Tuesday, January 15, 2013

MAOFISA ARDHI KUSHUGHULIKIWA


Na John Gagarini, Bagamoyo
MKUU wa wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani Bw Ahmed Kipozi ametaka apewe majina ya ofisa aliyetoa viwanja kwenye hifadhi ya Misitu ya Mikoko wilayani humo.
Akizungumza na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya mara baada ya zira kutembelea misitu ya hifadhi ya Uzigua na Mikoko iliyoandaliwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Bagamoyo na kusema uharibifu uliofanyika alisema kuwa misitu hiyo imeharibiwa kwa kiasi kikubwa.
Bw Kipozi alisema kuwa inashangaza kuona maofisa hao kugawa viwanja kwenye hifadhi ya misitu badala ya kutoa viwanja kwenye maeneo yaliyotengwa maalumu kwa ajili ya viwanja.
“Siwezi kukubaliana na watu ambao hawawajibiki ipasavyo kwani inashangaza kuona kuwa watu wanatoa maeneo ambayo ni hifadhi kwani misitu ni muhimu kwa viumbe hai hivyo nataka niwajue waliofanya hivi ili hatua ziweze kuchukuliwa,” alisema Bw Kipozi.
Aidha alisema kuwa watu waliopewa viwanja kwenye maeneo hayo ya hifadhi ya mikoko wamekata miti hiyo ambapo baadhi walikata ili kuona madhari ya bahari na wengine walianzisha miradi ya samaki.
“Wameharibu hifadhi hii kwa kiasi kikubwa kwani kila mtu anaelewa umuhimu wa misitu kwani kukata miti kuna athari nyingi ikiwa ni pamoja na ukosefu wa mvua kuharibu mazalio ya samaki na kubadili uoto wa asili hivyo lazima wahusika wawajibike,” alisema Bw Kipozi.
Kwa upande wake meneja wa wilaya ya Bagamoyo Bw Charles Mwamfute alisema kuwa hifadhi za misitu hiyo zimeharibiwa na watu kwa ajili ya kukata miti, kuchoma mkaa na wafugaji kuingia kwenye misitu hiyo.
“Sisi wakala mpya ambao umeanzishw akwa ajili ya kulinda misitu ya asili kila wailaya hivyo hatua ya kjwanza ni kuangalia eneo ambalo limeathirika na uharibifu ambapo tutawachukulia hatua za kisheria wale waliongia kwenye hifadhi za misitu,” alisema Bw Mwamfute.
Bw Mwamfute alisema kuwa Misitu ya Uzigua zaidi ya nusu ya misitu hiyo imeharibiwa ambayo ni hekta 24,436 kwenye msitu wa Uzigua huku ile ya mikoko hekta 70 zimeharibiwa kati ya hekta zaidi ya 5,000.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment