Saturday, April 29, 2023

MAPATO YA UTALII YAONGEZEKA KUPITIA ROYAL TOUR

MAPATO ya utalii yaongezeka maradufu kutokana na watalii kuongezeka nchini kutoka Dola za Marekani 1.310.34 (Sawa na Shilingi Trilioni 3.01) mwaka 2021 hadi Dola za Marekani,527.77 (sawa la Shilingi Trilioni 5.82)  ukiwa ni   matunda ya filamu  ya The Royal Tour.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt Hassan Abbasi  wakati akielezea mafanikio ya  mwaka mmoja tangu Mhe Dkt  Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, alipozindua  filamu hiyo Jijini Arusha.

Amesema  filamu ya THE  ROYAL TOUR imejenga hamasa kwa watalii na wawekezaji na hamasa hiyo  imekuwa na manufaa katika sekta ya usafiri wa Anga hadi kuongeza Ruti na  Miruko ikiwemo ndege ya  kimataifa KIA imeongezeka  kwa asilimia 28 kutoka miruko 6,115 April 2021 hadi 7,850 April, 2023.

Aidha  amesema kuwa  Novemba mwaka jana huko Dallas,Texas, USA, Taasisi ya Tuzo za Afrimma ilimtangaza Rais Dkt. Samia  Suluhu Hassan kuwa Rais Mwanamke wa kwanza Afrika na Kushinda Tuzo ya Mageuzi Katika Uongozi .

Pia amesema kuwa filamu ya The Royal Tour sio ya  mwisho ni mwanzo wa kuitangaza nchi kimataifa zaidi hivyo Kamati ya mwaka mmoja sasa, imepokea na inaendelea kuchambua The royal Tours nyingine .


No comments:

Post a Comment