Saturday, May 18, 2024

JKT RUVU YAZINDUA BUSTANI YA WANYAMAPORI

MKUU wa Wilaya ya Kibaha Nickson John amezindua bustani ya Wanyamapori ya Kikosi cha  Jeshi cha Ruvu JKT (Wildlife).

John akizindua bustani hiyo iliyopo kwenye eneo la Kikosi  cha 832 KJ Mlandizi Wilayani Kibaha Mkoani Pwani amewataka wananchi kujitokeza kwenda kuangalia wanyama ambao sasa wanapatikana karibu. 

Amesema uwepo wa Mbuga hiyo mbali ya kuwapunguzia gharama wananchi wanaotaka kuangalia wanyama pia itaongeza mapato ya Kikosi hicho na serikali.

Kwa upande wake Mkuu wa Kikosi hicho Kanali Peter Mnyani amesema kuwa wameanza na wanyama wachache lakini watawaongeza ili wawe wengi ambapo watakuwa na fursa ya kupiga picha na wanyama hao.

Mnyani amesema kuwa mwezi Juni wataongeza wanyama wakiwemo Simba ili kuongeza idadi ya wanyama na eneo hilo lina ukubwa wa hekari 70.

Amesema mbali ya kufuga wanyama hao pia wanatunza mazingira kutokana na eneo hilo kuwa na mazingira mazuri na ya asili.


No comments:

Post a Comment