Wednesday, January 23, 2013

WANAFUNZI WADAKWA


Na John Gagarini, Kibaha
WANAFUNZI 12 wa shule ya Sekondari ya  Kata ya Maili Moja wilayani Kibaha mkoani Pwani wamekamatwa na mgambo wa kata hiyo wakiwa vichakani huku wengine wakikutwa na kondomu kwenye mifuko yao.
Tukio hilo lilitokea juzi mjini Kibaha baada ya mgambo hao kuendesha opereshani kuwakamata wanafunzi ambao hawaingii madarasani na kuishia njiani.
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye ofisi ya Kata ya Maili Moja mara baada ya kukamatwa wanafunzi hao, diwani wa kata Bw Andrew Lugano alisema kuwa zoezi hilo ni endelevu kwani baadhi wanafunzi wamekuwa hawafiki shuleni.
“Baada ya kuona kuwa wanafunzi wamekithiri kwa utoro shule ileta suala hili ngazi ya kata na sisi tliamua kuchukua hatua kuwatuma mgambo kuwasaka wanafunzi ambao hawaingii madarasani tulifanikiwa kuwakamata wanafunzi hao ambao ni wa kidato cha tatu na nne,” alisema Bw Lugano.
“Tuliwapekua ambapo tuliwakuta na baaadhi ya vitu ikiwemo ni pamoja na simu na kondomu jambo ambalo ni kinyume cha taratibu za shule na kesho baraza la kata litakaa pamoja na wazazi wao ambao tumewaandikia barua ili waje na ndipo maamuzi yatatolewa dhidi yao,” alisema Bw Lugano. 
Aidha alisema kuwa kata itahakiksha wanafunzi wa shule hiyo wanazingatia maadili ya shule na kuachana na vitendo ambavyo ni kinyume na maadili na wataendeleza operesheni hiyo ili kusafisha shule hiyo ili itoe matokeo mazuri.
Kwa upande wake mwalimu mkuu wa shule hiyo Flora Chibululu alisema kuwa shule yao imekuwa ikidhibiti wanafunzi ambao hawafiki shuleni lakini imekuwa ngumu kwani licha ya kutoa adhabu lakini bado wanafunzi hao hawabadiliki.
Bi Chibululu alisema kuwa wamekuwa wakitoa adhabu zikiwemo za kuwataka wakae nyumbani kwa muda Fulani lakini bado vitendo hivyo bado vinaendelea hali iliyosababisha kuomba kusaidiwa na kata hiyo ambayo iliwapa mgambo kufanya hivyo.
Aliwataka wazazi kutoa ushirikiano kwa shule ili wanafunzi waweze kupata elimu bora kwani vitendo hivyo vinasababisha elimu kushuka kutokana na wanafunzi kutojituma na kufanya matokeo kuwa mabaya.
Mwisho.   
Na John Gagarini, Kibaha
TIMU ya soka Lisborn ya Kongowe wilayani Kibaha imeifunga timu ya Veteran kwa magoli 3-0 kwenye mchezo wa kuwania ngombe wa Mbepo Cup.
Mchezo huo ulipigwa jana kwenye uwanja wa Mwendapole wilayani Kibaha mkoani Pwani ulikuwa mkali na wa kuvutia na kuwakusanya mashabiki wengi akiwemo Diwani wa Kata ya Kibaha Said Nangurukuta na Meya wa Mji wa Kibaha Adhudadi Mkomambo.
Washindi walipata mabao hayo kupitia kwa mshambuliaji wao mahiri Kulwa Mwanda akishirikiana na Jesse Joseph Magoli.
Kulwa alifunga magoli hayo kwenye dakika za 22,64 na 72, michuano hiyo itaendelea Januari 26 mwaka huu kwa mchezo baina ya Mwanalugali na Cargo.
Kutokana na matokeo hayo timu za Nyumbu, Kigogo na Palasupalasu zimefanikiwa kuingia hatua ya robo fainali.
Akiongelea mashindano hayo diwani wa kata ya Kibaha Nangurukuta alisema kuwa mashindano hayo yamefanikiwa kukusanya vipaji vya vijana kwenye kata hiyo na zingine na wilaya ya Kibaha.
Nangurukuta aliwataka wakazi wa eneo hilo kujitokeza kwa wingi ili kuwahamasisha vijana wao kushiriki michezo na kukuza vipaji vyao kwani mbali ya kuboresha afya pia ni ajira kwao.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment