Na John
Gagarini, Kibaha
WANANCHI
wenye hasirakali wa Kitongoji cha Umwelani eneo la Kibaha Kwa Mathiasi mkoani
Pwani wamemwua mtu anayedhaniwa kuwa ni mwizi baada ya kuvunja nyumba na kuiba.
Akizungumza na
waandishi wa habari ofisini kwake kamanda wa Polisi mkoani humo Ulrich Matei alisema
kuwa mtu huyo alikuwa na wenzake wawili ambao walikimbia mara baada ya tukio
hilo.
Alisema kuwa
tukio hilo lilitokea Januari 14 mwaka huu majira ya saa 8 usiku, ambapo watu
hao walivamia nyumbani kwa Bi Mwajab Shaban (30) mfanyabiashara wa eneo hilo.
“Watu hao
walivunja nyumba hiyo kwa kutumia jiwe kubwa maarufu kama fatuma kisha kuingia
ndani ndipo mlalamikaji alipopiga simu kwa majirani wakati huo wezi hao
walikuwa wakiwa kwenye chumba cha watoto ndipo watu walipofika na kumkamata
marehemu kisha kumpiga hadi kumwua,” alisema Matei.
Alisema kuwa
watu hao walifanikiwa kuiba na kuiba vitu
mbalimbali ikiwa ni pamoja na fedha taslimu kiasi cha shilingi 400,000, simu
mbili aina ya Techno zenye tahamani ya shilingi 100,00 na Dvd Player yenye
thamani ya shilingi 65,00.
“Katika eneo
la tukio kulipatikana waya wa kufyatulia baruti ambapo wezi hao hutumia
kuwatisha watu kabla ya kufanya uhalifu, hata hivyo kitendo cha kumwua mhalifu
si kitendo chema kwani wangempeleka kwenye vyombo vya sheria ili hatua
zichukuliwe,” alisema Matei.
Aidha alisema
kuwa mwili wa marehemu umehifadhiwa kwenye hospitali ya Tumbi kwa uchunguzi wa
wa daktari na hakuna mtu aliyekamatwa kuhusiana na mauji hayo na juhudi za
kuwasaka wezi hao zinaendelea.
Aliwataka wananchi
kutojichukulia sheria mkononi kwani vitendo vya kuwaua wahalifu ni kinyume cha
sheria kwani watuhumiwa wanapaswa kupelekwa kwenye vyombo vya sheria.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment