Na John
Gagarini, Kibaha
BONDIA machachari anayechipukia wa Maili Moja
wilayani Kibaha mkoani Pwani Zumba Nkukwe (Chenchi Dola) anatarajia kuzikipiga
na bondia Maisha Samson wa Mbeya mwaka mpya Januari Mosi 2013.
Chenchi Dola
alisema kuwa yuko sawasawa kwa ajili ya pambano hilo ambalo litapigwa wilaya ya
Kyela mkoani Mbeya.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mjini Kibaha jana alisema kuwa hana wasiwasi na bondi huyo kwani amefanya mazoezi ya kutosha chini ya mwalimu
wake aitwaye Poti ambapo mazoezi yake amekuwa akiyafanya Jijini Dar es Salaam.
“Nimejiandaa
vya kutosha na siogopi bondia yoyote kwani nimejiandaa ipasavyo na hata raundi
ya tatu hatafika ijapokuwa yeye atakuwa yuko nyumbani mbele ya mashabiki wake,”
alisema Chenchi Dola.
Alisema kuwa
watu wa Kyela wanatakiwa wajipange sawa sawa kupata burudani ya nguvu siku ya
kufungua mwaka wa 2013 na ndipo anapoanza safari yake ya kuapambana na mabingwa
waliopo sasa.
“Malengo
yangu ni kuja kupambana na mabondia wakubwa wanaotamba kwa sasa ili tuweze
kwenda sawa kwani malengo yangu ni kuwa bingwa kwani nitajiweka sawa ili nije
kupambana na bondia mmoja wapo maarufu,” alisema Chenchi Dola.
Kwa upande
wake meneja wa bondia huyo Ibrahim Kame kutoka TPBO alisema kuwa lengo la pambano
hilo ni kutafuta mshindi ambaye atashiriki kwenye mashindano mbalimbali ili
kujiongezea uzoefu.
“Bondia
Chenchi Dola ni mzuri na natarajia atafanya vizuri na kumshinda mpinzani wake
na baadaye tutamtafutia mapambano mengi zaidi ili aweze kuonyesha kipaji chake,”
alisema Kame.
Aliongeza kuwa
katika pambano hilo mabondia wakongwe kama vile Rshid Matumla “Snake Boy” na
Maneno Oswald “Mtambo wa Gongo” watakuwepo kuangalia vijana wanavyopambana.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment