Thursday, May 23, 2024

CHONGELA AAPISHWA KUWA DIWANI

DIWANI wa Kata ya Msangani kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Gunze Chongela ameapishwa baada ya kushinda uchaguzi mdogo uliofanyika hivi karibuni kufuatia kifo cha aliyekuwa diwani wa kata hiyo Leonard Mlowe .

Chongela alikula kiapo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Hamis Ally wakati wa kikao cha baraza la madiwani wa Halmashauri ya Mji Kibaha.

Gunze ameahidi kuwatumikia wananchi wa kata hiyo kwa kusimamia miradi ya maendeleo kupitia ilani ya CCM.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Kibaha Mussa Ndomba amemtaka diwani huyo kuebdeleza mazuri yaliyoachwa na mtangulizi wake ili kuleta maendeleo kwenye kata hiyo.

No comments:

Post a Comment