WAKAZI wa Mtaa wa Zegereni Wilayani Kibaha Mkoani Pwani wamejitolea kujenga ofisi ya kisasa ya Mtaa ili kuboresha utoaji huduma kwa wananchi.
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye eneo la ujenzi Mwenyekiti wa Mtaa huo Rashid Likunja amesema ofisi iliyopo ni ya zamani ambapo imejengwa miaka 20 iliyopita.
Naye Mtendaji wa Mtaa huo Femida Ayubu amesema kuwa wameweka utaratibu wa kila kaya kuchangia ujenzi huo ambao hufanywa kila Jumatano.
Kwa upande wake moja ya wananchi Leah Chambo amesema kuwa wanashirikiana na mtaa kwa kujitolea shughuli mbalimbali za maendeleo kwenye mtaa wao ili huduma ziwe bora.
No comments:
Post a Comment