Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Mjini Kibaha katibu wa mashindano hayo Idd Mpingo amesema kuwa michuano hiyo inatarajia kuanza mwezi Juni kwenye uwanja wa Mwanakalenge.
Mpingo amesema kuwa maandalizi yanaendelea vizuri ambapo kwa sasa ni usajili wa timu zitakazoshiriki michuano hiyo ambapo timu ya Kiduli imethibitisha kushiriki michuano hiyo.
Amesema kuwa zawadi kwa mshindi mwaka huu zitakuwa nzuri ikilinganishwa na mwaka jana ambapo mwaka jana mshindi alijinyakulia milioni 3 na mshindi wa pili alijinyakulia milioni 1.5.
Kiingilio cha ushiriki kwa timu ni shilingi 150,000 ambapo pia zawadi zitatolewa kwa mchezaji bora, mfungaji bora na kipa bora lengo likiwa ni kuongeza hamasa kwa wachezaji.
Ametoa wito kwa vilabu ndani na nje ya Mkoa wa Pwani kujitokeza kushiriki michuano hiyo na wanawakaribisha wadhamini kujitokeza kudhamini michuano hiyo.
Ameishukuru serikali na vyama vya soka na waamuzi kwa ushirikiano wanaoutoa kwao katika kufanikisha michuano ambayo imeibua vipaji vingi vinavyotamba kwenye ligi mbalimbali nchini.
No comments:
Post a Comment