CHAMA Cha Ushirika wa Umwagiliaji Mpunga Ruvu (CHAURU) cha Halmashauri ya Chalinze Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani kimefanikiwa kumchagua Mchujuko Mchujuko kuwa mwenyekiti atakayeongoza kwa kipindi cha miaka mitano.
Kwenye uchaguzi huo ambao ulisimamiwa na Ofisa Ushirika Halmashauri ya Chalinze alimtangaza Mchujuko aliyepata jumla ya kura 214 sawa na asilimia 91.8 kati ya kura 1,165 halali zikiwa 1,162 na kura zilizoharibika ni tatu ambapo mshindi alipaswa kupata angalau asilimia 50 ya kura.
Akitangaza washindi wa uchaguzi huo msimamizi huyo Raphael Kajale amemtangaza makamu wa mwenyekiti ni Otnel Mbura aliyepata kura 186 sawa na asilimia 79.8.
Kajale amewataja wagombea wengine kuwa ni Sade Mwakitalu alipata kura 173 sawa na asilimia 74, Renatha Mwaipopo alipata kura 171 sawa na asilimia 73.3 na Shea Bilali aliyepata kura 154 sawa na asilimia 67 hawa wote wataunda bodi ya ushirika huo.
Amewataja wajumbe wa kamati ya maadili waliochaguliwa ni Moses Polepole, Rajab Mfyome, Theresia Shayo, James Ole Njolay na Zuhura Matimbwa.
Akiwashukuru wajumbe wa mkutano huo mkuu wa uchaguzi uliompa ushindi mwenyekiti mpya Mchujuko amesema kuwa kikubwa atakachokifanya ni kuhakikisha wanaongeza uzalishaji kutoka tani tano za sasa hadi saba mpaka 10 na kukarabati miundombinu.
Awali mwenyekiti aliyemaliza muda wake Chacha Sadala akishukuru amesema pia wamefanikiwa kununua trekta na jembe lake ukarabati wa pampu nne kukarabati mashine mbili za kukoboa mpunga na tayari hekari 800 zimepandwa kati ya hekari 1,800 na hadi itakapofika Juni 30 wakulima wote watakuwa wamepanda mashamba yao.
No comments:
Post a Comment