UMOJA wa Kusaidiana Wanajeshi Wastaafu wa Vifaru (UKUWAWAVI) wametoa msaada wa vitu mbalimbali kwenye Kituo cha Kulea Yatima cha Buloma.waanze na kidogo walichojaliwa na hiyo ni sadaka na wataendelea kusaidia pale watakapojaliwa wakati mwingine.
UMOJA wa Kusaidiana Wanajeshi Wastaafu wa Vifaru (UKUWAWAVI) wametoa msaada wa vitu mbalimbali kwenye Kituo cha Kulea Yatima cha Buloma.
MTAA wa Machinjioni Kata ya Tangini umeishukuru Serikali kwa ujenzi wa kivuko kwenye barabara inayoelekea Shule ya Msingi Mamlaka kwa kuwaondolea adha ya wanafunzi kuvuka kwa kubebwa mgongoni.
MTAA wa Machinjioni Kata ya Tangini umeishukuru Serikali kwa ujenzi wa kivuko kwenye barabara inayoelekea Shule ya Msingi Mamlaka kwa kuwaondolea adha ya wanafunzi kuvuka kwa kubebwa mgongoni.
Hawa Wazee wangu ni Wawakilishi wa wana Kijiji cha Kwipipa kata ya Rubeho.
Walituma salam zao kupitia kwa Mhe. Diwani wiki mbili zilizopita kuwa wananiita. Na leo nimekutana nao kuwasilikiza, kumbe walitaka kunipa shukrani kwa ajili ya Mradi wa Shule ya AMALI iliyojengwa kwenye Kijiji cha Kwipipa. Wameshukuru kwa Usimamizi hadi Ukamilishaji wa shule na hatimae watoto wameanza masomo
Wazee wangu hawa tulianza nao wakati tunatafuta eneo na wakatoa eneo lote la Mradi. Wametoa salamu zao kwa Maandishi, kuongea na mwisho wakatoa mbuzi.
KIKUNDI cha wanawake cha Lulu ya Wajane kilichopo Kongowe, Manispaa ya Kibaha mkoani Pwani, kimeishukuru Manispaa ya Kibaha kwa kuwapatia mkopo wa shilingi milioni 46 uliowawezesha kuendesha na kukuza shughuli zao za kiuchumi.
Akizungumza kwa niaba ya wanakikundi, Mwenyekiti wa kikundi hicho Kanyenda Mweri amesema mkopo huo waliupata kupitia mpango wa mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri kwa makundi maalum, na wamefanikiwa kuurejesha ndani ya kipindi cha miezi 11.
Amesema kikundi chao kinajishughulisha na ufugaji wa kuku wa aina mbalimbali, ambapo huuza kuku hao kwa jumla na rejareja na hivyo kuwa chanzo kikuu cha kipato kwa wanachama wake.
Aidha, amesema baada ya mafanikio waliyoyapata, kwa sasa wanatarajia kuomba mkopo mwingine ambao utawawezesha kununua mashine ya kutotolea vifaranga ili kupanua zaidi shughuli zao za ufugaji na kuongeza uzalishaji.
Kikundi hicho kimebainisha kuwa mkopo huo umewasaidia kujikwamua kiuchumi na kuboresha maisha yao, sambamba na kutoa ajira kwa baadhi ya wananchi katika eneo lao.
Zoezi hilo limehusisha wanafunzi, walimu pamoja na viongozi wa Serikali na Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Pangani kwa lengo la kuboresha mazingira ya shule hiyo.
Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Tatu Mwambala amefafanua miti hiyo ni ya kivuli na mbao ambapo miti 220 imetolewa na kitalu cha Manispaa, miti 110 kutoka Wakala wa Misitu kupitia Shule ya Sekondari Msangani II na miti 14 ya matunda imenunuliwa na shule.
Amesema miti hiyo itasaidia kukuza stadi za utunzaji wa mazingira kwa wanafunzi pamoja na kuboresha mazingira ya shule.
Diwani wa Kata ya Pangani, John Katele amebainisha zoezi hilo ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya CCM pamoja na mikakati ya kupanda miti milioni 1.5 katika mkoa huo.
Kwa upande wake Ofisa Kilimo wa kata hiyo, Omary Ngulengule ameeleza kuwa, wanafunzi wamepata elimu ya vitendo kuhusu uchimbaji mashimo na upandaji sahihi wa miti ili wawe mabalozi wa utunzaji wa mazingira katika jamii.
Mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule hiyo, Stanley Amos ameeleza elimu waliyoipata itawasaidia kuhamasisha familia na jamii kupanda miti na kutunza mazingira.
MWENYEKITI wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii Hawa Mchafu amesema mhimili wa Mahakama unatakiwa kuangalia uwezekano wa kushughulikia kwa karibu changamoto za Wanawake ili ziweze kutatuliwa kwa wakati.Mchafu ambaue pia ni Mbunge Vitimaalumu Mkoa wa Pwani amesema Serikali inatakiwa kuweka madawati ya jinsia na dawati la msaada wa kisheria katika Halmashauri ili Wanawake wanufaike kwa kupata ushauri wa kisaikolojia utakaosaidia kujikwamua kiuchumi kwa kushirikiana na wenza wao ili kupata kipato kwa ajili ya kujikimu na familia zao.
Ametoa angalizo hilo Machi 6 alipokuwa akihutubia wakazi wa Manispaa ya Kibaha walioshiriki kwenye maadhimisho ya siku ya Wanawake duniani ambapo Manispaa hiyo ilifanya maadhimisho yake mjini Mailimoja.
Katika hotuba yake Mchafu amebainisha kwamba dawati la jinsia Polisi ambalo lina kazi ya kusikiliza na kutoa ushauri kwa matatizo yanayowasilishwa wanawake waliofanyiwa ukatili wa kijinsia, mashauri 461 yalipokelewa na kati ya hayo 63 yamepelekwa Mahakamani kwa ajili ya maamuzi zaidi.
Mwenyekiti huyo wa Kamati ya Kudimu ya Bunge amesema kauli mbiu ya Siku ya Wanawake Duniani kitaifa kwa Mwaka 2026 ni Haki na Usawa kwa Wanawake na Wasichana Msingi Jumuishi kufikia Dira 2050 inahimiza kujenga uelewa kwa jamii na wadau, kuwekeza kwenye Maendeleo Jumuishi ikiwemo kutambua Haki za Wanawake na Wasichana.
Amesema lengo lingine ni kuhakikisha Haki za Wanawake na Wasichana zinafanyiwa kazi kwa vitendo na kuleta mabadiliko ya kweli kama ilivyoainishwa kwenye nguzo za Dira 2050 .
Akizungumza katika Maadhimisho hayo Ofisa Maendeleo ya Jamii Manispaa ya Kibaha Lea Lwanji amesema kwasasa wanaendelea kuratibu shughuli za wamachinga kwa kuwatambua na kuwasajili kwenye mfumo ambapo tayari wamachinga 1,112 kati yao wakes 732 wanaume 380.
Akielezea kuhusiana na uwezeshwaji kiuchumi Lwanji amesema katika mwaka wa fedha 2025/2026 Halmashauri imetenga sh. Biln 1.1 na kwamba mikopo yenye thamani ya sh.Billion 2.1 imetolewa kwa vikundi 436 na watu binafsi 21 kati ya vikundi hivyo 275 ni vya Wanawake ambao wamepata zaidi ya sh. Billion 1.
Ofisa Maendeleo huyo amebainisha kwamba Wajasiriamali wengi wamekuwa na mwamko wa kufanya biashara na wengi wanajitokeza kutafuta fursa za mitaji katika taasisi wezeshi.
Wakati huo huo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dk Rogers Shemwelekwa amewapongeza watumishi wanawake katika Manispaa hiyo kwa mchango wao katika ukusanyaji wa mapato uliowezesha Manispaa hiyo kushika nafasi ya pili kitaifa miongoni mwa Halmashauri 184 nchini Tanzania.
Dkt. Shemwelekwa amesema Manispaa ya Kibaha imefanikiwa kushika nafasi ya pili kitaifa katika ukusanyaji wa mapato baada ya kukusanya shilingi bilioni 17, huku idara ya Uhasibu na Mapato ikiongozwa na mwanamke.
Ameongeza kuwa Halmashauri hiyo inaendelea kuimarisha ukusanyaji wa mapato ambapo kwa sasa imefikia shilingi bilioni 18, ikilinganishwa na awali ambapo ilikuwa ikikusanya shilingi bilioni 7.3.
WANANCHI wa Manispaa ya Kibaha wameendelea kujitokeza kwa wingi kupata huduma katika Kliniki ya Ardhi ijulikanayo kama Samia Ardhi Kliniki, huku baadhi yao wakiomba muda wa utoaji wa huduma hizo uongezwe kutokana na umuhimu wake.
Wananchi hao pia wameishukuru Serikali kwa kusogeza huduma hizo karibu yao na kueleza kuridhishwa na namna wanavyohudumiwa katika kliniki hiyo.
Maoni hayo yametolewa Machi 4, 2026, wakati kambi maalum ya kushughulikia masuala ya ardhi ikiendelea kwa siku ya tatu katika viwanja vya Maili Moja, Stendi ya Zamani, Manispaa ya Kibaha, ambapo wananchi wengi wameendelea kumiminika kupata huduma mbalimbali.
Mkazi wa Kibaha, Ester Joel, aliyefika katika kliniki hiyo kupata huduma ya hati, amesema ameridhishwa na huduma aliyoipata na kuomba muda wa kliniki hiyo uongezwe ili wananchi wengi zaidi wapate fursa ya kuhudumiwa.
“Nimeridhika na huduma niliyoipata hapa. Kwanza nimepokelewa vizuri na nimeelekezwa namna ya kutatua changamoto yangu. Hata hivyo, kutokana na umuhimu wa huduma hii, ningependa siku ziongezwe hata kufikia wiki mbili,” amesema Ester Joel.
Kwa upande wake Coletha Nombo, ambaye pia alifika kupata huduma ya hati, amepongeza juhudi za Serikali kwa kuwaletea wananchi huduma hiyo karibu na maeneo yao.
Naye Ruth Kadema, mkazi wa Pangani, amesema ameridhishwa na huduma aliyoipata na kueleza kuwa amepewa maelekezo ya kufika tena siku ya Jumamosi kwa ajili ya kukamilisha taratibu za kupata hati yake.
“Huduma hii ni nzuri sana. Nimeridhika na nimeambiwa nije Jumamosi kuchukua hati yangu baada ya kuwasilisha taarifa zangu leo,” amefafanua Ruth.
Kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo huadhimishwa Machi 8 kila mwaka, Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeandaa kambi hiyo maalum ya huduma za ardhi kwa lengo la kusikiliza na kutatua kero mbalimbali za wananchi zinazohusu masuala ya ardhi, hususan umilikishwaji wa ardhi na upatikanaji wa hati.
Kambi hiyo maalum ya siku sita ijulikanayo kama Samia Ardhi Kliniki ilianza rasmi Machi 2 na inatarajiwa kuhitimishwa Machi 7, 2026.
MKOA wa Pwani umeanza maandalizi ya Siku ya Wanawake Duniani ambapo kilele cha maadhimisho kimkoa yatafanyika Machi 8, 2026 katika Uwanja wa Ujamaa, Kata ya Umwe, Tarafa ya Ikwiriri, Halmashauri ya Mji Rufiji.
Mratibu wa maadhimisho hayo, Roseline Kimaro, amesema mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge.
Akizungumza kuhusu maandalizi, Kimaro amesema maadhimisho ya mwaka huu yanaongozwa na kaulimbiu isemayo, “Haki kwa Wanawake na Wasichana: Msingi wa Maendeleo Jumuishi Dira 2050,” ikisisitiza umuhimu wa usawa wa kijinsia na haki kama nguzo ya maendeleo endelevu.
Amesema lengo ni kutambua na kuenzi mchango wa wanawake katika nyanja za kijamii, kisiasa na kiuchumi, sambamba na kuimarisha mapambano dhidi ya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia.
Amebainisha kuwa kuanzia Machi 1 hadi 7 kutafanyika shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo utoaji wa elimu kwa umma na kampeni za uhamasishaji kuhusu usawa wa kijinsia, kilele cha maadhimisho Machi 8.
Ameongeza kuwa maandalizi yanaendelea vizuri na kutoa wito kwa wananchi na wadau wa maendeleo kujitokeza kwa wingi kushiriki na kuunga mkono jitihada za kulinda na kuimarisha haki za wanawake na wasichana.
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Pwani kuanza utaratibu mpya ukusanyaji mapato Bandari ya Bagamoyo Machi Mosi mwaka huu.Akizungumza na wafanyabiashara wa mafuta ya kula kwenye Bandari hiyo Meneja wa TRA Mkoa huo Masawa Masawa alisema kuwa changamoto iliyopo ni malalamiko ya wafanyabiashara kulalamikia bei ya kodi ya mafuta yanayotoka Zanzibar.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Shaibu Ndemanga alisema kuwa wananchi wengi wanategemea biashara ya mafuta na kuna wadau wengi wanategemea shughuli zinazohusiana na biashara ya mafuta.
Naye Diwani wa Kata ya Dunda Amiry Mpwimbwi alisema kuwa eneo hilo la Bandari linatoa ajira zaidi ya 8,000 hivyo kutokana na shughuli kutofanyika kumesababisha serikali kukosa mapato.
Mwenyekiti wa wafanyabiashara wa Mafuta kwenye Bandari hiyo Shaban Hamsini alisema kuwa hali imeshakuwa mbaya kwani wanategemea shughuli hizo kuendeshea maisha yao.
MWENYEKITI wa Mtaa wa Mwendapole B Manispaa ya Kibaha Abubakar Matumla ameendelea na ziara ya kutafutia majawabu changamoto zinazowakabili wananchi wa Mtaa huo.
Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha mkoani Pwani wamepitisha kwa kishindo bajeti ya mwaka wa fedha 2026/2027 yenye jumla ya Shilingi Bilioni 68.7 katika Baraza Maalum la Madiwani lililofanyika katika Ukumbi wa Manispaa ya Kibaha.
Akizungumza wakati wa kupitisha bajeti hiyo, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kibaha, Dkt. Mawazo Nicas, amesema bajeti hiyo ni chachu ya maendeleo kwa wananchi na imezingatia mahitaji halisi ya Halmashauri.
“Bajeti hii imepitia kamati zote, imejadiliwa na kuboreshwa. Ni wajibu wetu kuipitisha ili ikalete maendeleo kwa wananchi wetu,” amesema Dkt. Nicas.
Diwani wa Kata ya Kibaha, Omary Bula, amesema bajeti hiyo imeandaliwa kwa ushirikishwaji wa madiwani wote na kuwataka wajumbe kuipitisha kwa maslahi ya wananchi.
Awali akiwasilisha rasimu ya bajeti hiyo, Naibu Meya wa Manispaa ya Kibaha, Aziza Mruma, amesema Halmashauri imekisia kutumia kiasi hicho cha Shilingi Bilioni 68.7, ikiwa ni ongezeko la asilimia sita ukilinganisha na bajeti ya mwaka 2025/2026.
Kwa mujibu wa Mruma, katika mchanganuo wa bajeti hiyo, mapato ya ndani yanatarajiwa kuwa Shilingi Bilioni 17.8, miradi ya maendeleo Shilingi Bilioni 8.7, huku asilimia 60 ya mapato ya ndani ikielekezwa kwenye miradi ya maendeleo na asilimia 40 kwenye matumizi ya kawaida.
Aidha, Shilingi Bilioni 1.4 zimetengwa kwa ajili ya mikopo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu.
Katika mwaka huo wa fedha, Halmashauri inatarajia kujenga kituo kimoja cha afya na zahanati mbili, pamoja na kutekeleza miradi ya kimkakati yenye thamani ya Shilingi Bilioni 1.3. Miradi hiyo ni pamoja na ujenzi wa maegesho ya malori yenye thamani ya Shilingi Milioni 242.3, kituo cha kibiashara Mbonde, na ujenzi wa kiwanda cha kusindika nyama chenye thamani ya Shilingi Milioni 524.7.
Baada ya majadiliano, madiwani kwa pamoja waliipitisha bajeti hiyo kwa kauli moja, wakiahidi kusimamia utekelezaji wake ili kuhakikisha inaleta tija na maendeleo kwa wananchi wa Manispaa ya Kibaha.
BENKI ya NMB imeingia mkataba wa udhamini wa maonyesho ya mifugo ya (Tri-Nations Livestock Expo) kwa kiasi cha shilingi milioni 300 kwa kipindi cha miaka mitatu.
Mkataba huo umeshuhudiwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dk Fabian Madele kwenye Shamba la Mifugo la Mbogo lililopo Ubena Halmashauri ya Chalinze Wilaya ya Bagamoyo ambapo maonyesho hayo mwaka huu yatafanyika Juni 19 hadi 21.
Madele alisema kuwa maonyesho hayo ni muhimu kwani kwani yanaleta tija kwenye ufugaji kuimarisha ushirikiano kukuza teknolojia kwenye sekta ya ufugaji kukuza masoko ya ndani na nje kwani soko la nje ni kubwa sana.
"Malengo ifikapo 2030 kufikia uuzaji wa tani 50 kwa soko la nje ambalo ni kubwa sana hasa la Mshariki ya Kati na China hivyo lazima tutumie fursa kama hizi kuboresha ufugaji wetu ili uakisi uwingi wa mifugo yetu,"alisema Madele.
Alisema kuwa Tanzania ni ya pili kwa kuwa na mifugo mingi ikiwa na ngombe zaidi ya milioni 35 ma mbuzi milioni 28 hivyo lazima tafsiri ya idadi iendane na mapato.
"Tuwavutie vijana ili wajikite kwenye ufugaji kwani endapo nguvu itawekezwa itainua uchumi wa nchi na ili kufika huko ni kufuga kwa utaalamu kwani maofisa mifugo wamesambazwa kila mahali kikubwa ni kujenga mahusiano mazuri,"alisema Madele.
Kwa upande wake mwakilishi wa benki hiyo kupitia Mkuu wa Idara ya Kilimo Biashara wa Benki ya NMB Nsolo Mlozi alisema kuwa mwaka jana walidhamini maonyesho hayo kwa kiasi cha milioni 30 ambayo hufanyika kila mwaka.
Mlozi alisema kuwa udhamini huo ni wa miaka mitatu na ni sehemu ya kuboresha sekta hiyo ya ufugaji ambapo pia hutoa fursa za mikopo kwa wafugaji ambapo hadi sasa imetoa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 130.
Alisema kuwa mbali ya kutoa mikopo pia inatoa elimu ya fedha, ushauri na masoko kwa wafugaji ili kuweza kukabiliana na changamoto mbalimbali ambapo imeweka mameneja mahusiano wanaoshughulikia wafugaji.
Naye Mkurugenzi wa Shamba la Mifugo la Mbogo Naweed Mulla alisema kuwa maonyesho hayo yamekuwa na mafanikio makubwa ambapo wafugaji wengi walijitokeza kushiriki na mwaka huu wataongezeka zaidi wakiwemo wafugaji toka nchi mbili jirani.
Mulla alisema kuwa mwaka huu wameongeza kipengele cha ufugaji wa kuku kwa upande wa wanawake ambapo kutakuwa na mshindi ambaye atatambulika kama Malkia wa ufugaji.
Mwenyekiti wa Chama Cha Wafugaji Mrida Maroche alisema kuwa wanapongeza uwekezaji unaofanyika kwenye mifugo kwani unapandisha thamani ya mifugo yao na watatumia fursa mbalimbali ili kuongeza uzalishaji kwa kuzingatia viwango ili kukabili soko la nje.
Maroche alisema kuwa mfano mzuri ni baadhi ya ngombe waliopo kwenye Shamba la Mbogo ngombe wa miaka miwili ana uzito wa kilogramu 350 na ndama wa miezi mitano ana uzito wa kilogramu 180 ambapo hayo ni mabadiliko makubwa.
The Government has announced a historic measure that could significantly transform the landscape of Tanzania’s digital content industry.
Speaking at the Annual Broadcasting Service Providers Conference (ABC 2026) in Dodoma, the Deputy Minister for Information, Culture, Arts and Sports, Hamisi Mwinjuma, revealed that the licence fee for online content creators has been reduced from TSh 500,000 to just TSh 50,000, with an application fee of only TSh 10,000.
This represents a reduction of more than 90 per cent — a move widely interpreted as opening a new door for young innovators, bloggers, and digital creators who had previously struggled with the high cost of compliance.
The decision follows nearly a year of strategic consultations between the Tanzania Bloggers Network (TBN) and the Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA), aimed at addressing financial barriers that had constrained the growth of digital journalism and online content production in the country.
In addition, licence fees for Online Content Aggregators have been reduced from TSh 1,000,000 to TSh 100,000.
A new “Amateur” category has also been introduced specifically for emerging young creators, enabling them to formalise their activities and nurture their talents without heavy financial burdens.
Within the broader context of a rapidly expanding digital economy, this decision is expected to stimulate employment, creativity, and tax revenue generation — in line with the development vision championed by President Samia Suluhu Hassan.
If effectively implemented, these reforms may well mark the beginning of a new chapter for Tanzania’s digital creative sector.
Serikali imetangaza hatua ya kihistoria inayoweza kubadili sura ya tasnia ya maudhui ya kidijitali nchini. Kupitia tamko lililotolewa katika Mkutano wa Mwaka wa Watoa Huduma za Utangazaji (ABC 2026) jijini Dodoma, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamisi Mwinjuma, amesema ada ya leseni kwa watoa maudhui mtandaoni imeshushwa kutoka Sh500,000 hadi Sh50,000, huku ada ya maombi ikiwa Sh10,000 pekee.
Ni punguzo la zaidi ya asilimia 90, hatua ambayo wengi wameitafsiri kama mlango mpya kwa vijana wabunifu, wanablogu na watengeneza maudhui waliokuwa wakikwama kwa gharama.
Hatua hiyo imekuja baada ya mazungumzo ya karibu mwaka mzima kati ya Tanzania Bloggers Network (TBN) na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), yakilenga kuondoa vikwazo vilivyokuwa vikizuia ukuaji wa sekta hii.
Zaidi ya hayo, ada ya wakusanyaji wa maudhui (Online Content Aggregators) imeshuka kutoka Sh1,000,000 hadi Sh100,000.
Aidha, kundi jipya la “Amateur” limeanzishwa mahsusi kwa vijana wanaochipukia, likiwawezesha kujisajili rasmi bila mzigo wa kifedha.
Kwa muktadha wa uchumi wa kidijitali unaokua kwa kasi, uamuzi huu unaweza kuwa kichocheo kikubwa cha ajira, ubunifu na mapato ya kodi kwa taifa, kama yalivyo maono ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.
SERIKALI imetangaza neema ya kihistoria kwa wanablogu, vijana wabunifu, na watoa maudhui mtandaoni nchini kwa kupunguza ada za leseni kwa kiwango kikubwa, hatua inayolenga kuchochea ukuaji wa uchumi wa kidijitali na kurasimisha shughuli za wahabarishaji wa mitandao.
Hatua hiyo imekuja kufuatia utafiti wa kina na mikutano ya kimkakati ya takribani mwaka mzima kati ya mtandao wa Tanzania Bloggers Network (TBN) na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), ikielezea vikwazo vya gharama vilivyokuwa vikikwaza uandishi wa habari za kidijitali nchini.
Akizungumza katika ufunguzi wa Mkutano wa Mwaka wa Watoa Huduma za Utangazaji (ABC 2026) jijini Dodoma leo, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamisi Mwinjuma, amesema ada ya leseni kwa watoa maudhui mtandaoni imeshushwa kutoka Sh500,000 hadi Sh50,000 tu, huku ada ya maombi ikiwa ni Sh10,000 pekee.
Mageuzi hayo pia yamegusa kundi la wakusanyaji wa maudhui (Online Content Aggregators), ambao ada yao imeshushwa kutoka Sh1,000,000 hadi Sh100,000 pekee. Aidha, kundi la "Amateteur" limeanzishwa kwa ajili ya vijana wanaochipukia ili waweze kujitambulisha rasmi na kukuza vipaji vyao bila vikwazo vya kifedha.
Mapinduzi ya Teknolojia ya DSB
Wakati neema hiyo ikitangazwa, Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Dkt. Jabiri Bakari, ametangaza kuanza kwa teknolojia mpya ya utangazaji wa redio ya kidijitali nchini inayojulikana kama Digital Sound Broadcasting (DSB).
Teknolojia hiyo itaanza kufanya kazi katika mikoa mitano ya majaribio ya Dar es Salaam, Dodoma, Mwanza, Arusha, na Mbeya, lengo likiwa ni kuongeza ubora wa sauti na huduma za utangazaji nchini.
"Tumekamilisha maandalizi yote ya kiudhibiti na watoa huduma wa miundombinu wameshapatikana. Hii ni hatua kubwa ya kuendana na mabadiliko ya teknolojia duniani na kuimarisha utangazaji, hususan maeneo ya vijijini," alisema Dkt. Bakari.
Utafiti: Redio Bado ni Kinara
Katika mkutano huo, Injinia Andrew Kisaka wa TCRA amewasilisha matokeo ya utafiti wa hali ya utangazaji kwa mwaka 2025/2026, ukionyesha kuwa redio inaendelea kuwa chanzo kikuu cha habari kwa asilimia 85 ya Watanzania. Hata hivyo, utafiti huo umebaini ukuaji mkubwa wa matumizi ya intaneti miongoni mwa vijana, ambapo asilimia 45 hupata habari kupitia mitandao ya kijamii kabla ya kusikiliza redio au kutazama televisheni.
Upande wa televisheni, utafiti unaonyesha asilimia 65 ya watazamaji wanatumia ving'amuzi, huku maudhui ya ndani yakipendwa zaidi kwa asilimia 70. Serikali imewahimiza watoa huduma za kienyeji kuwekeza zaidi kwenye majukwaa ya kidijitali (OTT) ili kukidhi mahitaji ya soko la sasa.
Ulinzi wa Hakimiliki na Mikopo
Ili kuhakikisha wanahabari wa kidijitali wanufaika na kazi zao, Serikali imezielekeza taasisi za COSOTA na TCRA kuandaa mpango wa kulinda hakimiliki na kudhibiti uharamia mtandaoni. Aidha, Serikali imeanza kutoa mikopo ya masharti nafuu kwa watengeneza maudhui kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya kisasa vya kufanyia kazi.
Hadi kufikia Desemba 2025, TCRA imetoa jumla ya leseni 707 za utangazaji, zikiwemo 318 za maudhui mtandaoni, jambo linaloashiria kukua kwa uhuru wa habari na demokrasia nchini chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan.
Na Allan Kitwe, Sikonge
RAIS wa Awamu ya Sita wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan amepeleka tabasamu kwa wakazi wa Wilaya ya Sikonge Mkoani Tabora baada ya maji safi na salama kutoka Ziwa Viktoria kufika Wilayani humo.
Shangwe na furaha za wananchi zimelipuka kwenye hafla ya kufungulia maji hayo iliyofanyika juzi katika Kata ya Misheni Mjini Sikonge kwenye eneo lilipojengwa tanki kubwa la kupokelea maji hayo ili yaanze kusambazwa kwa wananchi.
Akizungumza na mamia ya wananchi, wadau wa maendeleo na viongozi mbalimbali wa chama na serikali kwenye hafla hiyo, Waziri wa Maji Mheshimiwa Jumaa Aweso ameeleza kufurahishwa na kazi nzuri ya utekelezaji mradi huo.
Amesema kuwa mradi huo ambao unatekelezwa na Mkandarasi kutoka China kwa gharama ya shilingi bilioni 143 umelenga kufikisha huduma ya maji safi na salama katika Wilaya tatu za Urambo, Kaliua na Sikonge yenyewe.
‘Ndugu zangu wana Sikonge, Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ameleta tabasamu kwenu, alipoingia madarakani, aliahidi kumaliza kero yenu ya maji ili akinamama wasitembee na ndoo kichwani umbali mrefu na leo hii maji yamefika’, amesema.
‘Kazi iliyobakia sasa ni kuyasambaza kwa wananchi, katika hili Wataalamu ongezeni kasi, na kila wananchi atakayetaka kuunganishiwa maji nyumbani kwake hakikisheni ndani ya siku 7 awe amepata maji, si vinginevyo’, ameonya.
Aidha Waziri Aweso amemwagiza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Mhandisi Mwajuma Waziri kuleta timu ya Wataalamu katika Wilaya hiyo ili kushughulikia mradi wa Bwawa la Utyatya ili uanze kufanya kazi ili kusaidiana na mradi huo.
Ameongeza kuwa kila Mtendaji wa Wizara hiyo anapaswa kuwa mwadilifu na mchapa kazi, Mtendaji mbabaishaji hana nafasi, hivi karibuni tutafanya tathmini ya Utendaji wa kila mmoja na kuchukua hatua kwa wanaozembea.
Amempongeza Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Tabora (TUWASA) Mhandisi Mayunga Kashilimu, RUWASA Mhandisi Hatari Kapufi, Mkuu wa Wilaya Thomas Myinga na Mbunge Amos Maganga kwa kusimamia vizuri utekelezaji mradi huo.
Katika kuhakikisha taasisi zinajengewa uwezo wa kiimadili katika kazi
Mtaalamu wa Kidiplomasia, Uongozi na maadili Ndugu Omary Abdull Punzi amewelekeza na kuwakumbusha taasisi ya SMAUJATA katika mafunzo yaliyoandaliwa na taasisi hiyo kufanyika Februari 7 hadi 8 mwaka 2026 katika Ukumbi wa Chuo Cha VETA Keko Dar es Salaam.