Wednesday, January 9, 2013

KRFA KUFANYA USAILI JANUARI 14 MWAKA HUU


Na John Gagarini
CHAMA cha soka mkoa wa Kilimanajaro (KRFA) kitafanya usaili kwa wadau walijitokeza kujaza nafasi za uongozi  Januari 14 mwaka huu.
Akizungumza kwa njia ya simu msemaji wa chama hicho Yusufu Mazimu alisema kuwa uchaguzi wa kujaza nafasi hizo uitafanyika Januari 26.
Mazimu alisema kuwa hadi sasa ni wadau sita waliojitokeza kujaza nafasi hizo ambazo zilibaki wazi kutokana na wagombea kutokuwa na sifa kwenye uchaguzi wa chama hicho uliofanyika Septemba 29 mwaka jana.
“Kwa muda uliobaki tunaomba wadau mbalimbali wajitokeze ili kuwania nafasi hizo ili kukifanya chama kuwa na uongozi uliokamilika kwani kwa sasa uongozi bado haujakamilika,” alisema Mazimu.
Alizitaja nafasi hizo zilizobaki wazi kuwa ni pamoja na makamu mwenyekiti, katibu msaidizi, mjumbe kwenda TFF, mwakilishi wa soka la wanawake na wajumbe wawili wa kamati ya utendaji.
“Gharama ya fomu kwa nafasi za juu ni shilingi 100,000 huku nafasi za ujumbe zikitolewa kwa shilingi 50,000 ambapo tunawaomba wadau wajitokeze kabla ya muda wa usaili kwisha,” alisema Mazimu.
Mwisho.
Na John Gagarini
TIMU za soka za Polisi na Magadini zinatarajiwa kuchuana kwenye ligi daraja la Tatu mkoa wa Kilimanajaro Jumamosi Januari  12 mwaka huu.
Kwa Mujibu wa Msemaji wa Chama Cha soka Mkoa wa Kilimanjaro KRFA Yusufu Mazimu alisema kuwa mchezo huo utapigwa kwenye kituo cha VETA.
Mazimu alisema kuwa siku ya Jumapili Januari 13 kutakuwa na mchezo baina ya timu za Panone na Kitayosce kwenye kituo hicho.
Katika kituo cha Holili utapigwa mchezo baina ya Mwanga Asilia na Machava huku Jumapili ikiwa ni kati ya Kurugenzi na Bodaboda.
Kwenye michezo iliyopita Machava imeicharaza Bodaboda kwa magoli 2-1.
Mchezo huo ulipigwa kwenye uwanja wa Holili magoli ya washindi yalifungwa na Adam Soba dakika ya 29 na Issa Kipese dakika ya 80 na la Bodaboda lilifungwa na Paul Wliam dakika ya 17.
Kwenye kituo cha Himo Kilimanajaro iliifunga Vijana kwa magoli 2-1 wafungaji wakiwa ni Omary Juma dakika ya 24 na Ramadhan Gumbo dakika ya 36  la vijana lilifungwa na Abdala Husein dakika ya 75.
Timu ya Polisi Hai iliifunga KIA kwa mabao 4-0 mchezo uliopigwa kituo cha VETA Soweto na Forest walishindwa kutambiana baada ya kutoka suluhu ya 0-0.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment