Na Mwandishi Wetu, Dodoma
MKURUGENZI Mkuu wa Vanilla International Limited Simon Mnkondya ameitaka jamii kutumia zao la Vanilla katika matumizi ya kila siku kwani zao hilo huchochea kuwa na akili zaidi.
Mnkondya amebainisha hayo Jijini Dodoma kwenye kikao Cha wadau wa zao la Vanilla.
Amebainisha kuwa ili kuweza kuwa na akili nyingi,hata wanasayansi Duniani wamekuwa wakitumia malighafi inayopatika katika zao la Vanilla hali inayopelekea kuwa wabunifu na kubuni vitu mbalimbali.
Aidha Mnkondya amebainisha kuwa vyama vya ushirika vimekuwa vikiwaibia wakulima bila kuwatengenezea masoko ya uhakika na badala yake vimekuwa vikitengeneza wezi.
Pia amebainisha kuwa kilimo Cha Vanilla soko lake linapatikana Kwa wingi katika nchi za uarabuni na Vanilla inayonuniliwa sana ni Vanilla ya gradi la kwanza.
Katika kuuza zao la Vanilla Kwa Duniani ya sasa Mnkondya amebainisha kuwa haina haja ya kubeba mzigo kupeleka katika nchi unaweza kuuza kupitia mtandao Kwa kuandika vigezo vya zao lako la Vanilla na wateja wakakufata wenyewe.
Ameongeza kuwa zao la Vanilla halitakiwi kulimwa kiholela na badala yake amewashauri wakulima kulima,kulima Kwa pamoja kilimo Cha Block Farming.
No comments:
Post a Comment