Sunday, May 29, 2016

WAIOMBA HALMASHAURI IWALIPE FIDIA BAADA YA KUPEWA SIKU 14 KUVUNJA NYUMBA ZAO

Na John Gagarini, Kibaha
BAADHI ya wakazi kwneye eneo la Sagulasagula maarufu kama Loliondo Mtaa wa Machinjioni kata ya Tangini wilayani Kibaha mkoani Pwani wanaodaiwa kuvamia eneo lililotengwa kwa ajili ya soko wameiomba Halmashauri ya Mji kuwalipa fidia na maeneo ya kuishi baada ya kupewa siku 14 kuhama kwenye eneo hilo.
Wakizungumza mara baada ya kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya kupitia na kuangalia eneo hilo na kutoa maagizo kwa wakazi hao kubomoa nyumba zipatazo 55 zilizojengwa kwenye eneo hilo walisema kuwa kwa kuwa ni mpango wa maendeleo basi nao waangaliwe kwani wamekaa hapo kwa muda mrefu.
Said Tekelo alisema kuwa baadhi ya watu wako hapo tangu mwaka 1970 na mwaka 2003 Rais Benjamin Mkapa wakati ule alifuta hati ya eneo hilo toka eneo la Viwanda na kutaka lirejeshwe kwenye mtaa kwa ajili ya matumizi mengine.
“Baada ya kurejeshwa kwenye mtaa baadhi ya watu walipimiwa maeneo yao baada ya kupigwa picha na kamahaitoshi hata alipokuja waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi alitoa miezi mitatu sasa sita Halmashauri ikae na wakazi hao ili kujadili namna nzuri ya kufanya,” alisema Tekelo.
Alisema kuwa licha ya maagizo hayo walikwenda Mahakamani kwenda kulalamika walipotakiwa kuondoka na kesi iliendeshwa na wao kushindwa na Mahakama ili amuru Halmashauri ikae nao lakini hakuna kilichofanyika hadi mwishoni mwa wiki walipotakiwa kuvunja wenyewe na endapo hawatafanya hivyo Halmashauri itabomoa nyumba hizo.
“Tumeambiwa tubomoe wenywe na kuanzia leo Tanesco na Dawasco wameshapewa maagizo ya kuondoa miundombinu yao ilkiwa ni maandalizi ya kubomoa sisi tunaomba Halmashauri itufikirie kwa kutulipa fidia pamoja na maeneo kwa ajili ya kuishi kwani wenzetu jirani ambao tuko kwenye mgogoro mmoja wamelipwa na kupewa viwanja,” alisema Tekelo.
Kwa upande wake Diwani wa kata ya Tangini Theodori Joseph alisema kuwa suala hilo ni la muda mrefu ambapo baraza la Madiwani miaka ya nyuma waliwatambua wakazi hao kutaka walipwe fidia na walikuwa wakishirikiana nao katika mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuchukua kodi za majengo.
Joseph alisema kuwa kuna haja ya Halmashauri kuwafikiria wakazi hao kwani wengine wako hapo miaka 40 iliyopita na wameendeleza ardhi kwa kipindi chote hicho lakini jirani zao ambao wametengwa na barabara wao  wamepewa fidia na watapewa viwanja.
Ofisa Habari wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha Inocent Byarugaba alisema kuwa eneo hilo lilitengwa kwa ajili ya soko na liko kwenye Ramani ya Mji na  wakazi hao walilivamia eneo hilo na wanapaswa kuliachia.
Byarugaba alisema kuwa tayari eneo hilo liko kwenye maandalizi ya ujenzi wa soko unatarajiwa kuanza wakati wowote kuanzia sasa kwani tayari ramani imeshatoka ambapo soko linalotumika kwa sasa liko kwenye hifadhi ya barabara na litabomolewa muda wowote na Tanroads.
Naye kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri Lucy Kimoi alisema kuwa wakazi hao wanapaswa kuondoka na kwa sasa wanaandaa notisi kwa ajili ya kuwataka waliachie eneo hilo kwani wako hapo kinyume cha Sheria.
Mwisho.

KITUO CH AFYA MKOANI CHAHITAJI JENERETA

Na John Gagarini, Kibaha
KITUO cha Afya cha Mkoani kinakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa Jenereta ili kukabiliana na tatizo la ukatikaji umeme kwenye chumba cha akinamama wanapojifungulia hivyo kuwaomba wadau mbalimbali.
Hayo yalisemwa mjini Kibaha na mganga mkuu wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha Happiness Ndosi wakati akipokea msaada wa vifaa mbalimbali kwa watoto waliozaliwa na watakaozaliwa kutoka shirika lisilokuwa la kiserikali la Abubaker Darwesh International Charitable Foundation (ADICF) la Jijini Dar es Salaam.
Dk Ndosi alisema kuwa kukatika kwa umeme kwenye kituo hicho ni changamoto kubwa hasa nyakati za usiku na wakati mama wajawazito wanapokuwa wanajifungua hali ambayo inahatarisha maisha ya akinamama hao.
“Kutokana na hali hiyo tunawaomba wadau mbalimbali wajitokeze kutusaidia kupata jenereta kwa ajili ya kusaidia mara umeme unapokatika katika chumba cha uzalishaji mama wajawazito ili kunusuru maisha yao,” alisema Dk Ndosi.
Aidha alisema mbali ya changamoto hiyo pia wanakabiliwa na changamoto nyingine ikiwa ni pamoja na ukosefu wa chumba cha upasuaji, Ultra Sound na X-Ray, gari la wagonjwa kwani lililopo ni chakavu, magodoro na vitanda hasa ikizingatiwa kuwa kituo hicho kiko mbioni kuwa Hospitali ya Wilaya.
Kwa upande wake mwanzilishi na meneja mradi wa shirika hilo Bilal Abubekar alisema kuwa shirika lake limeamua kutoa misaada hiyo kwa lengo la kuisaidia jamii hasa kwa watoto wadogo wenye umri chini ya miaka mitano ili kuisaidia serikali kuhakikisha watoto chini ya miaka mitano wanapata huduma bora.
Abubaker alisema kuwa shirika lao limekuwa likisaidia makundi mbalimbali ikiwa ni pamoja na wajane yatima na watu wenye mahitaji, pia kusaidia elimu watu wenye ulemavu.
Naye moja ya wagonjwa waliopata msaada huo Mariamu Ally alishukuru shirika hilo na kusema kuwa wameonyesha moyo wa upendo na kuwataka waendelee kusaidia hospitali hiyo ili iweze kukabiliana na changamoto zilizopo kwa wagonjwa.
Alisema kuwa moja ya changamoto iliyopo kwenye wodi hiyo ni kuchanganywa kati ya akinamama waliojifungua na wale wanaosubiri kujifungua na kutaka watu hao kutenganishwa ili kila moja wawe na sehemu yao.
Mwisho.   


Thursday, May 26, 2016

MWENYEKITI AKATALIWA KWENYE MKUTANO

Na John Gagarini, Kibaha
SAKATA la Mwenyekiti wa Mtaa wa Muheza wilayani Kibaha mkoani Pwani Maulid Kipilili limechukua sura mpya baada ya wananchi wa mtaa huo kumkataa mwenyekiti huyo kwenye mkutano wa wananchi uliofanyika mtaani hapo.
Wananchi hao walimkataa mwenyekiti wao wakati wa mkutano ulioitishwa na diwani wa kata ya Maili Moja Ramadhan Lutambi ili kujadilia suala la malalamiko ya wananchi wa mtaa huo baada ya kuifunga ofisi ya mtaa hadi pale watakapofikia muafaka juu ya mwenyekiti wao.
Mkutano huo ambao ulifanyika mtaani hapo chini ya diwani huyo wa kata na ofisa Mtendaji wa Kata hiyo Thadeo Mtae wananchi hao walilalamika kuwa mwenyekiti wao tangu achaguliwe kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika mwishoni mwa mwaka 2015 hajaitisha mkutano wa wananchi.
Kabla ya kufikia hatua ya kumkataa mwenyekiti wao wananchi hao walitoa malalamiko yao mbalimbali ikiwa ni pamoja na kulalamika kuwa mwenyekiti wao haitishi vikao vya wananchi, hasomi mapato na matumizi, kutofungua ofisi hivyo kuwapa shida wananchi wanapokwenda kupata huduma za kiofisi.
Akizungumza juu ya mwenyekiti wao kushindwa kuwajibika mwananchi wa mtaa huo Kitai Mganga alisema kuwa ni pamoja na tuhuma nyingine ni kushindwa kusimamia mali za mtaa ikiwa ni pamoja na baadhi ya watu kumega na kuuziana eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa shule ya Msingi lakini hakuna hatua zozote ambazo amezichukuwa.
“Mtaa wetu una changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na ukosefu wa maji, umeme, Shule ya Msingi, bararabara na zahanati lakini kutokana na mwenyekiti wetu kutowajibika tumeshindwa kufanya lolote hata kuweka mikakati ya maenedeleo hakuna,” alisema Mganga.
Naye Paulo Chacha alisema kuwa mwenyekiti lazima awe na wajumbe wa mtaa lakini cha kushangaza wajumbe hawapo hivyo mwenyekiti anafanya kazi peke yake jambo ambalo haliwezi kuleta mafanikio.
Chacha alisema kuwa kamati ya mtaa ni sawa na baraza la mawaziri sasa haiwezekani Rais kuongoza nchi bila ya kuwa na Mawaziri kwani maendeleo hayawezi kupatikana.
Kwa upande wake Maulid Kipilili alisema kuwa kwa upande wa mikutano alishindwa kufanya kutokana na sababu maalumu ikiwa ni pamoja na shughuli za kitaifa.
Kipilili alisema kuwa aliitisha mikutano mitatu ya dharura na miwili ya kikatiba na kuwashangaa wananchi hao kumsingizia kuwa hajafanya kabisa mikutano na mmoja wa Mei 15 ulishindwa kufanyika kutokana na akidi kushindwa kuenea.
“Kuhusu wajumbe wa serikali ya mtaa hawajafika kwa sababu mbalimbali lakini wapo na sina mgogoro na wajumbe wangu na tunafanya kazi vizuri na baadhi ya kamati zipo na zinafanya kazi kama ya maji na shule zipo na aliyeuziwa eneo la shule kama kuna mtu anaushahidi alete ili tuchukue hatua za kisheria,” alisema Kipilili.
Akielezea juu ya changamoto hiyo ya wananchi kumkataa mwenyekiti wao diwani wa kata hiyo Ramadhan Lutambi alisema kuwa kama hawamtaki wanapaswa kufuata taratibu kwani hatua ya kwanza ni hiyo.
Lutambi alisema kuwa kutokana na hali hiyo itabidi uitishwe mkutano wa dharura wa kata kujadili suala hilo na wao ndiyo watakaoamua hatma ya mweneyekiti wao.
Kufuatia kukataliwa na wananchi ofisa mtendaji wa kata ya Maili Moja Thadeo Mtae alisema kuwa hoja zilizotolewa ni 15 ambapo zimejibiwa na mwenyekiti huyo ambapo baadhi wamekataa majibu yake na nyingine wamekubali majibu.
Mtae alisema kuwa atapeleka sehemu husika kwa ajili ya majibu na hatua zaidi kwani yeye hatoweza kutoa majibu hivyo wasubiri majibu ambapo kutaitishwa mkutano mwingine.   

Mwisho.   

MWENYEKITI AKATALIWA KWENYE MKUTANO

Na John Gagarini, Kibaha
SAKATA la Mwenyekiti wa Mtaa wa Muheza wilayani Kibaha mkoani Pwani Maulid Kipilili limechukua sura mpya baada ya wananchi wa mtaa huo kumkataa mwenyekiti huyo kwenye mkutano wa wananchi uliofanyika mtaani hapo.
Wananchi hao walimkataa mwenyekiti wao wakati wa mkutano ulioitishwa na diwani wa kata ya Maili Moja Ramadhan Lutambi ili kujadilia suala la malalamiko ya wananchi wa mtaa huo baada ya kuifunga ofisi ya mtaa hadi pale watakapofikia muafaka juu ya mwenyekiti wao.
Mkutano huo ambao ulifanyika mtaani hapo chini ya diwani huyo wa kata na ofisa Mtendaji wa Kata hiyo Thadeo Mtae wananchi hao walilalamika kuwa mwenyekiti wao tangu achaguliwe kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika mwishoni mwa mwaka 2015 hajaitisha mkutano wa wananchi.
Kabla ya kufikia hatua ya kumkataa mwenyekiti wao wananchi hao walitoa malalamiko yao mbalimbali ikiwa ni pamoja na kulalamika kuwa mwenyekiti wao haitishi vikao vya wananchi, hasomi mapato na matumizi, kutofungua ofisi hivyo kuwapa shida wananchi wanapokwenda kupata huduma za kiofisi.
Akizungumza juu ya mwenyekiti wao kushindwa kuwajibika mwananchi wa mtaa huo Kitai Mganga alisema kuwa ni pamoja na tuhuma nyingine ni kushindwa kusimamia mali za mtaa ikiwa ni pamoja na baadhi ya watu kumega na kuuziana eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa shule ya Msingi lakini hakuna hatua zozote ambazo amezichukuwa.
“Mtaa wetu una changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na ukosefu wa maji, umeme, Shule ya Msingi, bararabara na zahanati lakini kutokana na mwenyekiti wetu kutowajibika tumeshindwa kufanya lolote hata kuweka mikakati ya maenedeleo hakuna,” alisema Mganga.
Naye Paulo Chacha alisema kuwa mwenyekiti lazima awe na wajumbe wa mtaa lakini cha kushangaza wajumbe hawapo hivyo mwenyekiti anafanya kazi peke yake jambo ambalo haliwezi kuleta mafanikio.
Chacha alisema kuwa kamati ya mtaa ni sawa na baraza la mawaziri sasa haiwezekani Rais kuongoza nchi bila ya kuwa na Mawaziri kwani maendeleo hayawezi kupatikana.
Kwa upande wake Maulid Kipilili alisema kuwa kwa upande wa mikutano alishindwa kufanya kutokana na sababu maalumu ikiwa ni pamoja na shughuli za kitaifa.
Kipilili alisema kuwa aliitisha mikutano mitatu ya dharura na miwili ya kikatiba na kuwashangaa wananchi hao kumsingizia kuwa hajafanya kabisa mikutano na mmoja wa Mei 15 ulishindwa kufanyika kutokana na akidi kushindwa kuenea.
“Kuhusu wajumbe wa serikali ya mtaa hawajafika kwa sababu mbalimbali lakini wapo na sina mgogoro na wajumbe wangu na tunafanya kazi vizuri na baadhi ya kamati zipo na zinafanya kazi kama ya maji na shule zipo na aliyeuziwa eneo la shule kama kuna mtu anaushahidi alete ili tuchukue hatua za kisheria,” alisema Kipilili.
Akielezea juu ya changamoto hiyo ya wananchi kumkataa mwenyekiti wao diwani wa kata hiyo Ramadhan Lutambi alisema kuwa kama hawamtaki wanapaswa kufuata taratibu kwani hatua ya kwanza ni hiyo.
Lutambi alisema kuwa kutokana na hali hiyo itabidi uitishwe mkutano wa dharura wa kata kujadili suala hilo na wao ndiyo watakaoamua hatma ya mweneyekiti wao.
Kufuatia kukataliwa na wananchi ofisa mtendaji wa kata ya Maili Moja Thadeo Mtae alisema kuwa hoja zilizotolewa ni 15 ambapo zimejibiwa na mwenyekiti huyo ambapo baadhi wamekataa majibu yake na nyingine wamekubali majibu.
Mtae alisema kuwa atapeleka sehemu husika kwa ajili ya majibu na hatua zaidi kwani yeye hatoweza kutoa majibu hivyo wasubiri majibu ambapo kutaitishwa mkutano mwingine.   

Mwisho.   

Monday, May 23, 2016

KIBAHA YAKAMATA KILOGRAMU 441 ZA DAWA ZA KULEVYA

Na John Gagarini, Kibaha

WILAYA ya Kibaha mkoani Pwani imefanikiwa kukamata madawa ya kulevya yenye uzito wa kilogramu 441.6 katika kipindi cha mwaka 2015 / 2016.

Hayo yamesemwa na mkuu wa wilaya ya Kibaha ambaye pia ni wenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya amesema kuwa katika mapambano dhidi ya madawa ya kulevya kipindi cha mwaka 2015/ 2016 wamefanikiwa kukamata dawa zenye uzito wa kilogramu 441.65.

Kihemba amesema kuwa kati ya hizo Cocain na Heroin ni kilo 6.1, Bhangi kilo 418,mirungi kilo 17.5 ambapo jumla ya kesi 153 zimefunguliwa kwenye kituo cha Polisi cha wilaya ya Kibaha.

Amesema kuwa kesi zilizopelekwa mahakamani ni 132 na zilizo kwenye upelelezi ni 21 ambapo kesi za Bhangi na Mirungi zilizo kwisha mahakamani ni 57. 

aidha amesema kuwa jumla ya watuhumiwa ambao walikamatwa na bangi na mirungi ni 163 wanawake wakiwa ni 28 na wanaume ni 135 na wilaya inaendelea kutoa elimu ili watu waepukane na dawa za kulevya.


Mwisho.       

MABILIONI YATENGWA SEKTA YA ELIMU KIBAHA

Na John Gagarini, Kibaha
KATIKA kukabiliana na changamoto za elimu  wilaya ya  Kibaha mkoani Pwani imetenga bajeti ya shilingi bilioni 1,789,828,891 kwa ajili ya miradi ya maendeleo kwa shule za sekondari kwa mwaka wa fedha wa 2016/2017.
Hayo yamesemwa na mkuu wa wilaya ya Kibaha Halima Kihemba na kusema kuwa fedha hizo ni kwa ajili ya kupunguza changamoto mbalimbali kwenye shule za sekondari wilayani humo.
Kihemba amesema kuwa kabla ya bajeti hiyo kupitishwa jumlaya shilingi milioni 640,424,679 zimetumika kwa ajili ya ujenzi wa bweni katika shule za sekondari za Zogowale na Hosteli ya shule ya sekondari ya Pangani.
Amesema kuwa pia fedha hizo zimetumika katika ujenzi wa matundu 20 ya vyoo, madarasa matano na nyumba moja ya mwalimu katika shule za sekondari za Pangani, Simbani na Ruvu Station.
Akizungumzia upande wa shule za msingi amesema kuwa katika bajeti hiyo zimetengwa kiasi cha shilingi milioni 943,144,394 kwa ajili ya miradi ya maendeleo  kwa elimu ya msingi.
Aidha amesema kuwa katika bajeti ya mwaka wa fedha ya 2015/ 2016 wilaya ilipokea kiasi cha shilingi milioni 140,254, 154 kwa ajili ya ujenzi wa ofisi ya mwalimu Kumba, vyumba 9 vya vya madarasa katika shule za Visiga, Lumumba, Bamba na Matuga.
Amebainisha kuwa fedha hizo pia zimetumika kwa ajili ya ujenzi wa matundu ya vyoo na ununuzi wa madawati 46, meza 4 na viti 6 kwa ajili ya shule ya Msingi ya Matuga.

VIONGOZI SIMBA WAWAJIBIKE


Na John Gagarini, Kibaha

UONGOZI wa Timu ya Soka ya Simba ya Jijini Dar es Salaam wametakiwa kuwajibika kutokana na matokeo mabaya ya timu kwenye mashindano ya Ligi Kuu ya Voda Com iliyomalizika mwishoni mwa wiki.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mjini Kibaha msemaji wa Tawi la Simba Kibaha maarufu kama “Simba Tishio” Fahim Lardhi alisema kuwa viongozi hao wamekuwa wakiwawajibisha wachezaji pale wanapofanya vibaya hivyo na wao lazima wawajibike kwa hilo.

Lardhi alisema kuwa timu hiyo imefanya vibaya kwenye misimu minne na kuifanya timu hiyo ishindwe kushiriki michuano ya kimataifa kutokana na matokeo mabaya ambapo kwa msimu huu imeshika nafasi ya tatu.

“Timu ina vitengo vingi na kamati mbalimbali hivyo kama kuna kiongozi ambaye alizembea kwenye kitengo chake na kufanya timu ifanye vibaya kwa kushindwa kutekeleza majukumu yake anapaswa kuwajibika kwa kuachia ngazi,” alisema Lardhi.

Alisema kuwa inasikitisha kuona timu inafanya vibaya kila mwaka ambapo kwa mwaka huu mwenendo wake haukuwa mzuri na kufanya timu kupata matokeo mabaya huku ikiwa imetambiwa na mtani wake Yanga kw akufungwa michezo yote.

“Tumechoka kusemwa vibaya na watani wetu hii ni fedheha kwetu tunaomba kiongozi yoyote ambaye alisababisha timu kufanya anapaswa kuwajibika kwa kuachia ngazi au kuondolewa,” alisema Lardhi.

Aidha alisema kuwa anawapongeza wanachama na wapenzi wa timu yao kwa kuwa na uvumilivu kwani kwa kipindi cha miaka minne timu yao imekuwa ikifanya vibaya lakini wametulia wakiamini kuwa timu itapata matokeo mazuri lakini imekuwa kinyume.

“Ligi imeshakwisha kila kiongozi atoe ripoti yake na kuonyesha uzaifu ulikuwa wapi ili kujipanga na msimu mwingine wa ligi ijayo ili timu ifanye vizuri na si kushika nafasi ambazo haiipi timu kushiriki michuano ya kimataifa,” alisema Lardhi.

Aliutaka uongozi kuwa makini katika usajili kwa kusajili wachezaji wenye uwezo na kuacha kusajili wachezaji wasio na uwezo kwani Simba inahitaji wachezaji wenye uwezo na si kila mchezaji anastahili kuichezea Simba kama ilivyokuwa kwa msimu huu kuwa na wachezaji wenye uwezo mdogo.

Mwisho.