Wednesday, June 12, 2024

WATU WENYE ULEMAVU WATAKA KUTEULIWA NAFASI NGAZI ZA MAAMUZI

CHAMA Cha Watu Wenye UalbinoTanzania (TAS) kimeiomba serikali iwateue kwenye nafasi za ngazi za maamuzi.

Aidha ametaja nafasi hizo za maamuzi kama vile Uwaziri, Ukuu wa Mikoa na Ukuu wa Wilaya kwani nao wanauwezo kama walivyo watu wengine.

Hayo yamesemwa na Mjumbe wa Bodi ya chama hicho Thomas Diwani wakati akitoa salama za chama kwenye kongamano la kuongeza uelewa juu ya Ualbino lililofanyika kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere Kwa Mfipa Kibaha.

Naye Mkurugenzi kitengo cha huduma kwa watu wenye ulemavu Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu Rasheed Maftah amesema kuwa serikali inaanda sera na miongozo mbalumbali kwa watu wenye ulemavu za kuweka usawa na haki.

Awali mwenyekiti wa Tas Godson Mollel amesema kuwa wanampongeza Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia Hospitali Rufaa ya KCMC kwa kuwapatia kiasi cha shilingi milioni 124 kwa ajili ya kuzalisha losheni zinazotumiwa na watu wenye ualbino.

Kwa upande wake kaimu mkuu wa mkoa wa Pwani Nickson John amesema kuwa watu wenye ualbino wapatao 368 wanapatiwa misaada mbalimbali na zimeundwa kamati za watu wenye ualbino.


No comments:

Post a Comment