MTOTO Fred Wiliam (4) ambaye ana uvimbe kichwani kwenye shavu hadi shingoni akiwa amekaa huko nyumbani kwao kijiji cha Mizuguni wilayani Kibaha Vijijini Mkoani Pwani Picha na John Gagarini. |
Na John Gagarini, Pwani
MTOTO Fred Wiliam mwenye umri wa miaka
(3) anaishi kwenye hali ngumu kutokana na kutokwa na uvimbe kichwani ambao
unamsababishia maumivu makali na kumsababisha kukosa raha kwa muda mwingi.
Mwandishi wa habari hizi alifika
kijijini hapo akiwa na baadhi ya viongozi wa chama cha albino Tanzania (CCT)
mkoa wa Pwani kwa lengo la kufanya sensa na mahitaji ya watoto wenye ulemavu
kwenye kata ya Magindu iliyofadhiliwa na shirika la Plan International tawi la
Kibaha.
Mtoto huyo anaishi katika Kijiji cha
Mizuguni kata ya Magindu mbali ya kuwa na maumivu hayo pia anapata maumivu
mengine ya kumpoteza mama yake mzazi ambaye alifariki mwaka jana hivyo
kumwongezea simanzi kubwa.
Anaonekana kuwa ni mchangamfu huku
akicheza na wenzake pamoja na kaka yake ambaye alimleta kwa mwandishi baada ya
kuambiwa kuwa kuna mtoto ana matatizo ya kutoka uvimbe kwenye kichwa chake hali
ambayo alizaliwa nayo.
Mtoto huyo yuko kwenye wakati mgumu
kwani mama yake alifariki dunia na kumwacha akiwa bado mdogo huku akiwa na
uvimbe huo na hali ni mbaya sana
kwani wakati mwingine anapata maumivu makali na kuishia kulia tu
Baba wa mtoto huyo ni mkulima pamoja
na kuchoma mkaa humwacha muda mwingi peke yake akiwa amekwenda kwenye shughuli
zake hizo za kujiongezea kipato cha familia yake ya watoto wanne.
Kwa upande wa baba yake
aliyejitambulisha kwa jina la Bw Wiliamu Joseph (30) alisema kuwa mwanae alizaliwa
akiwa na uvimbe kichwani na baada ya kuzaliwa hivyo walimpeleka kwenye
hospitali iyopo Kijijini hapo ambapo walishindwa na kumpeleka hospitali Teule
ya Tumbi lakini hata hivyo nao walishindwa.
Amesema ilibidi wammpeleke Jijini
Dar es Salaam Msasani kwenye hospitali ya CCBRT ambapo alifanyiwa operesheni
kutoa uvimbe huo mara mbili miaka miwli mfululizo lakini kwa mwaka jana mwezi
wanne mama yake alifariki hivyo alishindwa kumpeleka
Amesema kwa mwaka huu anatarajia
kumpeleka tena ambapo kwa gharama ya watoto ni bure ila gharama za yeye
kumhudumia wakati wa matibabu ni kiasi cha kama
sh 70,000 ambazo inambidi kuzitafuta ndipo akatibiwe.
Amesema kuwa tatizo ni uwezo wake
kuwa ni mdogo kwa ajili ya matumizi hayo na kuacha nyumbani kwa familia yake na
inambidi achome mkaa na kilimo ili kuweza kulisha familia yake.
Amewaomba watu mbalimbali kujitokeza
kumsaidia ili kumpeleka mtoto huyo akapatiwe matibabu aweze kurudia katika hali
yake ya kawaida kwani kwa uvimbe wa mwanzo uliotolewa hali imekuwa nzuri.
Katibu
wa chama hicho cha albino mkoa wa Pwani Bi Aichi Ngure alisema kuwa
watoto wenye ulemavu wamekuwa wakikosa matibababu kutokana na jamii kuwa
na mtizamo mbaya juu ya watoto hao hivyo kuwaficha.
Bi
Ngure alisema kuwa serikali na wadau wengine wanapaswa kutupia macho
vijijini ili kuangalia changamoto zinazowakabili watoto zikiwemo za
afya, elimu na maji
Kwa upande wake mwenyekiti wa chama
cha albino mkoani Pwani Bw Thomas Diwani amesema kuwa watoto wenye ulemavu
vijijini ni wengi sana
na wamekuwa wakikosa huduma za afya na elimu.
Bw Diwani amesema kuwa jamii
inapaswa kuzisiadia familia zenye watoto wenye ulemavu ili wapate matibabu na
elimu ambavyo ni vitu vya msingi katika maisha ya kawaida ya kila siku.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment