IMEELEZWA watu kuoneana aibu ndani ya familia kumesababisha vitendo vya ukatili kuendelea ndani ya jamii ambapo hali hiyo imezipeleka familia pabaya.
Aidha serikali ya Mkoa wa Pwani imesema kuwa itachukua hatua kali kwa watu wanaowafanyia ukatili watoto washindwe kufikia ndoto zao na kukosa haki zao.
Hayo yamesemwa na Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Shangwe Twamala wakati wa Siku ya Mtoto wa Afrika kimkoa iliyofanyika Mjini Kibaha.
Twamala amesema kuwa baadhi ya taarifa zinaonyesha kuwa wanaofanya vitendo hivyo ni ndugu wa karibu.
"Ukatili unafanywa na ndugu wa karibu ambapo familia zinashindwa kuchukua hatua sababu ya kuoneana Muhali (Aibu) hili hatulikubali,"amesema Twamala.
Akisoma risala ya watoto wa mkoa wa Pwani Evelin Mhema amesema kuwa baadhi ya changamoto ni pamoja kufanyiwa vitendo vya ukatili mimba za utotoni, ubakaji, vipigo na vitendo vingine vinavyowanyima haki zao.
Mhema amesema kuwa watashirikiana na viongozi wakiwemo walimu ili waweze kufikia ndoto zao walizojiwekea kwa kusoma kwa bidii na kutii wazazi na walezi wao.
Kwa upande wake Said Mwinjuma amesema kuwa matumizi ya dawa za kulevya yamekuwa changamoto kwa vijana na kusababisha mmomonyoko wa maadadili.
Naye Mkurugenzi wa Kituo cha Msaada wa Kisheria Kibaha (KPC) Catherine Mlenga amesema kuwa watoto pia nao wajilinde kwa kutotembea usiku na kwenda kwenye mabanda ya video ma kulindana wao kwa wao.
Mlenga amesema kuwa pia wasipokee zawadi au kuomba fedha kwa watu wasiowafahamu na wazazi wawalinde watoto kwa kutokuwa wakali na
No comments:
Post a Comment