Sunday, January 20, 2013

WATATU WAFA AJALINI


Na John Gagarini
WATU watatu wamefariki dunia na wengine  11 kujeruhiwa baada ya gari walilokuwa wakisafiria kugongana na pikipiki.
Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoa wa Pwani Ulrich Matei alisema kuwa ajali hiyo ilitokea jana majira ya mchana eneo la Msata- Kihangaiko wilayani Bagamoyo.
Kamanda Matei alisema kuwa watu hao waliofariki wawili waliokuwa wamepakia pikipiki na dereva wa basi la Jay.
 “Chanzo cha ajali hiyo ni mwendo wa kasi wa basi la Jay lenye namba za usajili T 732 AFP lililokuwa likitoka Morogoro kwenda mkoani Tanga na kugongana ambapo watu wote walifia papo hapo,” alisema Kamanda Matei.
Aliwataja waliokufa kuwa ni Bw Sindi Kombo (48) mkazi wa Tanga ambaye ni dereva wa basi, Bw Mangulu Idd (48) fundi bomba na Bi Sharifa Omary (42).
Aidha alisema kuwa maiti wamehifadhiwa zahanati ya Msata huku majeruhi wakiwa wamepelekwa hospitali ya Chalinze na Lugoba ambapo wangine watahamishiwa hospitali ya Tumbi kwa matibabu zaidi.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment