Sunday, March 22, 2026

UKUWAWAVI WATOA MISAADA KITUO CHA YATIMA BULOMA


UMOJA wa Kusaidiana Wanajeshi Wastaafu wa Vifaru (UKUWAWAVI) wametoa msaada wa vitu mbalimbali kwenye Kituo cha Kulea Yatima cha Buloma.
Wametoa misaada hiyo ikiwa ni sehemu ya kusherehekea Sikukuu ya Iddi el Fitri na Mfungo wa Kwaresma.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukabidhi misaada hiyo Mwenyekiti wa (UKUWAWAVI) SSGT Omari Makore amesema kuwa wameguswa kuwasaidia watoto hao ili nao waweze kufurahi kama walivyo watoto wanaoishi na familia zao.

Makore amesema wanajua kuwa watoto hao wana mahitaji mengi lakini wameona
waanze na kidogo walichojaliwa na hiyo ni sadaka na wataendelea kusaidia pale watakapojaliwa wakati mwingine.

"Tutarudi tena kwani watoto hawa wametuonyesha mapenzi makubwa na huu ni mfano na vikundi na watu mbalimbali nao wajitokeze kuwasaidia watoto hawa,"amesema Makore.

Kwa upande wake Mlezi wa (UKUWAWAVI) Brigedia Jenerali Rajabu Hanti (Mstaafu) amesema kuwa watoto hao ni Taifa la kesho wanahitaji malezi ya watu.

Hanti amesema kuwa watoto hao wanapaswa kupelekewa furaha kwa kuwashika mkono kwa misaada mbalimbali ambayo ni mahitaji yao ya msingi.

Naye Mchungaji Jackson Bukelebe amesema kuwa umoja huo umechukua jukumu la kidini kwani dini bora ni ile inayojali yatima watu wanapaswa kujotolea kuwasaidia watoto hao.

Mwasisi wa kituo hicho Anna Kyando amesema kuwa wanashukuru kwa misaada hiyo kwani wadau ndiyo wamekuwa wakiendesha kituo hicho kwani bila wao peke yake asingeweza.

Kyando amesema kuwa changamoto kubwa ni chakula kwani ndicho kinachohitajika muda wote uzio wa ukufa, vifaa vya shule, ada kwa wanafunzi walioko vyuoni kutoka kituo hicho.

Moja ya watoto wa kituo hicho Yohana Almas amesema kuwa wanashukuru kwa misaada hiyo na kuahidi kufanya vizuri kwenye masomo yao na kuomba watu waendelee kuwasaidia.

Baadhi ya vitu vilivyotolewa ni pamoja na mchele kilo 100, unga wa sembe kilo 50, maharage kilo 50, mafuta lita 20, madaftari 100, juisi katoni 5, maji katoni 10, doti 5 za khanga, sabuni za unga, taulo za kike na biskuti.

Saturday, March 21, 2026

DA ARUL ARQAM LEARNING CENTRE (DAALC) KUJENGA HOSPITALI YA KISASA.

TAASISI ya DA ARUL ARQAM LEARNING CENTRE (DAALC) ya Kibaha Mkoani Pwani inatarajia kujenga kituo cha taasisi chenye huduma mbalimbali za kijamii kikiwa ni pamoja Hospitali ya kisasa kwa gharama za shilingi bilioni 5.5.


Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mwalimu wa Taasisi hiyo Karume Amri Abeid amesema kuwa kituo hicho kitajengwa eneo la Boko Wilaya ya Kibaha.

Abeid amesema kuwa eneo hilo ndilo litakalokuwa makao makuu ya Taasisi ambalo lina ukubwa wa hekari 11 na tayari nyumba ya mlinzi tayari imejengwa kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi.

"Eneo hilo pia kutajengwa ofisi, Msikiti, shule ya awali hadi elimu ya juu yaani kidato cha sita, chuo cha elimu ya dini Ibtidai mpaka Thanawi, kituo cha kuhifadhisha Quran kwa watoto kuanzia miaka 5 na kuendelea,"amesema Abeid.

Amesema kuwa njia watakayoitumia kupata fedha ni michango mbalimbali toka kwa wadau, waumini na kufanya harambee ambapo hadi sasa wamekusanya kiasi cha shilingi milioni 2.

"Huduma zikiwemo za afya zitatolewa kulingana na jinsi badala ya huduma kutolewa na jinsi tofauti na wanufaika kwenye sekta ya afya na ajira haitajali dini bali ni kwa dini zote kwani lengo ni kutoa huduma bora na za kisasa,"amesema Abeid.

Aidha amesema kuwa matarajio ni kuanza ujenzi Januari mwakani mara fedha zitakapopatikana na kikubwa wadau mbalimbali wajitokeze kuchangia fedha ili kufanikisha ujenzi huo kwani watu wajitoe kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na kujenga ahera yetu.

Akizungumzia kuhusu sikukuu ya Iddi amesema kuwa siyo kuvaa vizuri na kupendeza bali ni kwa yule mwenye kumuogopa Mwenyezi Mungu na kukumbuka siku ya hesabu (Kiyama) ndiyo maana ya Iddi.

Ameongeza kuwa watu wamwabudu Mwenyezi Mungu na kuacha kumkasirisha na waishi maisha haya na si wakati wa mfungo peke yake ili wasimkosee.

DA ARUL ARQAM LEARNING CENTRE (DAALC) KUJENGA HOSPITALI YA KISASA.

TAASISI ya DA ARUL ARQAM LEARNING CENTRE (DAALC) ya Kibaha Mkoani Pwani inatarajia kujenga kituo cha taasisi chenye huduma mbalimbali za kijamii kikiwa ni pamoja Hospitali ya kisasa kwa gharama za shilingi bilioni 5.5.


Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mwalimu wa Taasisi hiyo Karume Amri Abeid amesema kuwa kituo hicho kitajengwa eneo la Boko Wilaya ya Kibaha.

Abeid amesema kuwa eneo hilo ndilo litakalokuwa makao makuu ya Taasisi ambalo lina ukubwa wa hekari 11 na tayari nyumba ya mlinzi tayari imejengwa kwa ajili ya maandalizi ya ujenzi.

"Eneo hilo pia kutajengwa ofisi, Msikiti, shule ya awali hadi elimu ya juu yaani kidato cha sita, chuo cha elimu ya dini Ibtidai mpaka Thanawi, kituo cha kuhifadhisha Quran kwa watoto kuanzia miaka 5 na kuendelea,"amesema Abeid.

Amesema kuwa njia watakayoitumia kupata fedha ni michango mbalimbali toka kwa wadau, waumini na kufanya harambee ambapo hadi sasa wamekusanya kiasi cha shilingi milioni 2.

"Huduma zikiwemo za afya zitatolewa kulingana na jinsi badala ya huduma kutolewa na jinsi tofauti na wanufaika kwenye sekta ya afya na ajira haitajali dini bali ni kwa dini zote kwani lengo ni kutoa huduma bora na za kisasa,"amesema Abeid.

Aidha amesema kuwa matarajio ni kuanza ujenzi Januari mwakani mara fedha zitakapopatikana na kikubwa wadau mbalimbali wajitokeze kuchangia fedha ili kufanikisha ujenzi huo kwani watu wajitoe kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na kujenga ahera yetu.

Akizungumzia kuhusu sikukuu ya Iddi amesema kuwa siyo kuvaa vizuri na kupendeza bali ni kwa yule mwenye kumuogopa Mwenyezi Mungu na kukumbuka siku ya hesabu (Kiyama) ndiyo maana ya Iddi.

Ameongeza kuwa watu wamwabudu Mwenyezi Mungu na kuacha kumkasirisha na waishi maisha haya na si wakati wa mfungo peke yake ili wasimkosee.

Thursday, March 12, 2026

KIVUKO MKOMBOZI WANAFUNZI SHULE YA MAMLAKA

 MTAA wa Machinjioni Kata ya Tangini umeishukuru Serikali kwa ujenzi wa kivuko kwenye barabara inayoelekea Shule ya Msingi Mamlaka kwa kuwaondolea adha ya wanafunzi kuvuka kwa kubebwa mgongoni.

Ujenzi wa kivuko hicho ambacho kimewekwa makalavati mawili kimeweza kuwaondolea adha wanafunzi wa shule hiyo ambapo kipindi cha mvua walishindwa kuvuka hadi wavushwe na watu wazima. 

Akizungumza na Mwenyekiti wa Mtaa huo Aidan Mchiwa amesema kuwa mbali ya changamoto iliyokuwepo kwa wanafunzi lakini pia iliwakumba wakazi wa maeneo karibu na shule hiyo.

Mchiwa amesema kuwa manufaa ya kivuko hicho yameonekana ambapo mvua kubwa zilizonyesha juzi wanafunzi na wananchi wanavuka bila ya shida yoyote tofauti na ilivyokuwa awali ikiwa ni wakati wa siku 100 za Rais Dk Samia Suluhu Hassan.

"Eneo hilo ni mkondo wa maji hivyo mvua zinazonyesha maeneo mbalimbali maji yake yanapita hapo kwani ni eneo ambalo kuna bonde hivyo maji yanakuwa mengi na kusababisha adha kwa watu wanaopita kwenye barabara hiyo inayoelekea shuleni,"amesema Mchiwa.

Amesema kuwa serikali kupitia Halmashauri ilitoa fedha kiasi cha shilingi milioni 9 na kwa kushirikiana na wananchi walifanikiwa kujenga kivuko hicho ambapo hata magari na pikiiki yalikuwa yakipita kwa shida.

"Kuna maboresho kidogo yanatakiwa kufanyika ikiwa ni pamoja na mitaro na tukifanikiwa kupata fedha tutaichimba kwani bajeti tuliyopewa ya ujenzi wa kivuko hicho iliisha tutaomba kwa bajeti hii ili tuboreshe zaidi,"amesema Mchiwa.

Aidha amesema kuwa pia kwa kushirikiana na wananchi walifungua barabara tatu za Aidan, Nida na Kilima huku mbili zikiwa zimebakia za kwa Kapungu na kwa Landa.

KIVUKO MKOMBOZI WANAFUNZI SHULE YA MAMLAKA

MTAA wa Machinjioni Kata ya Tangini umeishukuru Serikali kwa ujenzi wa kivuko kwenye barabara inayoelekea Shule ya Msingi Mamlaka kwa kuwaondolea adha ya wanafunzi kuvuka kwa kubebwa mgongoni.

Ujenzi wa kivuko hicho ambacho kimewekwa makalavati mawili kimeweza kuwaondolea adha wanafunzi wa shule hiyo ambapo kipindi cha mvua walishindwa kuvuka hadi wavushwe na watu wazima. 

Akizungumza na Mwenyekiti wa Mtaa huo Aidan Mchiwa amesema kuwa mbali ya changamoto iliyokuwepo kwa wanafunzi lakini pia iliwakumba wakazi wa maeneo karibu na shule hiyo.

Mchiwa amesema kuwa manufaa ya kivuko hicho yameonekana ambapo mvua kubwa zilizonyesha juzi wanafunzi na wananchi wanavuka bila ya shida yoyote tofauti na ilivyokuwa awali ikiwa ni wakati wa siku 100 za Rais Dk Samia Suluhu Hassan.

"Eneo hilo ni mkondo wa maji hivyo mvua zinazonyesha maeneo mbalimbali maji yake yanapita hapo kwani ni eneo ambalo kuna bonde hivyo maji yanakuwa mengi na kusababisha adha kwa watu wanaopita kwenye barabara hiyo inayoelekea shuleni,"amesema Mchiwa.

Amesema kuwa serikali kupitia Halmashauri ilitoa fedha kiasi cha shilingi milioni 9 na kwa kushirikiana na wananchi walifanikiwa kujenga kivuko hicho ambapo hata magari na pikiiki yalikuwa yakipita kwa shida.

"Kuna maboresho kidogo yanatakiwa kufanyika ikiwa ni pamoja na mitaro na tukifanikiwa kupata fedha tutaichimba kwani bajeti tuliyopewa ya ujenzi wa kivuko hicho iliisha tutaomba kwa bajeti hii ili tuboreshe zaidi,"amesema Mchiwa.

Aidha amesema kuwa pia kwa kushirikiana na wananchi walifungua barabara tatu za Aidan, Nida na Kilima huku mbili zikiwa zimebakia za kwa Kapungu na kwa Landa.

Wednesday, March 11, 2026

BIDHAA SOKO LA LOLIONDO BEI NZURI

BEI ya Vitunguu kwenye Soko la Loliondo Halmashauri ya Manispaa Kibaha iko juu kutoka shilingi 130,000 hadi 250,000 kwa gunia.

Aidha viazi mbatata ambavyo ni maarufu kwa ajili ya kukaangia chipsi vimeshuka bei kutoka shilingi 140,000 hadi 70,000 kwa gunia.

Akizungumza ofisini kwake Mjini Kibaha Naibu Katibu Mkuu wa soko hilo Alex Msimbe alisema kuwa kwa sasa bidhaa nyingi bei zake hazijapanda sana bali bei iko wastani.

Msimbe alisema kuwa bei hiyo ya vitungu imeongezeka sana kutokana na kipindi hichi ndiyo bei huwa inapanda sana lakini baadaye bei hiyo itashuka.

"Bei ya tenga la nyanya  imeshuka kutoka kati ya shilingi 85,000 na 70,000 hadi 35,000 huku mchele ukiuzwa kati ya shilingi 3,000, 2,500 hadi 2,700 kwa kilo na maharage yakiuzwa kati ya shilingi 2,700 hadi 3,000 kwa kilo.

Alisema kuwa bei ya unga wa sembe ni kati ya shilingi 1,400 na 1,500 kwa kilo na ngano ni shilingi 125,000 kwa kilo 50 huku sukari ikiuzwa shilingi 3,000 kwa kilo.

"Bei za bidhaa nyingi bei hazijapanda kwani kipindi hichi ni cha baadhi ya maeneo ni mavuno na mengine ndiyo wamepanda muda siyo mrefu hivyo kutoathiri sana bei,"alisema Msimbe.

Aidha alisema kuwa kwa sasa hakuna changamoto kwenye soko hilo kwani miundombinu ikiwemo ya maji, umeme na huduma muhimu kama za vyoo zote ziko vizuri kwani wanashirikiana vizuri na Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha ambao ndiyo wanaowasimamia.

"Kuhusu mitaji baadhi ya wafanyabiashara wananufaika na mikopo ya Halmashauri ile ya asilimia 10 na asilimia 7,"alisema Msimbe.

Tuesday, March 10, 2026

DED GAIRO APONGEZWA UJENZI WA SHULE YA AMALI

Hawa Wazee wangu ni Wawakilishi wa wana Kijiji cha Kwipipa kata ya Rubeho.

Walituma salam zao kupitia kwa Mhe. Diwani wiki mbili zilizopita kuwa wananiita. Na leo nimekutana nao kuwasilikiza, kumbe walitaka kunipa shukrani kwa ajili ya Mradi wa Shule ya AMALI iliyojengwa kwenye Kijiji cha Kwipipa. Wameshukuru kwa Usimamizi hadi Ukamilishaji wa shule na hatimae watoto wameanza masomo

Wazee wangu hawa tulianza nao wakati tunatafuta eneo na wakatoa eneo lote la Mradi. Wametoa salamu zao kwa Maandishi, kuongea na mwisho wakatoa mbuzi.


Saturday, March 7, 2026

KIKUNDI CHA LULU YA WAJANE WAISHUKURU MANISPAA YA KIBAHA KWA MKOPO WA MILIONI 46

KIKUNDI cha wanawake cha Lulu ya Wajane kilichopo  Kongowe, Manispaa ya Kibaha mkoani Pwani, kimeishukuru Manispaa ya Kibaha kwa kuwapatia mkopo wa shilingi milioni 46 uliowawezesha kuendesha na kukuza shughuli zao za kiuchumi.

Akizungumza kwa niaba ya wanakikundi, Mwenyekiti wa kikundi hicho Kanyenda Mweri amesema mkopo huo waliupata kupitia mpango wa mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri kwa makundi maalum, na wamefanikiwa kuurejesha ndani ya kipindi cha miezi 11.

Amesema kikundi chao kinajishughulisha na ufugaji wa kuku wa aina mbalimbali, ambapo huuza kuku hao kwa jumla na rejareja na hivyo kuwa chanzo kikuu cha kipato kwa wanachama wake.

Aidha, amesema baada ya mafanikio waliyoyapata, kwa sasa wanatarajia kuomba mkopo mwingine ambao utawawezesha kununua mashine ya kutotolea vifaranga ili kupanua zaidi shughuli zao za ufugaji na kuongeza uzalishaji.

Kikundi hicho kimebainisha kuwa mkopo huo umewasaidia kujikwamua kiuchumi na kuboresha maisha yao, sambamba na kutoa ajira kwa baadhi ya wananchi katika eneo lao.

PANGANI SEKONDARI WAPANDA MITI 344

SHULE ya Sekondari Pangani, Manispaa ya Kibaha imefanya zoezi la kupanda miti zaidi ya 344 katika mazingira ya shule hiyo ikiwa ni sehemu ya kutekeleza agizo la Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan la kuhimiza taasisi za elimu kuhifadhi mazingira na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Zoezi hilo limehusisha wanafunzi, walimu pamoja na viongozi wa Serikali na Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Pangani kwa lengo la kuboresha mazingira ya shule hiyo.

Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Tatu Mwambala amefafanua miti hiyo ni ya kivuli na mbao ambapo miti 220 imetolewa na kitalu cha Manispaa, miti 110 kutoka Wakala wa Misitu kupitia Shule ya Sekondari Msangani II na miti 14 ya matunda imenunuliwa na shule.

Amesema miti hiyo itasaidia kukuza stadi za utunzaji wa mazingira kwa wanafunzi pamoja na kuboresha mazingira ya shule.

Diwani wa Kata ya Pangani, John Katele amebainisha zoezi hilo ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya CCM pamoja na mikakati ya kupanda miti milioni 1.5 katika mkoa huo.

Kwa upande wake Ofisa Kilimo wa kata hiyo, Omary Ngulengule ameeleza kuwa, wanafunzi wamepata elimu ya vitendo kuhusu uchimbaji mashimo na upandaji sahihi wa miti ili wawe mabalozi wa utunzaji wa mazingira katika jamii.

Mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule hiyo, Stanley Amos ameeleza elimu waliyoipata itawasaidia kuhamasisha familia na jamii kupanda miti na kutunza mazingira.

MUHIMILI WA MAHAKAMA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WANAWAKE KWA WAKATI

MWENYEKITI wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii Hawa Mchafu amesema mhimili wa Mahakama unatakiwa kuangalia uwezekano wa kushughulikia kwa karibu changamoto za Wanawake ili ziweze kutatuliwa kwa wakati.

Mchafu ambaue pia ni Mbunge Vitimaalumu Mkoa wa Pwani amesema Serikali inatakiwa kuweka madawati ya jinsia na dawati la msaada wa kisheria katika Halmashauri ili Wanawake wanufaike kwa kupata ushauri wa kisaikolojia utakaosaidia kujikwamua kiuchumi kwa kushirikiana na wenza wao ili kupata kipato kwa ajili ya kujikimu na familia zao.

Ametoa angalizo hilo Machi 6 alipokuwa akihutubia wakazi wa Manispaa ya Kibaha walioshiriki kwenye maadhimisho ya siku ya Wanawake duniani ambapo Manispaa hiyo ilifanya maadhimisho yake mjini Mailimoja.

Katika hotuba yake Mchafu amebainisha kwamba dawati la jinsia Polisi ambalo lina kazi ya kusikiliza na kutoa ushauri kwa matatizo yanayowasilishwa wanawake waliofanyiwa ukatili wa kijinsia, mashauri 461 yalipokelewa na kati ya hayo  63 yamepelekwa Mahakamani kwa ajili ya maamuzi zaidi. 

Mwenyekiti huyo wa Kamati ya Kudimu ya Bunge amesema kauli mbiu ya Siku ya Wanawake Duniani kitaifa kwa Mwaka 2026 ni Haki na Usawa kwa Wanawake na Wasichana Msingi Jumuishi kufikia Dira 2050 inahimiza kujenga uelewa kwa jamii na wadau, kuwekeza kwenye Maendeleo Jumuishi ikiwemo kutambua Haki za Wanawake na Wasichana.

Amesema lengo lingine ni kuhakikisha Haki za Wanawake na Wasichana  zinafanyiwa kazi kwa vitendo na kuleta mabadiliko ya kweli kama ilivyoainishwa kwenye nguzo za Dira 2050 . 

Akizungumza katika Maadhimisho hayo Ofisa Maendeleo ya Jamii Manispaa ya Kibaha Lea Lwanji amesema kwasasa wanaendelea kuratibu shughuli za wamachinga kwa kuwatambua na kuwasajili kwenye mfumo ambapo tayari wamachinga 1,112 kati yao wakes 732 wanaume 380.

Akielezea kuhusiana na uwezeshwaji kiuchumi Lwanji amesema katika mwaka wa fedha 2025/2026 Halmashauri imetenga sh. Biln 1.1 na kwamba mikopo yenye thamani ya sh.Billion 2.1 imetolewa kwa vikundi 436 na watu binafsi 21 kati ya vikundi hivyo 275 ni vya Wanawake ambao wamepata zaidi ya sh. Billion 1.

Ofisa Maendeleo huyo amebainisha kwamba Wajasiriamali wengi wamekuwa na mwamko wa kufanya biashara na wengi wanajitokeza kutafuta fursa za mitaji katika taasisi wezeshi.

Wakati huo huo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dk Rogers Shemwelekwa amewapongeza watumishi wanawake katika Manispaa hiyo kwa mchango wao katika ukusanyaji wa mapato uliowezesha Manispaa hiyo kushika nafasi ya pili kitaifa miongoni mwa Halmashauri 184 nchini Tanzania.

Dkt. Shemwelekwa amesema Manispaa ya Kibaha imefanikiwa kushika nafasi ya pili kitaifa katika ukusanyaji wa mapato baada ya kukusanya shilingi bilioni 17, huku idara ya Uhasibu na Mapato ikiongozwa na mwanamke.

Ameongeza kuwa Halmashauri hiyo inaendelea kuimarisha ukusanyaji wa mapato ambapo kwa sasa imefikia shilingi bilioni 18, ikilinganishwa na awali ambapo ilikuwa ikikusanya shilingi bilioni 7.3.

WANANCHI WAMIMINIKA KLINIKI YA ARDHI KIBAHA WAOMBA SIKU ZIONGEZWE

 

WANANCHI wa Manispaa ya Kibaha wameendelea kujitokeza kwa wingi kupata huduma katika Kliniki ya Ardhi ijulikanayo kama Samia Ardhi Kliniki, huku baadhi yao wakiomba muda wa utoaji wa huduma hizo uongezwe kutokana na umuhimu wake.

Wananchi hao pia wameishukuru Serikali kwa kusogeza huduma hizo karibu yao na kueleza kuridhishwa na namna wanavyohudumiwa katika kliniki hiyo.

Maoni hayo yametolewa Machi 4, 2026, wakati kambi maalum ya kushughulikia masuala ya ardhi ikiendelea kwa siku ya tatu katika viwanja vya Maili Moja, Stendi ya Zamani, Manispaa ya Kibaha, ambapo wananchi wengi wameendelea kumiminika kupata huduma mbalimbali.

Mkazi wa Kibaha, Ester Joel, aliyefika katika kliniki hiyo kupata huduma ya hati, amesema ameridhishwa na huduma aliyoipata na kuomba muda wa kliniki hiyo uongezwe ili wananchi wengi zaidi wapate fursa ya kuhudumiwa.

“Nimeridhika na huduma niliyoipata hapa. Kwanza nimepokelewa vizuri na nimeelekezwa namna ya kutatua changamoto yangu. Hata hivyo, kutokana na umuhimu wa huduma hii, ningependa siku ziongezwe hata kufikia wiki mbili,” amesema Ester Joel.

Kwa upande wake Coletha Nombo, ambaye pia alifika kupata huduma ya hati, amepongeza juhudi za Serikali kwa kuwaletea wananchi huduma hiyo karibu na maeneo yao.

Naye Ruth Kadema, mkazi wa Pangani, amesema ameridhishwa na huduma aliyoipata na kueleza kuwa amepewa maelekezo ya kufika tena siku ya Jumamosi kwa ajili ya kukamilisha taratibu za kupata hati yake.

“Huduma hii ni nzuri sana. Nimeridhika na nimeambiwa nije Jumamosi kuchukua hati yangu baada ya kuwasilisha taarifa zangu leo,” amefafanua Ruth.

Kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo huadhimishwa Machi 8 kila mwaka, Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeandaa kambi hiyo maalum ya huduma za ardhi kwa lengo la kusikiliza na kutatua kero mbalimbali za wananchi zinazohusu masuala ya ardhi, hususan umilikishwaji wa ardhi na upatikanaji wa hati.

Kambi hiyo maalum ya siku sita ijulikanayo kama Samia Ardhi Kliniki ilianza rasmi Machi 2 na inatarajiwa kuhitimishwa Machi 7, 2026.

Friday, March 6, 2026

UMILIKI RASILIMALI KWA WANAWAKE WAPUNGUZA VITENDO VYA UKATILI

SERIKALI imeweka mazingira wezeshi ikiwa ni pamoja na umiliki rasilimali ili kupunguza vitendo vya ukatili kwa wanawake kuelekea Dira ya Maendeleo ya mwaka 2050.

Akizungumza wakati wa sherehe za Siku ya Wanawake Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Pwani Hawa Mchafu amesema uwepo wa mazingira hayo unaondoa ukatili wa kijinsia.

Mchafu amesema kuwa uwepo wa usawa na kulinda kulinda haki za wanawake kuna mchango mkubwa katika suala la maendeleo.

"Usawa wezeshi hiyo ni nyenzo muhimu ili kuketa utandaji wa pamoja wa kufikia malengo ya dira ya maendeleo na kuongeza ushiriki wanawake kwenye masuala muhimu yakiwemo ya uongozi,"amesema Mchafu.

Amesema kuwa dhumuni la kuwarudisha wasichana waliopata mimba wakiwa shuleni ni kutimiza ndoto zao kwani siyo wote waliopata ujauzito kwa kupenda au tamaa bali ni kutokana na mazingira wanayoishi na wengine wamepewa na ndugu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dk Rogers Shemwelekwa aesma kuwa asilimia 70 ya watumishi ni wanawake menejimenti idara tano zinaongozwa na wanawake ambapo wanafanya kazi nzuri ikiwemo kwenye zoezi la ukusanyaji mapato.

Shemwelekwa amesema kuwa wamewawezesha wanawake wenye biashara ndogo ndogo kuunda vikundi ambapo walikuwa hawakopesheki lakini sasa wamekopeshwa bilioni 2 na wanarejesha vizuri.

Naye Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii Leah Lwanji amesema kuwa vikundi 275 vya wanawake vimekopeshwa zaidi ya bilioni 1 ikiwa ni asilimia 94. 

Lwanji amesema kuwa majukwaa yamehamasishwa kuanzishwa miradi ya kiuchumi ili waweze kujikwamua na mpaka sasa zimekopeshwa milioni 70 kwa akinamama wa majukwaa.

Moja ya kikundi ambacho ni cha mfano cha Lulu ya Wajane mwaka jana kilipata mkopo wa shilingi milioni 46 ambapo walipaswa kurejesha mkopo huo kwa miaka mitatu lakini kimeweza kurejesha ndani ya miezi 11.

Kiongozi wa kikundi hicho Kanyenda Mweri amesema kuwa fedha hizo za mikopo isiyokuwa na riba zimewasaidia kuwakwamua kiuchumi na kuweza kutoa ajira kwa wanawake wenzao.

Thursday, March 5, 2026

MAOFISA USAFIRISHAJI WATAKIWA KUUNDA VIKUNDI WAKOPE HALMASHAURI





MAOFISA Usafirishaji maarufu kama Bodaboda kwenye Mtaa wa Mwendapole B wametakiwa kuunda vikundi ili waweze kukopa vyombo vya usafiri vinavyotolewa na Halmashauri kuachana na mikopo ya taasisi za watu binafsi ambazo zina gharama kubwa.

Aidha alisema kuwa gharama za mikopo ya Halmashauri ni ndogo na marejesho yake ni madogo tofauti na mikopo ya vyombo hivyo kwenye taasisi au watu binafsi.

Hayo yalisemwa na Mwenyekiti wa Mtaa huo Abubakar Matumla wakati wa kikao na waendesha pikipiki wa Mtaa huo na kuwa wanashindwa kufanikiwa kwa kukopa pikipiki kwa riba kubwa.

Matumla alisema kuwa gharama za kukopa pikipiki kwa watu binafsi imekuwa ikiwafanya wasifanikiwe kutokana na gharama kuwa kubwa za mikopo hiyo hivyo hujikuta wanashindwa kujiongezea kipato.

"Serikali imewawekea mazingira mazuri ya mikopo yake kwani mnauwezo wa kukopa pikipiki, bajaji na Toyo kwa gharama nafuu na unarejesha kiasi kilekile ulichokopa na hakuna riba ya mkopo unaokopa hivyo ni wakati wenu wa kujiunga na kuwa na vikundi na mtumie fursa ya mikopo pale Halmashauri fedha zipo za kutosha na vyombo vya moto vipo,"alisema Matumla.

Alisema kuwa yuko tayari kuwasimamia kuhakikisha wanapata mikopo hiyo kwani hapendi kuona waendesha pikipiki wakitaabika ili hali kuna sehemu wanaweza kukopa bila ya kuwa na marejesho makubwa pia aliwataka kutoa taarifa kwa wale wanaojihusisha na vitendo vya kiuhalifu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa waendesha pikipiki hao Abdulatif Mbonganga alisema kuwa tayari wameshaanzisha kikundi kimoja na tayari kimeshasajiliwa kikiwa kinasubiri wakati ukifika waende kukopa.

Mboganga alisema kuwa changamoto kubwa kwao ni kukosa vyombo vya usafiri hali inayowabidi kukopa vyombo hivyo kwenye taasisi za watu binafsi ambazo zinagharama kubwa na kujikuta wakitumia nguvu kubwa kwenye marejesho.

Moja ya maofisa usafirishaji Salum Msaku alisema kuwa changamoto ya uhalifu inatokana na baadhi yao kuwapa ma "day worker" hasa nyakati za usiku ambapo wanawaletea sifa mbaya.

Msaku alisema kuwa ili kudhibiti hali hiyo kila mwendesha pikpiki aendeshe pikipiki yake na siyo kumpa mtu mwingine pia wahakikishe wanavaa riflector ambazo zitawatambua kwa namba zinazoandikwa mgongoni inakuwa rahisi katika ufuatiliaji.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Mtaa wa Miembe Saba B Nuru Awadh alisema kuwa wanapaswa kuwa na ushirikiano na kuunda vikundi vya bodaboda ili wapate mikopo nafauu.

Awadh aliwataka wajiheshimu na wasijiunge na makundi mabaya kwani Rais amewapa kipaumbele vijana katika uongozi na sehemu mbalimbali ili wawe vinara kwa utendaji kazi.

Tuesday, March 3, 2026

KAMBI SAMIA ARDHI KLINIKI YAANZA PWANI

HALMASHAURI ya Manispaa Kibaha kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeweka kambi ya Samia Ardhi Kliniki ikiwa ni maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani.

Akizungumza kuhusu huduma zinazotolewa katika kambi hiyo ya siku sita, Kamishna Msaidizi wa Ardhi Mkoa wa Pwani Rugambwa Banyika alisema kuwa kliniki hiyo inalenga kutoa ushauri wa kisheria kuhusu masuala ya ardhi.

Banyika alisema kuwa shughuli nyingine zitakuwa ni kufanya makadirio ya pango la ardhi, kuandaa nyaraka za umiliki, kujibu changamoto za upimaji, urasimishaji, upangaji miji na michoro pamoja na kutoa hati za umiliki.

"Wananchi wote wanakaribishwa ili kupata huduma zote zihusiananazo na masuala ya ardhi ambapo huduma zimesogezwa ili kila mwananchi apate fursa katika kipindi hichi kuanzia Machi 2 hadi 7 kuelekea kilele cha siku ya Wanawake Duniani Machi 8,"alisema Banyika. 

Alisema kuwa kambi hiyo maalum ina lengo la kushughulikia changamoto mbalimbali za ardhi kwa wananchi hususan wanawake na wasichana katika masuala yanayohusiana na ardhi.

Baadhi ya wananchi Mariam Juma na Ahmed Abdala wameishukuru Serikali kwa kusogeza huduma hizo karibu yao na kueleza kuridhishwa na namna wanavyohudumiwa na wataalamu wa ardhi kwani wanatoa elimu ya kujitosheleza.

Kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani kimkoa kinatarajiwa kufanyika Machi 8 2026 katika Uwanja wa Ujamaa Kata ya Umwe Tarafa ya Ikwiriri Halmashauri ya Mji wa Rufiji ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge.

Sunday, March 1, 2026

PWANI YAANZA MAANDALIZI MAADHIMISHO SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

MKOA wa Pwani umeanza maandalizi ya Siku ya Wanawake Duniani ambapo kilele cha maadhimisho kimkoa yatafanyika Machi 8, 2026 katika Uwanja wa Ujamaa, Kata ya Umwe, Tarafa ya Ikwiriri, Halmashauri ya Mji Rufiji. 

Mratibu wa maadhimisho hayo, Roseline Kimaro, amesema mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge.

Akizungumza kuhusu maandalizi, Kimaro amesema maadhimisho ya mwaka huu yanaongozwa na kaulimbiu isemayo, “Haki kwa Wanawake na Wasichana: Msingi wa Maendeleo Jumuishi Dira 2050,” ikisisitiza umuhimu wa usawa wa kijinsia na haki kama nguzo ya maendeleo endelevu. 

Amesema lengo ni kutambua na kuenzi mchango wa wanawake katika nyanja za kijamii, kisiasa na kiuchumi, sambamba na kuimarisha mapambano dhidi ya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia.

Amebainisha kuwa kuanzia Machi 1 hadi 7 kutafanyika shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo utoaji wa elimu kwa umma na kampeni za uhamasishaji kuhusu usawa wa kijinsia,  kilele cha maadhimisho Machi 8. 

Ameongeza kuwa maandalizi yanaendelea vizuri na kutoa wito kwa wananchi na wadau wa maendeleo kujitokeza kwa wingi kushiriki na kuunga mkono jitihada za kulinda na kuimarisha haki za wanawake na wasichana.

Friday, February 27, 2026

TRA PWANI KUBADILI UTARATIBU UKUSANYAJI KODI BANDARI YA BAGAMOYO

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Pwani kuanza utaratibu mpya ukusanyaji mapato Bandari ya Bagamoyo Machi Mosi mwaka huu.

Akizungumza na wafanyabiashara wa mafuta ya kula kwenye Bandari hiyo Meneja wa TRA Mkoa huo Masawa Masawa alisema kuwa changamoto iliyopo ni malalamiko ya wafanyabiashara kulalamikia bei ya kodi ya mafuta yanayotoka Zanzibar.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Shaibu Ndemanga alisema kuwa wananchi wengi wanategemea biashara ya mafuta na kuna wadau wengi wanategemea shughuli zinazohusiana na biashara ya mafuta.

Naye Diwani wa Kata ya Dunda Amiry Mpwimbwi alisema kuwa eneo hilo la Bandari linatoa ajira zaidi ya 8,000 hivyo kutokana na shughuli kutofanyika kumesababisha serikali kukosa mapato.

Mwenyekiti wa wafanyabiashara wa Mafuta kwenye Bandari hiyo Shaban Hamsini alisema kuwa hali imeshakuwa mbaya kwani wanategemea shughuli hizo kuendeshea maisha yao.

Saturday, February 21, 2026

MATUMLA AWATAKA WANANCHI KUSHIRIKIANA NA SERIKALI ILI KUTATUA CHANGAMOTO


MWENYEKITI wa Mtaa wa Mwendapole B Manispaa ya Kibaha Abubakar Matumla ameendelea na ziara ya kutafutia majawabu changamoto zinazowakabili wananchi wa Mtaa huo.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Matumla amesema ziara hiyo inaifanya kwa kutembelea Balozi zote zilizopo kwenye Mtaa huo ili kubaini changamoto ili kupeleka sehemu husika kwa utatuzi.

Changamoto ambazo zimekuwa zikijirudia ni pamoja na miundombinu ya barabara, uhalifu, uvutaji wa bhangi, maji, elimu ya msingi.

Matumla amesema kuwa kutokana na changamoto hizo watawasiliana na mamlaka husika ili wazifanyie kazi changamoto hizo ili ziweze kupatiwa majawabu.

Akizingumzia uhalifu amesema kuwa tayari baadhi ya maeneo yameainishwa kuwa ni kitovu cha uhalifu pamoja na matumizi ya dawa za kulevya aina ya bhangi.

"Tayari tumeshaweka mikakati ya kudhibiti uhalifu kwa kushirikiana na Polisi Kata ili kuwakama wahalifu hao pia ni kufanya doria za kushtukiza ambapo baadhi ya wahalifu wanajificha kwenye Bodaboda ambapo tayari mipango ya kuwatambua inafanyika,"amesema Matumla.

Amesema baadhi ya maeneo kuna changamoto ya upatikanaji wa maji, miundombinu ya barabara imeharibika lakini hata hivyo Mtaa huo umepata barabara moja ambayo itajengwa lami.

"Kwa upande wa elimu ya Msingi changamoto kubwa ni uhaba wa madawati na vyumba vya madarasa ambapo Manispaa ya Kibaha imetoa madawati 20 ambayo yatasaidia kukabiliana na changamoto ya upungufu wa madawati,"amesema Matumla.




DIWANI TANGINI ATOA POLE MTOTO ALIYENUSURIKA KIFO KWA KUSOMBWA NA MAJI NA WALIOEZULIWA PAA ZA NYUMBA ZAO

DIWANI wa Kata ya Tangini Antony Milao ametoa pole kwa wananchi waliokumbwa na kadhia ya mvua ikiwemo ya mwanafunzi Morhat Abdala (9) kunusurika kifo baada ya kusombwa na maji akitoka shuleni.

Mvua hiyo iliyonyesha jana jioni ilileta athari kwa baadhi ya wakazi wa Mtaa wa Machinjioni Kata ya Tangini ambapo nyumba mbili na Machinjio ya mbuzi ambapo mapaa yaliezuliwa baada mvua kubwa kunyesha ikiambatana na upepo mkali kwenye Mtaa huo.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutokea matukio hayo Milao amesema kuwa mwanafunzi huyo ambaye amepumzishwa kwenye Kituo cha Afya Mkoani akipatiwa matibabu anaendelea vizuri.

Milao amesema anamshukuru Mungu kumnusuru mtoto huyo ambaye anasoma darasa la nne Shule ya Msingi Maendeleo akiwa anatoka shule akiwa na mwenzake waliteleza wakati wakivuka kalavati na kusombwa na maji kabla ya wasamaria wema kuwaokoa.

"Pia nilimtembelea Mzee Boniface Mpanda ambaye nyumba yake imeezuliwa paa na nyumba ya Jackson Sellu ambaye hakuwepo nitawasiliana naye pamoja na sehemu ya paa la Machinjio jambo la kushukuru hakuna madhara kwa binadamu zaidi ya mapaa kungoka nimewashika mkono wale waliopata athari hizo ili waweze kutengeneza nyumba zao ili waendelee na maisha yao,"amesema Milao.

Mama wa mwanafunzi aliyesombwa na maji Fatuma Juma amesema kuwa alipata taarifa toka kwa wasamaria wema kuwa mwanae yuko Hospitali baada ya kusombwa na maji baada ya mvua kubwa kunyesha.

Juma amesema anamshukuru Mungu kwani mwanae kwa sasa anaendelea vizuri baada ya kupatiwa matibabu na anawashukuru wasamaria wema kumuokoa mwanae na kumuwaisha hospitali.

Naye Mzee Boniface Mpanda ambaye nyumba yake imeezuliwa paa amesema kuwa alikuwa ndani wakati mvua inanyesha mara akashtukia paa linarushwa na upepo mkali na vitu vyake vyote kulowa.

Mpanda anasema majirani walimsaidia kutoa vitu vyake na kuviweka kwenye mazingira salama wanatoa shukrani zao kwa majirani kwa kutoa msaada na diwani jinsi alivyojitoa kuwasaidia.

Kwa upande wake jirani ambapo nyumba hizo mbili zilizoezuliwa paa Remminister Komanga amesema kuwa mvua hiyo ilinyesha na ilikuwa na upepo mkali na kuezua mapaa hayo pamoja na kuangusha sehemu ya ukuta wake uliozungushiwa kwenye nyumba yake.

Komanga amesema upepo huo ulikuwa ni kama kimbunga na ulikuwa ni sehemu hiyo tu kwani maeneo mengine hakukuwa na upepo zaidi ya mvua kuwa tu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Machinjioni Aidan Saimon amesema kuwa baada ya kutokea madhara hayo waliwasiliana na diwani ili waangalie namna ya kuwasaidia wananchi hao.

Simon amesema kuwa alipewa maagizo na diwani kuhakikisha vifaa vyote vya upauaji atakavyovitoa vinatumika kwa haraka ili nyumba ya Mzee Mpanda ipauliwe upya na atawasiliana na Sellu kuona atamsaidiaje ambapo vyumba vyake viwili vimeezuliwa na upepo.


 

Thursday, February 19, 2026

ATAKA MASLAHI KWA WAFANYAKAZI WA MAJUMBANI

JAMII imetakiwa kuheshimu ajira ya wafanyakazi wa majumbani kwani nitaaluma kama zilivyo taaluma zingine kwa kuifanya kuwa yenye staha kwani ni sehemu ya ustawi wa jamii na ukuzaji wa uchumi.

Hayo yalisemwa Jijini Dar es Salaam kwenye ukumbi wa Confucius wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na Rashid Ally Salim Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kazi na Uwekezaji Zanzibar wakati akifungua mkutano wa mradi wa Urasimishaji wa kitaaluma kwa wafanyakazi wa majumbani Tanzania.

Salim alisema kuwa jamii inapaswa kuona kazi za nyumbani ni taaluma kwa kuzingatia maslahi na haki za msingi za mfanyakazi kwani anaiendeleza jamii.

"Hawa ni watu muhimu sana kwani wanatunza familia zetu pale tunapokuwa kazini au kwenye majukumu mengine ya kimaendeleo hivyo tuwape heshima yao,"alisema Salim.

Alisema kupatiwa mafunzo ya ujuzi kupitia vituo vya VETA ni moja ya vitu vitavyoweza kuwasaidia katika maisha yao kwani ujuzi huo utakuwa ni mkombozi kwao na utawasaidia kujitambua na kujiamini.

Naye mwakilishi kutoka Veta Abdala Ulomi alisema kuwa tayari wametoa mafunzo ya ujuzi kwa wafanyakazi wa majumbani 1,280 kwenye vyuo sita vya Bara na vitatu vya Zanzibar na mtaala wao tayari umeshaandaliwa.

Ulomi alisema kuwa wanarasimisha mafunzo kwa wafanyakazi wa majumbani kwani mahitaji yao ni makubwa ndani na nje ya nchi na hiyo itakuwa taaluma kama taaluma zingine.

Kwa upande wake Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Profesa Rose Upor alisema kuwa asilimia 95 ya wafanyakazi wa majumbani ni wanawake ambapo kuna umuhimu wa kuboresha mazingira ya hali za kijinsia.

Upor alisema kuwa suluhisho ni kukuza utu na mazingira bora ya kazi ambapo kuna haja ya kushughulikia tafiti zinazofanywa ili kuleta usawa na kuepukana na vitendo vya ukatili wa kijinsia.

Mkurugenzi wa Shirika la CVM Tanzania Magesa Nathaniel alisema kuwa wamekuwa wakitekeleza mradi wa miaka mitatu ambao umefika mwisho wa kukuza kazi za staha na haki kwa wafanyakazi kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na wadau mbalimbali wa ndani na nje.

Nathaniel alisema kuwa baadhi ya kazi walizokuwa wakifanya ni kuwajengea uelewa na kuwajengea uwezo kuwaunganisha na chama cha wafanyakazi wa majumbani CHODAWU katika utetezi wa haki zao.

Asteria Gerald mwakilishi wa CHODAWU alisema kuwa kutambuliwa kwa kazi zao kutasababisha kupata heshima ulinzi na stahiki nyingine kwani bado wananyanyaswa wanafanyiwa ukatili na wanafanya kazi kwa muda mrefu.

Gerald alisema kuwa wanaomba kuridhiwa kwa mkataba namba 189 wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) ambayo inalinda haki hadhi usalama wa wafanyakazi wa majumbani.

Mkurugenzi wa Taasisi za Taaluma za Kijinsia Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Dk Sara Kisanga alisema kuwa wafanyakazi wa nyumbani wanapaswa kutambuliwa na kulindwa na kuendelezwa kiujuzi.

Kisanga alisema kuwa wataalamu wanaotoka chuoni hapo wanawezesha jamii ili kuleta mabadiliko chanya ili kuwa kazi ambazo zina staha na kuzingatia haki za binadamu.

MADIWANI MANISPAA YA KIBAHA WAPITISHA BAJETI YA 2026/2027 YA TSH BILIONI 68.7 KWA KISHINDO

Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha mkoani Pwani wamepitisha kwa kishindo bajeti ya mwaka wa fedha 2026/2027 yenye jumla ya Shilingi Bilioni 68.7 katika Baraza Maalum la Madiwani lililofanyika katika Ukumbi wa Manispaa ya Kibaha.

Akizungumza wakati wa kupitisha bajeti hiyo, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kibaha, Dkt. Mawazo Nicas, amesema bajeti hiyo ni chachu ya maendeleo kwa wananchi na imezingatia mahitaji halisi ya Halmashauri.

“Bajeti hii imepitia kamati zote, imejadiliwa na kuboreshwa. Ni wajibu wetu kuipitisha ili ikalete maendeleo kwa wananchi wetu,” amesema Dkt. Nicas.

Diwani wa Kata ya Kibaha, Omary Bula, amesema bajeti hiyo imeandaliwa kwa ushirikishwaji wa madiwani wote na kuwataka wajumbe kuipitisha kwa maslahi ya wananchi.

Awali akiwasilisha rasimu ya bajeti hiyo, Naibu Meya wa Manispaa ya Kibaha, Aziza Mruma, amesema Halmashauri imekisia kutumia kiasi hicho cha Shilingi Bilioni 68.7, ikiwa ni ongezeko la asilimia sita ukilinganisha na bajeti ya mwaka 2025/2026.

Kwa mujibu wa Mruma, katika mchanganuo wa bajeti hiyo, mapato ya ndani yanatarajiwa kuwa Shilingi Bilioni 17.8, miradi ya maendeleo Shilingi Bilioni 8.7, huku asilimia 60 ya mapato ya ndani ikielekezwa kwenye miradi ya maendeleo na asilimia 40 kwenye matumizi ya kawaida.

Aidha, Shilingi Bilioni 1.4 zimetengwa kwa ajili ya mikopo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu.

Katika mwaka huo wa fedha, Halmashauri inatarajia kujenga kituo kimoja cha afya na zahanati mbili, pamoja na kutekeleza miradi ya kimkakati yenye thamani ya Shilingi Bilioni 1.3. Miradi hiyo ni pamoja na ujenzi wa maegesho ya malori yenye thamani ya Shilingi Milioni 242.3, kituo cha kibiashara Mbonde, na ujenzi wa kiwanda cha kusindika nyama chenye thamani ya Shilingi Milioni 524.7.

Baada ya majadiliano, madiwani kwa pamoja waliipitisha bajeti hiyo kwa kauli moja, wakiahidi kusimamia utekelezaji wake ili kuhakikisha inaleta tija na maendeleo kwa wananchi wa Manispaa ya Kibaha.

Monday, February 16, 2026

NMB WATOA MILIONI 300 MAONYESHO YA MIFUGO

BENKI ya NMB imeingia mkataba wa udhamini wa maonyesho ya mifugo ya (Tri-Nations Livestock Expo) kwa kiasi cha shilingi milioni 300 kwa kipindi cha miaka mitatu.

Mkataba huo umeshuhudiwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dk Fabian Madele kwenye Shamba la Mifugo la Mbogo lililopo Ubena Halmashauri ya Chalinze Wilaya ya Bagamoyo ambapo maonyesho hayo mwaka huu yatafanyika Juni 19 hadi 21.

Madele alisema kuwa maonyesho hayo ni muhimu kwani kwani yanaleta tija kwenye ufugaji kuimarisha ushirikiano kukuza teknolojia kwenye sekta ya ufugaji kukuza masoko ya ndani na nje kwani soko la nje ni kubwa sana.

"Malengo ifikapo 2030 kufikia uuzaji wa tani 50 kwa soko la nje ambalo ni kubwa sana hasa la Mshariki ya Kati na China hivyo lazima tutumie fursa kama hizi kuboresha ufugaji wetu ili uakisi uwingi wa mifugo yetu,"alisema Madele.

Alisema kuwa Tanzania ni ya pili kwa kuwa na mifugo mingi ikiwa na ngombe zaidi ya milioni 35 ma mbuzi milioni 28 hivyo lazima tafsiri ya idadi iendane na mapato.

"Tuwavutie vijana ili wajikite kwenye ufugaji kwani endapo nguvu itawekezwa itainua uchumi wa nchi na ili kufika huko ni kufuga kwa utaalamu kwani maofisa mifugo wamesambazwa kila mahali kikubwa ni kujenga mahusiano mazuri,"alisema Madele.

Kwa upande wake mwakilishi wa benki hiyo kupitia Mkuu wa Idara ya Kilimo Biashara wa Benki ya NMB Nsolo Mlozi alisema kuwa mwaka jana walidhamini maonyesho hayo kwa kiasi cha milioni 30 ambayo hufanyika kila mwaka.

Mlozi alisema kuwa udhamini huo ni wa miaka mitatu na ni sehemu ya kuboresha sekta hiyo ya ufugaji ambapo pia hutoa fursa za mikopo kwa wafugaji ambapo hadi sasa imetoa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 130.

Alisema kuwa mbali ya kutoa mikopo pia inatoa elimu ya fedha, ushauri na masoko kwa wafugaji ili kuweza kukabiliana na changamoto mbalimbali ambapo imeweka mameneja mahusiano wanaoshughulikia wafugaji.

Naye Mkurugenzi wa Shamba la Mifugo la Mbogo Naweed Mulla alisema kuwa maonyesho hayo yamekuwa na mafanikio makubwa ambapo wafugaji wengi walijitokeza kushiriki na mwaka huu wataongezeka zaidi wakiwemo wafugaji toka nchi mbili jirani.

Mulla alisema kuwa mwaka huu wameongeza kipengele cha ufugaji wa kuku kwa upande wa wanawake ambapo kutakuwa na mshindi ambaye atatambulika kama Malkia wa ufugaji.

Mwenyekiti wa Chama Cha Wafugaji Mrida Maroche alisema kuwa wanapongeza uwekezaji unaofanyika kwenye mifugo kwani unapandisha thamani ya mifugo yao na watatumia fursa mbalimbali ili kuongeza uzalishaji kwa kuzingatia viwango ili kukabili soko la nje.

Maroche alisema kuwa mfano mzuri ni baadhi ya ngombe waliopo kwenye Shamba la Mbogo ngombe wa miaka miwili ana uzito wa kilogramu 350 na ndama wa miezi mitano ana uzito wa kilogramu 180 ambapo hayo ni mabadiliko makubwa.


GOOD NEWS FOR TANZANIA DIGITAL CONTENT CREATORS AS NEW LICENCE FEES ANNOUNCED

The Government has announced a historic measure that could significantly transform the landscape of Tanzania’s digital content industry.

Speaking at the Annual Broadcasting Service Providers Conference (ABC 2026) in Dodoma, the Deputy Minister for Information, Culture, Arts and Sports, Hamisi Mwinjuma, revealed that the licence fee for online content creators has been reduced from TSh 500,000 to just TSh 50,000, with an application fee of only TSh 10,000.

This represents a reduction of more than 90 per cent — a move widely interpreted as opening a new door for young innovators, bloggers, and digital creators who had previously struggled with the high cost of compliance.

The decision follows nearly a year of strategic consultations between the Tanzania Bloggers Network (TBN) and the Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA), aimed at addressing financial barriers that had constrained the growth of digital journalism and online content production in the country.

In addition, licence fees for Online Content Aggregators have been reduced from TSh 1,000,000 to TSh 100,000.

A new “Amateur” category has also been introduced specifically for emerging young creators, enabling them to formalise their activities and nurture their talents without heavy financial burdens.

Within the broader context of a rapidly expanding digital economy, this decision is expected to stimulate employment, creativity, and tax revenue generation — in line with the development vision championed by President Samia Suluhu Hassan.

If effectively implemented, these reforms may well mark the beginning of a new chapter for Tanzania’s digital creative sector.

NEEMA KWA WATENGENEZA MAUDHUI YA KIDIJITALI ADA MPYA ZA LESENI ZIKITANGAZWA

 

Serikali imetangaza hatua ya kihistoria inayoweza kubadili sura ya tasnia ya maudhui ya kidijitali nchini. Kupitia tamko lililotolewa katika Mkutano wa Mwaka wa Watoa Huduma za Utangazaji (ABC 2026) jijini Dodoma, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamisi Mwinjuma, amesema ada ya leseni kwa watoa maudhui mtandaoni imeshushwa kutoka Sh500,000 hadi Sh50,000, huku ada ya maombi ikiwa Sh10,000 pekee.

Ni punguzo la zaidi ya asilimia 90, hatua ambayo wengi wameitafsiri kama mlango mpya kwa vijana wabunifu, wanablogu na watengeneza maudhui waliokuwa wakikwama kwa gharama.

Hatua hiyo imekuja baada ya mazungumzo ya karibu mwaka mzima kati ya Tanzania Bloggers Network (TBN) na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), yakilenga kuondoa vikwazo vilivyokuwa vikizuia ukuaji wa sekta hii.

Zaidi ya hayo, ada ya wakusanyaji wa maudhui (Online Content Aggregators) imeshuka kutoka Sh1,000,000 hadi Sh100,000. 

Aidha, kundi jipya la “Amateur” limeanzishwa mahsusi kwa vijana wanaochipukia, likiwawezesha kujisajili rasmi bila mzigo wa kifedha.

Kwa muktadha wa uchumi wa kidijitali unaokua kwa kasi, uamuzi huu unaweza kuwa kichocheo kikubwa cha ajira, ubunifu na mapato ya kodi kwa taifa, kama yalivyo maono ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.

Saturday, February 14, 2026

NEEMA YA KIDIJITALI: Serikali Yashusha Ada kwa Wanablogu, TCRA Yazindua Redio ya Kisasa 'DSB'

 

SERIKALI imetangaza neema ya kihistoria kwa wanablogu, vijana wabunifu, na watoa maudhui mtandaoni nchini kwa kupunguza ada za leseni kwa kiwango kikubwa, hatua inayolenga kuchochea ukuaji wa uchumi wa kidijitali na kurasimisha shughuli za wahabarishaji wa mitandao.

Hatua hiyo imekuja kufuatia utafiti wa kina na mikutano ya kimkakati ya takribani mwaka mzima kati ya mtandao wa Tanzania Bloggers Network (TBN) na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), ikielezea vikwazo vya gharama vilivyokuwa vikikwaza uandishi wa habari za kidijitali nchini.

Akizungumza katika ufunguzi wa Mkutano wa Mwaka wa Watoa Huduma za Utangazaji (ABC 2026) jijini Dodoma leo, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamisi Mwinjuma, amesema ada ya leseni kwa watoa maudhui mtandaoni imeshushwa kutoka Sh500,000 hadi Sh50,000 tu, huku ada ya maombi ikiwa ni Sh10,000 pekee.

Mageuzi hayo pia yamegusa kundi la wakusanyaji wa maudhui (Online Content Aggregators), ambao ada yao imeshushwa kutoka Sh1,000,000 hadi Sh100,000 pekee. Aidha, kundi la "Amateteur" limeanzishwa kwa ajili ya vijana wanaochipukia ili waweze kujitambulisha rasmi na kukuza vipaji vyao bila vikwazo vya kifedha.

Mapinduzi ya Teknolojia ya DSB

Wakati neema hiyo ikitangazwa, Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Dkt. Jabiri Bakari, ametangaza kuanza kwa teknolojia mpya ya utangazaji wa redio ya kidijitali nchini inayojulikana kama Digital Sound Broadcasting (DSB).

Teknolojia hiyo itaanza kufanya kazi katika mikoa mitano ya majaribio ya Dar es Salaam, Dodoma, Mwanza, Arusha, na Mbeya, lengo likiwa ni kuongeza ubora wa sauti na huduma za utangazaji nchini.

"Tumekamilisha maandalizi yote ya kiudhibiti na watoa huduma wa miundombinu wameshapatikana. Hii ni hatua kubwa ya kuendana na mabadiliko ya teknolojia duniani na kuimarisha utangazaji, hususan maeneo ya vijijini," alisema Dkt. Bakari.

Utafiti: Redio Bado ni Kinara

Katika mkutano huo, Injinia Andrew Kisaka wa TCRA amewasilisha matokeo ya utafiti wa hali ya utangazaji kwa mwaka 2025/2026, ukionyesha kuwa redio inaendelea kuwa chanzo kikuu cha habari kwa asilimia 85 ya Watanzania. Hata hivyo, utafiti huo umebaini ukuaji mkubwa wa matumizi ya intaneti miongoni mwa vijana, ambapo asilimia 45 hupata habari kupitia mitandao ya kijamii kabla ya kusikiliza redio au kutazama televisheni.

Upande wa televisheni, utafiti unaonyesha asilimia 65 ya watazamaji wanatumia ving'amuzi, huku maudhui ya ndani yakipendwa zaidi kwa asilimia 70. Serikali imewahimiza watoa huduma za kienyeji kuwekeza zaidi kwenye majukwaa ya kidijitali (OTT) ili kukidhi mahitaji ya soko la sasa.

Ulinzi wa Hakimiliki na Mikopo

Ili kuhakikisha wanahabari wa kidijitali wanufaika na kazi zao, Serikali imezielekeza taasisi za COSOTA na TCRA kuandaa mpango wa kulinda hakimiliki na kudhibiti uharamia mtandaoni. Aidha, Serikali imeanza kutoa mikopo ya masharti nafuu kwa watengeneza maudhui kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya kisasa vya kufanyia kazi.

Hadi kufikia Desemba 2025, TCRA imetoa jumla ya leseni 707 za utangazaji, zikiwemo 318 za maudhui mtandaoni, jambo linaloashiria kukua kwa uhuru wa habari na demokrasia nchini chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan.

Monday, February 9, 2026

RAIS DK SAMIA SULUHU HASSAN APELEKA TABASAMU SIKONGE

Na Allan Kitwe, Sikonge

RAIS wa Awamu ya Sita wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan amepeleka tabasamu kwa wakazi wa Wilaya ya Sikonge Mkoani Tabora baada ya maji safi na salama kutoka Ziwa Viktoria kufika Wilayani humo.

Shangwe na furaha za wananchi zimelipuka kwenye hafla ya kufungulia maji hayo iliyofanyika juzi katika Kata ya Misheni Mjini Sikonge kwenye eneo lilipojengwa tanki kubwa la kupokelea maji hayo ili yaanze kusambazwa kwa wananchi.

Akizungumza na mamia ya wananchi, wadau wa maendeleo na viongozi mbalimbali wa chama na serikali kwenye hafla hiyo, Waziri wa Maji Mheshimiwa Jumaa Aweso ameeleza kufurahishwa na kazi nzuri ya utekelezaji mradi huo.

Amesema kuwa mradi huo ambao unatekelezwa na Mkandarasi kutoka China kwa gharama ya shilingi bilioni 143 umelenga kufikisha huduma ya maji safi na salama katika Wilaya tatu za Urambo, Kaliua na Sikonge yenyewe.

‘Ndugu zangu wana Sikonge, Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ameleta tabasamu kwenu, alipoingia madarakani, aliahidi kumaliza kero yenu ya maji ili akinamama wasitembee na ndoo kichwani umbali mrefu na leo hii maji yamefika’, amesema.

‘Kazi iliyobakia sasa ni kuyasambaza kwa wananchi, katika hili Wataalamu ongezeni kasi, na kila wananchi atakayetaka kuunganishiwa maji nyumbani kwake hakikisheni ndani ya siku 7 awe amepata maji, si vinginevyo’, ameonya.

Aidha Waziri Aweso amemwagiza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Mhandisi Mwajuma Waziri kuleta timu ya Wataalamu katika Wilaya hiyo ili kushughulikia mradi wa Bwawa la Utyatya ili uanze kufanya kazi ili kusaidiana na mradi huo.

Ameongeza kuwa kila Mtendaji wa Wizara hiyo anapaswa kuwa mwadilifu na mchapa kazi, Mtendaji mbabaishaji hana nafasi, hivi karibuni tutafanya tathmini ya Utendaji wa kila mmoja na kuchukua hatua kwa wanaozembea.

Amempongeza Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Tabora  (TUWASA) Mhandisi Mayunga Kashilimu, RUWASA Mhandisi Hatari Kapufi, Mkuu wa Wilaya Thomas Myinga na Mbunge Amos Maganga kwa kusimamia vizuri utekelezaji mradi huo.       

                                                                                                                                                              

MAFUNZO YA ITIFAKI KWA TAASISI YA SMAUJATA



Wapatiwa mafunzo ya Protocol and Etiquette (Ustarabu na Itifaki za Viongozi) Maadili na Uzalendo kwa watumishi. 

Katika kuhakikisha  taasisi  zinajengewa uwezo wa kiimadili katika kazi 

Mtaalamu wa Kidiplomasia, Uongozi na maadili Ndugu Omary Abdull Punzi amewelekeza  na kuwakumbusha taasisi ya SMAUJATA  katika mafunzo yaliyoandaliwa na taasisi hiyo kufanyika  Februari 7 hadi 8 mwaka 2026  katika Ukumbi wa Chuo Cha VETA Keko Dar es Salaam.


