Saturday, April 15, 2023
Wednesday, April 12, 2023
BAJETI OFISI YA WAZIRI MKUU
Nimeshiriki kikao cha Bunge kinachojadili Bajeti ya ofisi ya Waziri Mkuu 2023/24. #KaziInaendelea #Bajeti2023
Friday, April 7, 2023
SERIKALI YABORESHA HUDUMA ZA MAJI.
Na Wellu Mtaki, Dodoma
SERIKALI ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dk Samia Suluhu Hassan imefanya jitihada kubwa katika kufanya mabadiliko na maboresho makubwa katika Sekta ya Maji ikiwa pamoja na kuongeza uwekezaji katika sekta hiyo ili kukabiliana na changamoto zilizoko.
Hayo yamesemwa na mkuu wa mkoa wa Dodoma Rosemary Sinyamule wakati wa ufunguzi wa tafiti juu ya maombi ya kurekebisha bei za huduma ya maji safi iliyoletwa na mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira Dodoma ( DUWASA)
Sinyamule amesema kuwa lengo kubwa la Serikali katika kufanya mabadiliko na kuongeza uwekezaji katika sekta ya Maji ni kuongeza ubora na upatikanaji wa huduma ili kuboresha maisha ya Wananchi wake na hatimaye kufikia lengo la asilimia 95 (kwa mijini) lililowekwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ifikapo mwaka 2025.
Awali mwakilishi wa Mkurugezi mkuu wa Ewura George Kabelwa katika maombi hayo Mamlaka ya Maji Dodoma imeomba kufanya marekebisho ya bei zitakazotumika kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia mwaka 2023/24 hadi 2025/26 kwa mujibu wa maombi yaliyowasilishwa EWURA, Mamlaka ya Maji Dodoma imebainisha kuwa marekebisho ya bei ya maji yanalenga kupata fedha za kutosha kukidhi gharama halisi za uendeshaji na matengenezo kwa lengo la kuboresha huduma zitolewazo.
Aidha Mamlaka ya Maji Dodoma imeeleza kuwa bei zinazopendekezwa zitaiwezesha mamlaka kumudu gharama zote za utoaji huduma pamoja na mambo mengine, kuendelea kuongeza ubora wa maji, kuiwezesha mamlaka kuwa endelevu na kukidhi matarajio ya wana Dodoma.
Kwa upande wa wakilishi wa wananchi Revina Petro Lamiula ametoa maoni kwa kusema kuwa pamoja na bei kupandishwa ila wanaitaka mamlaka ya maji safi (Duwasa) kuhakikisha wanaboresha huduma zao.
Wednesday, April 5, 2023
WATAKIWA KUTUMIA VANILLA MARA KWA MARA
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
MKURUGENZI Mkuu wa Vanilla International Limited Simon Mnkondya ameitaka jamii kutumia zao la Vanilla katika matumizi ya kila siku kwani zao hilo huchochea kuwa na akili zaidi.
Mnkondya amebainisha hayo Jijini Dodoma kwenye kikao Cha wadau wa zao la Vanilla.
Amebainisha kuwa ili kuweza kuwa na akili nyingi,hata wanasayansi Duniani wamekuwa wakitumia malighafi inayopatika katika zao la Vanilla hali inayopelekea kuwa wabunifu na kubuni vitu mbalimbali.
Aidha Mnkondya amebainisha kuwa vyama vya ushirika vimekuwa vikiwaibia wakulima bila kuwatengenezea masoko ya uhakika na badala yake vimekuwa vikitengeneza wezi.
Pia amebainisha kuwa kilimo Cha Vanilla soko lake linapatikana Kwa wingi katika nchi za uarabuni na Vanilla inayonuniliwa sana ni Vanilla ya gradi la kwanza.
Katika kuuza zao la Vanilla Kwa Duniani ya sasa Mnkondya amebainisha kuwa haina haja ya kubeba mzigo kupeleka katika nchi unaweza kuuza kupitia mtandao Kwa kuandika vigezo vya zao lako la Vanilla na wateja wakakufata wenyewe.
Ameongeza kuwa zao la Vanilla halitakiwi kulimwa kiholela na badala yake amewashauri wakulima kulima,kulima Kwa pamoja kilimo Cha Block Farming.
WATAKIWA KUPINGA UKATILI
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
MKUU wa Mkoa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amewaasa wananchi wa Kata ya Chang'ombe kukubali kubadilika kupinga Ukatili kwa kushirikiana pamoja ili Mkoa wa Dodoma kuwa wa Mfano kwa maendeleo ya Taifa.
Ameyasema hayo aliposhiriki katika Kongamano la Kupinga Ukatili Mkoa wa Dodoma lililoandaliwa na kamati ya kutokomeza Ukatili wa Kijinsia na Msaada wa Kisheria, kupitia kikundi cha Wanawake na Samia na kusikiliza kero za wananchi wake katika Mtaa wa Mazengo Chang'ombe.
