SHULE ya Sekondari ya Kata ya Maili Moja Bundikani Halmashauri ya Mji Kibaha imefanikiwa kufaulisha wanafunzi wote wa kidato cha nne 375 kufaulu na kuondoa daraja sifuri.
Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Bernard Muyenjwa alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake.
Muyenjwa alisema kuwa ufaulu huo ni asilimia 100 ya wanafunzi waliofanya mtihani wa kidato cha nne waliofanya mitihani yao mwaka jana.
"Wanafunzi 234 wamefaulu kwenda kidato cha tano na vyuo mbalimbali vya kati ambapi ufaulu huo ni sawa na asilimia 65 huku wengine wakisubiri uteuzi wa awamu ya pili,"alisema Muyenjwa.
Alisema kuwa jumla ya wanafunzi waliofanya mtihani walikuwa 375 wasichana wakiwa 218 wavulana 157 ambapo daraja la kwanza walikuwa 22 wasichana tisa wavulana 13.
"Daraja la pili 79 wasichana 53 wavulana 26 daraja la tatu 144 wasichana 73 wavulana 71 na daraja la nne ni 130 wasichana 83 wavulana 47 huku daraja sifuri kukiwa hakuna hata mmoja,"alisema Muyenjwa.
Aidha alisema kuwa mafanikio hayo yalitokana na mshikamano walionao walimu na kujitolea, kusimamia vizuri mipango iliyowekwa ya kufikia ufaulu.
"Ushirikiano kati ya shule, wazazi na bodi, kusimamia nidhamu kwa wanafunzi na kuhimiza walimu kufundisha kwa kasi na mazoezi ya mara kwa mara na ufuatiliaji, ufanyaji wa mitihani kila Jumamosi,"alisema Muyenjwa.
Aliongeza kuwa upande wa nidhamu ni kuweka uzio na walinzi ili kudhiti wanafunzi kutoka bila ya sababu zisizokuwa na msingi bali iwe ya msingi ndipo atoke au muda wa kuingia shuleni.
"Malengo ni kuhakikisha tunapunguza wanafunzi wanaopata daraja la nne na kuongeza ufaulu wa daraja la kwanza wafikie angala 60 au 70 na hilo linawezekana,"alisema Muyenjwa.
Alibainisha kuwa shule yao ambayo ni kinara kwa shule za Kata kwa kufaulisha kwenye Halmashauri ya Mji Kibaha ikiwa inazidiwa na shule ya Tumbi na Kibaha wasichana ambazo ziko chini ya Shirika la Elimu Kibaha.
"Tunaishukuru Serikali kwa kutoa kiasi cha shilingi milioni 120 kwa ujenzi wa vyumba vya madarasa vinne na changamoto zilizopo ni ndogondogo ambazo ziko ndani ya uwezo wetu walimu wapo wa kutosha zaidi ya 100,"alisema Muyenjwa.
Aliwaomba wazazi na wadau kuendelea kutoa ushirikiano ili shule hiyo iendelee kufanya vizuri kwenye matokeo ya kidato cha nne na kufikia malengo ya kuwa na kidato cha tano na sita.
No comments:
Post a Comment