Na John Gagarini, Kibaha
JESHI la Polisi mkoa wa Pwani limetakiwa kudhibiti uhalifu
kuanzia ngazi ya familia ambako ndiko chimbuko la vitendo hivyo.
Hayo yalisemwa jana na mkuu wa mkoa wa Pwani Bi Mwantumu
Mahiza alipokuwa akikabidhi pikipiki 25 kwa wakaguzi wa polisi ngazi ya Tarafa
kwenye mkoa huo.
Alisema kuwa uhalifu huo ukidhibitiwa kuanzia ngazi hiyo
utasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza uhalifu na jamii zitaishi kwa amani.
“Tukianza kudhibiti ngazi ya familia itapunguza matatizo hayo
na kuimarisha maendeleo na ustawi wa jamii,” alisema Bi Mahiza.
Bi Mahiza alisema kuwa pikipiki hizo zitasaidia kukabiliana
na uhalifu hivyo kuna haja ya kufikia ngazi hiyo ambapo baadhi ya wahalifu
wanatoka ndani ya familia.
“Mpango huu utakuwa daraja la kuunganisha kila familia katika
kutambua viashiria vya vya uvunjifu wa amani pia kuwa na stadi za utatuzi wa
migogoro,” alisema Bi Mahiza.
Kwa upande wake kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani Ulrich Matei
alisema kuwa jeshi la polisi lilizindua mradi huo wa kuzuia uhalifu ndani ya
jamii mwaka huu kitaifa.
“Wahalifu wengi hutokea ndani ya familia hivyo mkakati huu wa
kifamilia katika kuzuia uhalifu utasaidia kutokomeza uhalifu,” alisema Bi
Mahiza.
Kamanda Matei aliwaomba wadau mbalimbali kujitokeza kutoa
ushirikiano kwa jeshi lake
ili kuweza kubaini vyanzo
vya uhalifu hasa ndani ya jamii.
Na John Gagarini, Kibaha
WAKAZI wa Mkoa wa pwani hususani wa wilaya ya Kibaha
wametakiwa kuwa na imani na serikali katika kutatua changamoto ya maji kwani
bunge limeidhinisha kiasi cha bilioni 27 kwa ajili ya kuboresha chanzo cha maji
cha mto Ruvu.
Akizungumza na wakazi wa kata ya Kongowe wilayani Kibaha
mbunge wa Viti Maalumu toka mkoa wa Pwani, Bi Subira Mgalu wakati wa ziara ya
Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) na kusema kuwa changamoto hiyo karibu
itapatiwa ufumbuzi.
Alisema kuwa serikali inatambua kero wanayoipata wakazi wa
Kibaha kutopata maji ya uhakika licha ya chanzo cha maji kuwa kwenye wilaya
hiyo.
“Serikali iko kwenye mchakato wa kulipatia ufumbuzi suala hilo na ndiyo sababu
bunge limeridhia kutumika fedha hizo ili kuboresha chanzo hicho cha Ruvu ili
wakazi wa Kibaha wapate maji ya uhakika,” alisema Bi Mgalu.
Alisema mbali ya kuboresha chanzo hicho pia serikali kupitia
benki ya dunia ambapo awamu ya kwanza imeshakamilika sasa itaakuja awamu ya
pili kwa vijiji.
“Nawataka watendaji, madiwani kuwajibika ipasavyo kwani sasa
hivi si wakati wa kupoteza muda kinachotakiwa ni kazi tu na kila mmoja atomize
wajibu wake ili kuwaletea maendeleo wananchi,” alisema Bi Mgalu.
Bi Mgalu ambaye ni mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM pia mkuu
wa wilaya ya Muheza mkoa wa Tanga alisema kuwa wakazi wa mkoa wa Pwani
wanapaswa kuwapeleka watoto wao shule hususani kwenye chuo cha ufundi stadi
VETA kilichopo Kongowe mkoani humo.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment