Thursday, January 24, 2013

WANAFUNZI WALIOKUTWA NA KONDOMU WAADHIBIWA


Na John Gagarini, Kibaha
HATIMAYE wanafunzi wa sekondari ya Kata ya Maili Moja wilayani Kibaha mkoani Pwani waliokamatwa na mgambo wa kata kwa tuhuma za kutoingia madarasani na kuishia vichakani na kukutwa na kondomu wameadhibi kwa kuchapwa viboko.
Wanafunzi hao walipata adhabu hiyo jana baada ya baraza la kata kuwakuta na hatia ya kujihusisha na vitendo kinyume na taratibu za shule.
Kwa mujibu wa mwenyekiti wa baraza la kata Bw Amadeus Ngombale alisema kuwa wanafunzi hao walikiri kujihusisha na vitendo hivyo kinyume cha maadili ikiwa ni pamoja na kukutwa na kondomu na simu.
“Baada ya kukiri baraza lilitoa adhabu ya viboko kutegemea na kosa la mhusika ambapo adhabu hizo za viboko walichapwa na wazazi wao ambao nao walitwa kwenye baraza hilo,” alisema Bw Ngombale.
Bw Ngombale alisema kuwa wao kama baraza walishatoa adhabu yao na wanatakiwa Jumatatu Januari 28 wanatakiwa kwenda shuleni na wazazi wao ili wapewe taratibu nyingine za shule.
“Bodi ya shule ndiyo itakayoamua hatma ya wanafunzi hao kama watapewa adhabu nyingine au kuwasamehe hilo litaamuliwa na bodi ya shule kwa lengo la kurejesha nidhamu kwa wanafunzi hao,” alisema Bw Ngombale.
Wanafunzi hao waliomba msamaha na kukiri kuwa hawatarudia tena kwani walifanya vitendo hivyo kwa kuiga tu mambo ya ujana.
Wanafunzi hao walikamakamatwa juzi na mgambo wa kata hiyo kwani walikuwa hawaingii madarasani na kuishia njiani huku wengine wakiwa vichakani na kukutwa na kondomu kwenye mifuko yao.


Mwisho.

No comments:

Post a Comment