Senyamule amesema kuwa Chang'ombe bila vitendo vya kikatili inawezekana na kutoa rai kwa wazazi na walezi wa Kata ya Chang'ombe kutoficha vitendo viovu vya watoto na vijana katika jamii inayowazunguka ili jitihada za pamoja za kutokomeza vitendo vya kikatili ziweze kufanikiwa.
Aidha, Mhe. Senyamule ameendelea kumshukuru Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuimarisha Mkoa wa Dodoma kwa miradi mikubwa ya kimkati ambayo ni fursa kwa vijana ambayo ni fursa kwao kujishughulisha na shughuli za uzalishaji mali kwani wana sehemu ya kupeka nguvu kazi zao ili kujiepusha na tabia zisizo na Maadili.
"Mimi kama Mkuu wa Mkoa wa Dodoma ningetamani kila Kata, Mtaa, Kaya na kila nyumbani isiwe na mhalifu wala mtu yeyote anaefanya ukatii na unyanyasaji wa kijinsia, lakini itawezekana kama sisi wananchi tutaamua kuungana na juhudi na dhamira nzurii za Serikali
"Vijana mjipange kubadilika sisi kama Mkoa tunadhamira njema na kizazi cha nchi hii, ni wakati sahihi wakujiwekea sheria ambazo tutasimamia wenyewe zinazohusu Ukatili wa Kijinsia kwani inawezekana kubadilika kusiwe na vijana vibaka, wezi ili kupongeza wale wenye Maadili mazuri na kuwa mfano wa kuigwa "Amesema Senyamule.
Naye Mwanakamati ya kupinga Ukatili Fatuma Madidi ametoa elimu juu ya Ukatili wa nafsi, watoto, vijana, wazee na Wanawake ili kuweza kutambua Madhara ya Ukatili kwa Ujumla na kuendelea kujihadhalisha .
Kwa Upande wake Diwani wa Chang'ombe Bw. Bakari Fundikira amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa ujio wake katika kata yake na kuahidi kuendelea kutekeleza maelekezo yake.
Friday, March 31, 2023
MAHAKIMU NA MAJAJI WAPATIWA MAFUNZO
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
MAHAKIMU na Majaji wamepatiwa mafunzo ya siku mbili kuhusu wajibu wa Mahakama katika kutunza na kulinda uhuru wa kujieleza pamoja na haki za binadamu nchini.
Mafunzo hayo ya siku mbili yanatolewa na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) likiwa Ni kukumbushana masuala mbalimbali katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.
Mratibu wa Mtadao wa THRDC, Onesmo Olengurumwa akizungumza na waandishi wa habari jijini dodoma wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo kwa Mahakimu na Majaji nchini amesema lengo ni kukumbushana wajibu katika kutekeleza majukumu ya kila siku.
Aidha amesema kuwa umekuwepo na mabadiliko mengi ya kisheria na masuala mbalimbali yanayohusu haki za binadamu hivyo wao kama watu ambao wanatoa haki kila siku katika Mahakama, wanapaswa kuyafahamu ili kulinda haki za binadamu na uhuru wa kujieleza
Amesema pia mafunzo mengine ambayo yatatolewa ni masuala ya maadili kwa Mahakimu na Majaji katika utekelezaji wa majukumu ya utoaji wa haki katika maeneo yao.
Amesema Suala la maadili ni jambo la muhimu sana katika mahakama zetu nchini hivyo mafunzo haya pia yatasaidia kuwakumbusha Mahakimu na Majaji wajibu wao wa kutenda haki kwa kuzingatia maadili ya kazi zao.
Naye Naibu katibu mkuu wa Chama cha Mahakimu na Majaji Tanzania (JMAT) Mary Kallomo, amesema mafunzo hayo yatawasaidia kuboresha utendaji wao wa kila siku katika kulinda haki za binadamu na uhuru wa kujieleza.
NAIBU WAZIRI KIKWETE ATEMBELEA WANANCHI WA MKANGE
Kuzungumza na Wananchi na kueleza hatua mbalimbali zilizofikiwa na serikali yetu katika kutatua changamoto zinazotokana na shughuli za maendeleo ikiwemo miradi mbalimbali inayotekelezwa katika Halmashauri yetu.
Nimetumia nafasi hiyo kuwakumbusha mabadiliko mbalimbali yanayofanyika katika sekta mbalimbali ikiwemo ya Afya, Elimu, Huduma za Jamii, Miundombinu, Maji, Utumishi wa Umma n.k. Ahadi yetu ni kuendelea kuwatumikia na kutatua changamoto zetu.#TukoPamoja #Chalinze #KaziInaendelea