Wednesday, April 26, 2023

MILIONI 2.9 HUPOTEZA MAISHA



TAKWIMU za kidunia zilizotolewa na Shirika la Kazi Duniani mwaka 2022 zinaonesha kwamba zaidi ya watu milioni 2.9 hupoteza maisha kutokana na ajali na magonjwa yatokanayo na kazi.

Aidha zaidi ya wafanyakazi milioni 402 huumia wakiwa kazini na hivyo kushindwa kutekeleza majukumu yao kwa kipindi chote wanachopatiwa matibabu hadi hapo watakapopona.

Akizungumza  na Waandishi wa habari Tarehe 26 April 2023 Jijini Dodoma kuelekea maadhimisho ya siku kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya kimataifa ya usalama na afya mahali pa kazi Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi,Vijana,Ajira, na Wenye Ulemavu Prof Joyce Ndalichako amesema Kwa upande wa Tanzania jumla ya ajali na magonjwa yaliyoripotiwa katika Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi kuanzia Julai 2019 hadi Juni 2021 ni ajali 4,993 na magonjwa 249. Katika ajali hizo vifo vilikuwa 217.

Prof Ndalichako amesema kuwa maadhimisho hayo yatafanyika kitaifa Mkoani Morogoro katika viwanja vya Tumbaku Aprili 28,2023 na lengo kubwa la maadhimisho hayo ni kuendeleza kampeni za kuhamasisha na kuweka mazingira salama katika sehemu za kazi miongoni mwa wadau kupitia kauli mbiu mbali mbali ambazo hutolewa na Shirika la Kazi Duniani ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni: “Mazingira Salama na Afya kazini ni Kanuni na Haki ya Msingi Mahali pa Kazi” (A Safe and Health Working Environment is a Fundamental Principle and Right at Work).

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda amesema kuwa moja kati ya eneo ambalo ajali nyingi zinaripotiwa ni katika sekta ya Uzalishaji ambapo imeajiri vijana wengi huku wengine wakiwa hawana ujuzi wa kutosha katika nafasi wanazofanyia kazi.

Mwenda amesema kuwa OSHA imejipanga vyema kuelekea maadhimisho hayo ya 19 ambapo washiriki wote watapatiwa Mafunzo ya Usalama na Afya miongoni mwa makundi mbali mbali wakiwemo wajasiriamali wadogo, wafanyakazi wa viwandani, wachimbaji wadogo pamoja na watu wenye ulemavu.

Siku ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi Duniani ilianza mwaka1996 Nchini Marekekani Katika Jiji la New York, ambapo waathirika wa watu walioumia na kupoteza maisha wakiwa kazini hukumbukwa. Maadhimisho hayo yalikuwa yakifanywa na Chama Cha Wafanyakazi Duniani. Ilipofika mwaka 2001,Shirika la Kazi Duniani liliona kuwa ni busara kubadilisha madhumuni ya siku hiyo na kuiita “Siku ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi Duniani


Mwisho.

KUNENGE AZINDUA DARAJA LA MIPEKO

MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge leo Aprili 26, 2023 amezindua Daraja la Mipeko iliyopo Barabara ya Mwanambaya lenye thamani ya shilinigi milion 214.

Kunenge akisalimia wananchi wa Mipeko  amepongeza Dkt Samia Suluhu Hassan  kwa kuleta Maendeleo ambayo yanamgusa mwanachi wa kawaida.

Ameeleza kuwa Rais alipofanya ziara Mkoani Pwani alisema nia yake ya kuhakisha Mkoa unapata Miundombinu ya yote muhimu ya Afya, Elimu, Maji, Nishati, Barabara.

Aidha amesema kuwa mkoa huo una Mtandao wa Barabara wa km 6629 zinazohudumiwa na TANROADS na TARURA. 

Ameongeza kuwa bajeti ya kutekeleza  shughuli za Barabara kwa mwaka 2021/22 ilikuwa ni bilion75.5 na kwa mwaka 2022/23 imeongezwa kufikia bilion 81.

Amewataka Wananchi wa eneo hilo kulinda Daraja hilo na kutoa maelekezo kwa Mkurugenzi wa  Halmshauri ya Mkuranga kupanga Mji wa Mkuranga kwa kuwa Mji huo unakuwa kwa kasi.

Kunenge ameeleza Serikali inafanyia kazi maombi ya Wananchi hao ya kujengewa Kituo cha Afya, kupelekewa Umeme na ujenzi wa Daraja.

Wednesday, April 19, 2023

WAZIRI JAFO AUPONGEZA MKOA WA PWANI KWA KAMPENI YA UPANDAJI MITI



WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Suleiman Jafo ameupongeza Mkoa wa Pwani kwa kuweka kampeni ya upandaji miti ili kukabiliana na uharibifu wa mazingira.

Jafo aliyasema hayo kwenye shule ya sekondari Ruvu Mlandizi Wilayani Kibaha wakati akizundua Kampeni ya utunzaji mazingira na matumizi ya nishati mbadala kwa mkoa huo iliyoandaliwa na benki ya NMB Wakala wa Misitu Tanzania TFS Mkoa wa Pwani, ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani na Taifa Gesi.

Alisema kuwa kwa kampeni hiyo kwani itasaidia kutunza mazingira pia utasaidia kutangaza teknolojia mbadala ya matumizi ya nishati mbadala baada ya kupunguza matumizi ya miti kama nishati kwa ajili ya kupikia na matumizi mengine ya binadamu ya kila siku.

Aidha alisema kuwa mkoa wa Pwani ni moja ya mikoa minne ambayo imeathirika kwa kiasi kikubwa na uharibifu wa mazingira lakini baada ya kupata maelekezo kutoka kwa Rais Dk Samia Suluhu Hassan ya kutaka mikoa hiyo iweke mipango ya kukabili hali hiyo mkoa umejiongeza kwa kuwa na kampeni hizo za kukabili changamoto za mazingira.

Awali akimkaribisha Waziri Jafo akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Pwani  Abubakar Kunenge Mkuu wa wilaya ya Kibaha Nickson John alisema kuwa mkoa umeweka mikakati mbalimbali ili kutunza mazingira ikiwa ni pamoja na kupanda miti million 13.5 lakini hadi sasa wameshapanda miti milioni 9.7 ikiwa ni zaidi ya asilimia 70 ya malengo ili kurejesha uoto wa asili.

Naye Mkurugenzi wa kampuni ya Taifa gesi Anjela Bhoke alisema kuwa kila mwaka hekari 400,000 za miti zinapotea kutokana na matumizi mbalimbali ya miti ambapo moja ya mikakati yao ni kujenga kiwanda cha kutengeneza mitungi ya gesi ambapo wako tayari kusambaza gesi majumbani na kwenye taasisi za umma.

Mwakilishi wa benki ya NMB Seka Urio alisema kuwa wametenga kiasi cha shilingi milioni 470 kwa ajili ya shule zitakazopanda miti 2,000 na kuitunza kwa asilimia 80 ambapo itapatiwa milioni 50, huku mshindi wa pilia kwa kupanda miti 1,500 akipata milioni 30 akiitunza kwa asilimia 70 na watatu akipata milioni 20 kwa kupanda miti 1,000 itakayokuwa imetunzwa kwa asilimia 70.


Tuesday, April 18, 2023

TANZANIA KUBORESHA MAWASILIANO

 


SERIKALI ya awamu ya sita inayoongozwa na Dkt Samia Suluhu Hassan imedhamiria kuhakikisha Tanzania inakuwa na miundombinu bora ya mawasiliano yenye kutumia Teknolojia ya kisasa ambayo italeta tija na ufanisi katika kuongeza uzalishaji na ujenzi wa uchumi na kuimarisha usalama na ulinzi wa Taifa.

Hayo yamesemwa Waziri wa Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nape Moses Nnauye katika hafla ya utiaji saini kati ya TTCL na HUAWEI kuhusu upanuzi wa mkongo wa Taifa wa mawasiliano katika Wilaya 23  uliyofanyika Jijini Dodoma.

Nape amesema zaidi ya  shilingi  bilion 37 zitangharimu ujenzi wa kilometa 1,520 ambazo zitaunganisha Wilaya 23 katika upanuzi wa mkongo wa Taifa wa mawasiliano kati ya shirika la mawasiliano Tanzania na kampuni ya HUAWEI International.

Amesema kuwa mradi huu unaenda kuleta mageuzi makubwa yakiwemo kukuza matumizi ya tehama Wilaya kuongeza kasi ya ukusanyaji mapato pamoja na kuleta fursa kwa wananchi kiuchumi.



Awali kwa upande wake Mkurugezi mkuu wa TCCL  mhandisi Peter Ulanga 

Amesema mradi huu utatoa fursa nzuri kwa wizara , Taasisi za umma na Taasisi binafsi kufikisha huduma Zao kwa wateja na watumiaji wao kwa haraka na wakati kwa kuwa mkongo wa Taifa utakuwa na uwezo mkubwa wa kubeba taarifa za kutuma kwa haraka.

Monday, April 17, 2023

RIDHIWANI AGAWA ZAWADI UHIFADHI QURAAN

Nimeshiriki kugawa zawadi katika mashindano ya Kimataifa ya uhifadhi wa Quraan yaliayofanyika Ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam. Namshukuru Mwenyezi Mungu kwa fursa hii.

Saturday, April 15, 2023

RIDHIWANI KIKWETE AWASHUKURU WANACHALINZE KWENYE FUTARI


Nimeshiriki futari na Wananchi wenzangu wa Halmashauri ya Chalinze pamoja na viongozi wa Chama na Serikali wa wilaya yetu. Nawashukuru sana Wananchi wenzangu kwa muitikio wenu. Asanteni sana. #RamadhanKareem #Chalinze.

Wednesday, April 12, 2023

BAJETI OFISI YA WAZIRI MKUU


Nimeshiriki kikao cha Bunge kinachojadili Bajeti ya ofisi ya Waziri Mkuu 2023/24. #KaziInaendelea #Bajeti2023