MTAA wa Uyaoni Kata ya Maili Moja Wilayani Kibaha umeishukuru serikali kwa kujenga madarasa saba yenye thamani ya shilingi milioni 140 kwenye Shule ya Sekondari ya Kata ya Maili Moja Bundikani kwa kipindi cha miaka mitatu na kuifanya iwe na miundombinu mizuri na kuongeza ufaulu.
Aidha serikali ilitoa fedha ambazo zimejenga vyoo matundu 18 pamoja ujenzi wa darasa moja ambalo kwa sasa liko hatua ya umaliziaji na mwaka huu imefuta daraja sifuri kwa kidato cha nne ambapo mtaa huo ni mlezi wa shule hiyo.
Mwenyekiti wa Mtaa huo Fadhil Kindamba amesema kuwa ufaulu mwaka huu wanafunzi 22 wamefaulu daraja la kwanza, 73 daraja la pili 144 daraja la tatu na 130 daraja la nne.
Kindamba amesema ufaulu huo umetokana ushirikiano uliopo baina ya walimu, wazazi na wadau wengine wa elimu na kuboreshwa kwa miundombinu ya shule.
Katika hatua nyingine mtaa huo unatarajia kujenga vibanda viwili vya biashara kwa ajili ya kuvipangisha ili kujiongezea mapato na tayari wana matofali 500 kwa ajili ya kuanzia ujenzi utakaoanza hivi karibuni.
Amesema pia wanatarajia kuanzisha mnada ambapo tayari eneo limeshapatikana baada ya mwananchi mmoja kwenye mtaa huo kujitolea eneo kwa ajilo hiyo.
No comments:
Post a Comment