaranyara alisema kuwa eneo walilokuwa wakitaka maji yapite
si sahihi kwani tayari maji ya mvua yamebadilisha mwelekeo hivyo kalavati
lazima liwekwe eneo jingine na si pale walipokuwa wakitaka wananchi.
“Lengo ni
maji haya ya mvua yasileta madhara kwenye nyumba za watu na si kama watu
wanavyofikiri na hatuna nia mbaya hata hivyo tumefikia makubaliano na
wamekubali kama tulivyowashauri,” alisema Kunyaranyara.
Naye mkandarasi
wa barabara za halamshauri ya Mji wa Kibaha Bw Lebulu Mfinanga alisema kuwa
baadhi ya watu wamejenga kwenye maeneo ambayo ni njia ya maji hali
inayosdababisha malumbano wakati wa kujenga barabara.
Aliwataka wananchi
kujenga kwa kufuata ramani ya Mji ili kuondoa migogoro kama hiyo ambayo
imesababisha kuchelewa kukamilika kwa barabara ambazo amekabidhiwa na
halmashauri.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment