Na John Gagarini, Kibaha
JUMUIYA ya
Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Pwani imesema kuwa imeandaa
mawakili ili kuhakikisha mali zote za Jumuiya hiyo zilizouzwa au kuchukluliwa
kinyume cha sheria zinarudi.
Hayo yalisemwa
jana na mwenyekiti wa mkoa wa jumuiya hiyo Bw Jackson Josian wakati akizungumza
na waandishi wa habari mara baada ya kufungua semina juu ya uajasiraiamali kwa
viongozi wa Jumuiya Kibaha Mjini.
Alisema kuwa
Jumuiya hiyo ina mali nyingi ambazo baadhi zimechukuliwa au kuuzwa kinyume cha
sheria jambo ambalo linafanya washindwe kujitegemea licha ya kuwa na rasilimali
na tayari wameshawapata mawakili ili kurejesha mali hizo kisheria.
“Tuna
rasilimali nyingi ambazo tunatarajia kuzirejesha kwani nyingine zimeporwa
lakini tutahakikisha kuwa mali zote zinarudi mikononi mwetu ili kujenga uchumi
wa Wazazi na chama kwa ujumla,” alisema Bw Josian.
Alizitaja baadhi
ya mali za Jumuiya kuwa ni pamoja na shule, viwanja na mashamba ambapo baadhi
ya viongozi wa Jumuiya hiyo wamehusika kusababisha mali hizo kupotea katika
mazingira ya kutatanisha.
Kwa upande
wake mwenyekiti wa Jumiya ya Wazazi Kibaha Mjini Dkt Athuman Mokiwa alisema
kuwa moja ya lengo la semina hiyo ni kuwafundisha juu ya kulinda mali za
Jumuiya.
Dkt Mokiwa
alisema kuwa viongozi wengine wameshindwa kabisa namna ya kusimamia miradi ya
Jumuiya hiyo na kuifanya mingine iyumbe ambapo ingesimamiwa vema ingekuwa
mkombozi ndani ya chama.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment