Friday, May 3, 2024

KPC YAWATAKA WANANCHI KUTUMIA KITUO CHAO KUTATUA CHANGAMOTO ZA KISHERIA.

 

WANANCHI wa Halmashauri ya Mji Kibaha wametakiwa kukitumia Kituo cha cha Msaada wa Kisheria (KPC) ili kutatua changamoto zinazohusiana na masuala ya kisheria ili kuokoa muda wa kwenda Mahakamani.


kimeendelea na utoaji elimu na msaada wa kisheria kwa makundi mbalimbali ili kuwajengea ufahamu wa sheria wananchi wa Halmashauri ya Mji Kibaha.

Akizingumza na waandishi wa habari Mjini Kibaha Mkurugenzi wa KPC Catherine Mlenga amesema kuwa baadhi ya masuala ya kisheria yanaweza kutatuliwa kituoni hapo kabla hawajayafikisha Mahakamani.

Mlenga amesema kuwa wananchi wanaweza kutatuliwa changamoto za kisheria na kuokoa muda ambao wangeutumia kwenda mahakamani na kufanya shughuli zao za maendeleo.

Aidha amesema kuwa wanatoa elimu pamoja na msaada kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo serikali kupitia ustawi wa jamii pamoja na mahakama.

Amewataka wananchi wa Kibaha kukitumia kituo hicho ili waweze kusaidiwa pale wanapopata changamoto za kisheria na wasifumbie vitendo vya ukatili ndani ya jamii kwa kutoa taarifa.

Mwisho.

No comments:

Post a Comment