Mafunzo hayo yaliyofunguliwa na Ndugu Salehe Omary Kaimu Mkuu wa Chuo cha VETA  akimwakilisha mkuu wa chuo hiko na kufungwa na Ndugu Fredrick Nelson Rwegasira - Makamu Mwenyekiti   SMAUJATA.

Aidha katika mafunzo hayo yalijikita katika 
Itifaki na Ustarabu wa Viongozi sambamba na maadili

Wednesday, February 4, 2026

JUMUIYA YA WAZAZI PWANI YAADHIMISHA MIAKA 49 YA CCM KWENYE KATA YA TANGINI

JUMUIYA ya Wazazi Mkoa wa Pwani imeadhimisha miaka 49 ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa  kupanda miti kwenye eneo la Shule mpya ya Msingi Tangini.

Aidha Jumuiya hiyo pia ilikabidhi vifaa kwa wagonjwa kwenye Zahanati mpya ya Tangini pamoja na kutoa fedha kiasi cha shilingi 180,000 kwa familia mbili zenye watu wenye ulemavu.

Akizungumza wakati wa kupokea ugeni kutoka Jumuiya hiyo ambapo sherehe hizo zimefanyika kimkoa kwenye Kata ya Tangini Mwenyekiti wa CCM na Diwani wa Kata ya Tangini Antony Mlao amesema kuwa anashukuru kwa kupewa heshima hiyo.

Milao amesema kuwa anaishukuru serikali kwa kuwapatia miradi hiyo ambayo ni muhimu ndani ya jamii kwani imewapunguzia wanafunzi na wananchi kwenda kupata huduma mbali.

"Tunamshukuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia miradi hii na tunaahidi kuitunza ili iendelee kuhudumia wananchi na wanafunzi kwenye Kata yetu na Halmashauri ya Manispaa nzima ya Kibaha,"amesema Milao.

Mgeni rasmi kwenye maadhimisho hayo kimkoa Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Pwani Yusufu Masombola amesema kuwa lengo ni kuwaweka wananchi wote karibu na chama kwa kutembelea sekta mbalimbali.

Masombola amesema kuwa viongozi waweke taratibu za kusikiliza kero za wananchi ili kujenga imani kwao na kila mmoja afanye kazi kulingana na eneo lake.

Naye Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Kibaha Mjini Yahaya Mtonda amesema kuwa viongozi kwa kushirikiana na wananchi wanapaswa kuendelea kuleta maendeleo ili kumuunga mkono Rais Dk Samia Suluhu Hassan.

Mtonda amesema kuwa viongozi na waccm wanapaswa kuendelea na shughuli za chama kama ilivyokuwa zamani kwani huu ni wakati wa kufanya kazi za chama kujiandaa na chaguzi za jumuiya za chama mwaka 2027.

Kwa upande wake Juma Nziajose mratibu wa chakula na lishe kutoka ofisi ya Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha alishukuru kwa msaada uliotolewa na jumuiya hiyo.

Nziajose alisema kuwa vifaa hivyo vitafikishwa kwa walengwa kama ilivyodhamiriwa na jumuiya licha ya kuwa Zahanati hiyo bado haijaanza kufanya kazi lakini watapeleka kwenye Hospitali mbalimbali za Manispaa.

MAADHIMISHO MIAKA 49 YA CCM YAFANYIKA WAZAZI KIMKOA KATA YA TANGINI

JUMUIYA ya Wazazi Wilaya ya Kibaha Mjini imeadhimisha miaka 49 ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa  kupanda miti kwenye eneo la Shule mpya ya Msingi Tangini.

Aidha Jumuiya hiyo pia ilikabidhi vifaa kwa wagonjwa kwenye Zahanati mpya ya Tangini pamoja na kutoa fedha kiasi cha shilingi 180,000 kwa familia mbili zenye watu wenye ulemavu.

Akizungumza wakati wa kupokea ugeni kutoka Jumuiya hiyo ambapo sherehe hizo zimefanyika kimkoa kwenye Kata ya Tangini Mwenyekiti wa CCM na Diwani wa Kata ya Tangini Antony Mlao amesema kuwa anashukuru kwa kupewa heshima hiyo.

Milao amesema kuwa anaishukuru serikali kwa kuwapatia miradi hiyo ambayo ni muhimu ndani ya jamii kwani imewapunguzia wanafunzi na wananchi kwenda kupata huduma mbali.

"Tunamshukuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia miradi hii na tunaahidi kuitunza ili iendelee kuhudumia wananchi na wanafunzi kwenye Kata yetu na Halmashauri ya Manispaa nzima ya Kibaha,"amesema Milao.

Mgeni rasmi kwenye maadhimisho hayo kimkoa Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Pwani Yusufu Masombola amesema kuwa lengo ni kuwaweka wananchi wote karibu na chama kwa kutembelea sekta mbalimbali.

Masombola amesema kuwa viongozi waweke taratibu za kusikiliza kero za wananchi ili kujenga imani kwao na kila mmoja afanye kazi kulingana na eneo lake.

Naye Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Kibaha Mjini Yahaya Mtonda amesema kuwa viongozi kwa kushirikiana na wananchi wanapaswa kuendelea kuleta maendeleo ili kumuunga mkono Rais Dk Samia Suluhu Hassan.

Mtonda amesema kuwa viongozi na waccm wanapaswa kuendelea na shughuli za chama kama ilivyokuwa zamani kwani huu ni wakati wa kufanya kazi za chama kujiandaa na chaguzi za jumuiya za chama mwaka 2027.

Kwa upande wake Juma Nziajose mratibu wa chakula na lishe kutoka ofisi ya Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha alishukuru kwa msaada uliotolewa na jumuiya hiyo.

Nziajose alisema kuwa vifaa hivyo vitafikishwa kwa walengwa kama ilivyodhamiriwa na jumuiya licha ya kuwa Zahanati hiyo bado haijaanza kufanya kazi lakini watapeleka kwenye Hospitali mbalimbali za Manispaa.

JUMUIYA YA WAZAZI MKOA WA PWANI WAFANYA MATENDO YA HURUMA MIAKA 49 YA CCM KATA TANGINI

JUMUIYA ya Wazazi Mkoa wa Pwani imeadhimisha miaka 49 ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kufanya matendo ya huruma kwa jamii kwa kutoa misaada mbalimbali.

Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Yahaya Mtonda amesema kuwa wameamua kufanya hivyo ili kuisaidia jamii kwani ni moja ya majukumu ya Jumuiya hiyo wakati wa maadhimisho hayo Kimkoa ambayo yamefanyika kwenye Kata ya Tangini.

Kwenye tukio la kwanza Jumuiya hiyo imetoa vifaa mbalimbali kwa wagonjwa kwenye ya Tangini ambayo hata hivyo iko kwenye hatua za mwisho kukamilika ambapo vifaa hivyo vitapelekwa kwenye Hospitali zilizopo kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha.

Tukio la pili ni la upandaji wa Miti kwenye Shule mpya ya Msingi Tangini ambapo shule hiyo ni mpya ambayo imeanzishwa mwaka huu ikiwa na wanafunzi 650.

Katika tukio la tatu ilitoa fedha kiasi cha shilingi 80,000 kwa familia ya Catherine Januari ina mtoto mwenye ulemavu Catherine John (12) ambaye hawezi kukaa wala kutembea au kufanya chochote zaidi ya kulala tu.

Tukio la tatu ilitoa fedha kiasi cha shilingi 80,000 kwa Mzee Burhan Rehani ambaye ni mlemavu wa miguu wote ni wa kwenye Mtaa wa Tangini Kata ya Tangini.

Mtonda amesema kuwa aliguswa alipotembelea Kata hiyo na kuahidi kusaidia pale atakapoguswa ambapo alitoa 150,000 na mdau mwingine akaongezea 30,000 ili kusaidia familia hizo zenye uhitaji.

"Tumeamua kufanya hivi ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 49 ya CCM ambapo Kimkoa yamefanyika kwenye Kata ya Tangini ambapo ni sehemu ya maadhinisho hayo,"amesema Mtonda.

Mgeni rasmi kwenye maadhimisho hayo Yusufu Masombola amesema kuwa matukio hayo yanaonyesha jinsi gani chama kinavyoshirikiana na jamii.

Masombola amesema kuwa matukio hayo ni sehemu ya maadhimisho ya chama kutimiza miaka 49 tangu kuanzishwa kwake ambapo matukio mbalimbali yamefanyika.

Amesema kuwa Jumuiya hiyo ihakikishe inafundisha maadili mema kwa watoto na vijana ili wawe na maadili mazuri na kuachana na tabia mbaya zisizofaa.

Naye Mwenyekiti wa CCM na Diwani wa Kata ya Tangini Antony Milao amesema kuwa anaishukuru serikali ya Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia miradi ya maendeleo ndani ya Kata hiyo.

Milao amesema kuwa miradi hiyo muhimu ikiwa ni pamoja na Zahanati Shule ya Msingi na Sekondari itakabili changamoto ya wakazi wa Kata hiyo kupata huduma mbali.