MKUU mpya wa Wilaya ya Kisarawe Petro Magoti amesema kuwa atafanya kazi kwa ushirikiano na viongozi waliopo ili kuleta maendeleo kwa wabanchi wa wilaya hiyo.
Magoti ameyasema hayo Mjini Kibaha alipokula kiapo cha kuwa Mkuu wa Wilaya ambapo aliapishwa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge
Amesema kuwa anamshukuru Rais kwa kumpa nafasi hiyo na hilo ni kama deni atalilipa deni hilo alilonalo kwa kuwatumikia wananchi wa Kisarawe katika kutatua changamoto zinazowakabili.
Kunenge amewataka wakuu wa Wilaya zote kuhakikisha wanasimamia mapato kwenye Halmashauri zao ili ziweze kuleta maendeleo kwa wananchi.
Amewataka kutatua changamoto za wananchi kwa wakati na usimamizi kwenye utoaji huduma za afya na maji na usimamizi wa miradi ya elimu, barabara ili fedha zinazotolewa na serikali ziwe na tija.
No comments:
Post a Comment