WANACHAMA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani wametakiwa wasizitumie taasisi mbalimbali zinazomuunga Mkono Rais na chama kama sehemu ya kupata teuzi za kuwa viongozi.
Aidha zimetakiwa zisitembee mifukoni na baadhi ya watu wanaotaka kuwania nafasi za uongozi bali wawaache waliopo madarakani wamalize muda wao wa uongozi.
Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Katibu wa Siasa na Uenezi Mkoa wa Pwani David Mramba wakati wa mkutano na taasisi hizo.
Mramba amesema kuwa baadhi wanajiunga na taasisi hizo ili waonekane wachaguliwe kwenye nafasi mbalimbali za uongozi kwenye chama na serikali.
Kwa upande wake Katibu Mwenezi wa CCM mkoa wa Ruvuma John Haule alizitaka taasisi hizo kuitumia vizuri mitandao ya kijamii kwa kuelezea mambo mazuri yanayofanywa na awamu ya sita.
Naye Katibu Mwenezi wa CCM mkoa wa Morogoro Zangina Zangina amesema kuwa taasisi hizo zihamasishe wale wenye sifa wajiandae kugombea wakati utakapofika.
No comments:
Post a Comment