SERIKALI kupitia wizara ya mifugo imeweza kuongeza vifaa vya malisho ya mifugo pamoja na Ngo'mbe 1,000 katika Ranchi ya Kongwa iliyopo Dodoma huku ikiwa na malengo ya kuhakikisha inatoa huduma Bora kwa wananchi Katika sekta ya ajira na uhuzaji wa majani ya malisho ya mifugo.
Hayo yamesemwa Tarehe 27 April 2023 na waziri wa mifugo na uvuvi Abdalah Ulega wakati wa uzinduzi wa vifaa vya malisho ya mifugo na ukaguzi wa Ngo'mbe 1,000 Katika eneo ilo la Narco.
Ulega amesema serikali imefanikiwa kununua Ngo'mbe hao pamoja vifaa hivyo vya malisho ikiwemo matreta manne, mower 3, Hay rake 10 pamoja na bailer 3 Ili kuboresha maeneo ya Malisho.
Amesema mpaka Sasa nyama zinazouzwa kwenye Ranchi hiyo ni tani 12,000 na kwa muelekeo unaoelekea wataenda kuuza nyama hadi tani 50 mpaka tani 1,000.
Aidha amemtaka Mkurugezi wa Nacro kupendezesha eneo ilo kwa kuweka mipaka minzuri ya eneo Ili kunusuru mifugo isitoke ndani eneo ilo na kuhakikisha wafugaji ambao wamepewa kitalu kwenye eneo hilo wafuge kisasa na kutafutiwa masoko.
Awali Mkurugezi mtendaji wa Ranchi ya taifa ( Nacro) Prof Peter Msoffe amesema kuwa kwa mwaka wa fedha 2022/2023 serikali ilitenga fedha kiasi cha shillingi bilioni 4.65 kwa ajili ya kuboresha na kuongeza uzalishaji katika Ranchi za Kongwa na Mzeri fedha hizo zilitengwa kwa ajili ya kununulia ng'ombe wazazi, vifaa vya shamba na uchungaji wa visima virefu.
Ikumbukwe kuwa Ranchi ya Kongwa ni miongoni mwa Ranchi kongwe za taifa iliyopo mkoani Dodoma wilaya ya Kongwa na ndiyo ya kwanza kuanzishwa na ilianza Mwaka 1948 na eneo hilo lina ukubwa wa hekta 3,8000 zenye uwezo wa kuweka uniti za mifugo 25,000.
No comments:
Post a Comment